Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 61,192
- 99,924
What a shame? Majivuno, kuringa, kujikweza, kujiona wao ndio wao, kumbe kuna Malaika wasio na hatia wanakaa chini! Mnatoza tozo mjenge Barbara na watoto wetu wakae chini? Hivi tuna akili kweli sisi? Yaani ununue ndege kwa pesa cash na huku Wanao wanashinda darsani wakiwa wamekaaa chini?
Tuna tatizo kubwa sana akilini mwetu, tuna IQ ndogo sana sana
====
Sengerema.Wanafunzi zaidi ya 400 wa darasa la nne na tano wanakaa chini na kutumia chumba kimoja cha darasa kwenye Shule ya Msingi Bugumbikiso iliyopo kata ya Chifunfu wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Paul Vicent amesema shule hiyo ina walimu 30 na wanafunzi 3, 118 kuanzia darasa la awali hadi la saba.
Amesema sababu ya kukaa chini ni idadi kubwa ya wanafunzi licha ya Serikali kutoka Sh71 milioni kujenga vyumba vitatu vya madarasa na matundu 10 ya vyoo.
Mbunge wa Sengerema, Hamisi Tabasamu amesikitishwa na hali hiyo licha ya kutoka ushauri kuwa fedha hizo zitumike kujenga shule nyingine ili kuondoa msongamano huo.
Tabasamu amesema ushauri wake ulipuuzwa na viongozi wa Halmashauri hiyo huku akimnyooshea kidogo ofisa elimu msingi Halmashauri ya Sengerema, Donalt Bunonosi kuwa ndiye aliyesababisha hali hiyo kwa kupuuza ushauri.
shulepiccc
ADVERTISEMENT
Naye Bunonosi amesema hakuwa na maelekezo ya fedha kutumika kujenga shule nyingine bali alikuwa na maelekezo ya kujenga vyumba vitatu vya madarasa na matundu 10 ya vyoo.
Mwenyekiti wa kijiji cha Chifunfu, Dominic Tilosahu amesema wataalamu hawana ushirikiano na wananchi na ndio sababu ya shule hiyo kuendelea kuwa na wanafunzi wanaokaa chini.
Kaimu mkurugenzi Halmashauri ya Sengerema, Ally Salim amesema watazifanyia kazi changamoto za shule hiyo na kuzipatia ufumbuzi.
Tuna tatizo kubwa sana akilini mwetu, tuna IQ ndogo sana sana
====
Sengerema.Wanafunzi zaidi ya 400 wa darasa la nne na tano wanakaa chini na kutumia chumba kimoja cha darasa kwenye Shule ya Msingi Bugumbikiso iliyopo kata ya Chifunfu wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Paul Vicent amesema shule hiyo ina walimu 30 na wanafunzi 3, 118 kuanzia darasa la awali hadi la saba.
Amesema sababu ya kukaa chini ni idadi kubwa ya wanafunzi licha ya Serikali kutoka Sh71 milioni kujenga vyumba vitatu vya madarasa na matundu 10 ya vyoo.
Mbunge wa Sengerema, Hamisi Tabasamu amesikitishwa na hali hiyo licha ya kutoka ushauri kuwa fedha hizo zitumike kujenga shule nyingine ili kuondoa msongamano huo.
Tabasamu amesema ushauri wake ulipuuzwa na viongozi wa Halmashauri hiyo huku akimnyooshea kidogo ofisa elimu msingi Halmashauri ya Sengerema, Donalt Bunonosi kuwa ndiye aliyesababisha hali hiyo kwa kupuuza ushauri.
shulepiccc
ADVERTISEMENT
Naye Bunonosi amesema hakuwa na maelekezo ya fedha kutumika kujenga shule nyingine bali alikuwa na maelekezo ya kujenga vyumba vitatu vya madarasa na matundu 10 ya vyoo.
Mwenyekiti wa kijiji cha Chifunfu, Dominic Tilosahu amesema wataalamu hawana ushirikiano na wananchi na ndio sababu ya shule hiyo kuendelea kuwa na wanafunzi wanaokaa chini.
Kaimu mkurugenzi Halmashauri ya Sengerema, Ally Salim amesema watazifanyia kazi changamoto za shule hiyo na kuzipatia ufumbuzi.