Aibu kwetu Watanzania sisi ni wanafiki

puza46b

Member
Nov 3, 2010
91
261
Leo nimetumiwa video ya binti mtanzania aliyeiba akiwa anapigwa mawe. Niliishia pale wamemuwekea kuni. Sikuweza endelea angalia.

Nilipofika kazini kuna swali moja likawa linakuja kichwani. Why we Africans, especially Tanzanians don't hold each other to the highest standards? Ingetokea Ulaya that would have been an outrage.

Lakini pia juzi tumewakasirikia South Africa kwa kuchoma Waafrica wenzao.

Sisi ni wanafiki. Na vyombo vya habari Tanzania ni vinafiki, vinaogopa kuwaambia Watanzania ukweli kwamba tuna psycho kwenye jamii yetu. Vinaogopa kuiambia serikali mihimili ya sheria nchini vimefeli kwenye wajibu wao. Vinaogopa kuwaambia wananchi wa Tanzania, haswa wale wanaoshangilia hawana tofauti na walioua Rwanda au waliokaa kimya ndani ya nazi Germany. They are all guilty.

Ningeomba vyombo vya habari vilishikie njugu hili balaa ya hukumu za mitaani kama ambavyo vilitangaza taarifa za ESCROW. Wachomaji na wauwaji wa vibaka au wezi wadogo waone aibu na kujificha kama ambavyo wauwaji wa albino wanajificha sasa.

Nakumbuka dunia ilipoanza kuonyesha mauaji ya albino tulisema hizo ni imani za vijijini. Ikachukua nguvu ya under the same sun project na kina Vic Mtetema kulazimisha serikali ikubali kuna tatizo nchini.

Leo tena tumekamatwa na mifupa. Sisi ni fisi na tunaringa kuwa ni kondoo. Tusijione kutopigana baada ya uchaguzi kunamaanisha kuna amani nchini. Amani ya kweli ni ile inayomfikia hadi mnyonge.

Shame on us.. again..

Tata.
 
Nimeiona hiyo video nikasikitika sana.

Nikaamini kweli Tanzania bado tuna safari ndefu sana ya kwenda.
 
Tunaomba uitume hiyo video humu ili nasi tuione pls! ulichosema uko sahihi kabisa!
 
In USA, Everyone suspect is innocent until he /she is proven guilty in a court of law. But, in Tanzania, it seems that every suspect is GUILTY, and no need to take him /her to the court of law. We, take matters into our own hands and renders our own verdicts. THIS NEEDS TO STOP....

The life of a man is in the blood. Every bloodshed has consequences, guilt or Innocent.
 
Ila wezi nao wanaudhi sana.

Kuwaua siyo sawa ila kuwakata viganja inatosha sana.
 
Dhambi ya wizi ni sawa na dhambi ya uongo mbele za Mungu. Maana kwa Mungu hakuna dhambi kubwa au ndogo, na ndio maana hukumu ya Mungu ni ya haki siku zote.
Kama Mungu akituhukumu leo hii, ni nani atabaki?.
 
In USA, Everyone suspect is innocent until he /she is proven guilty in a court of law. But, in Tanzania, it seems that every suspect is GUILTY, and no need to take him /her to the court of law. We, take matters into our own hands and renders our own verdicts. THIS NEEDS TO STOP....

The life of a man is in the blood. Every bloodshed has consequences, guilt or Innocent.

This same US whose cops shoot unarmed black people?
 
Cha ajabu dada siyo mwizi bali ni boifrendi wake ndio mwizi waliompiga walifanya yao ndo wakamtoa kitaa apigwe Mungu ni mwema lakini nimesikia alipona baada ya kuokolewa na walinzi
 
Nimeiona hiyo video nikasikitika sana.

Nikaamini kweli Tanzania bado tuna safari ndefu sana ya kwenda.

Kwani sheria za sharia zinasemaje kuhusu watu wenye makosa ya wizi na ambapo ushahidi kutoka kwa mwanaume umetolewa?
 
,nafiki ni huyo aliyechukua video badala ya kuripoti sehemu husika ili huyo binti aokolewe siku hizi kuna tabia hata ajali ikitokea badala ya watu kutoa msaada wanakimbilia kupiga picha za video na kuposti kwenye mitandao
 
Hakuna namna sharia ni mwizi kupigwa mawe mpaka kufa,bahati yake alipona
 
inahitajika elimu hapa, wananchi waelimishwe na kuzingatia sheria, vyombo vya dola vitimize wajibu ipasavyo
 
Back
Top Bottom