Leo hii ni karibu miezi miwili na nusu tangu makanisa yachomwe huko Zanzibar na 'watu wasiojulikana'. Na vile vile ni karibu wiki tatu tangu Dr Ulimboka akamatwe na 'watu wasiojulkana na kupigwa vibaya.
Matukio yote mawili jeshi letu la polisi lilidai kuwa lingefanya uchunguzi wa kina na kuwakamata wahusika na kuwapeleka katika vyombo vya sheria, lakini hata mtu mmoja hajakamatwa.
Hii jamani siyo aibu kubwa kwa jeshi letu la polisi ambalo juzi tu waziri wao, Dr Nchimbi alijidai ni jeshi makini na kwamba yoyote asiyeliamini ana matatizo?
Zanzibar ni sehemu ndogo sana na watu wachache ambao wengi wanajijua. Inakuwaje hadi sasa polisi imeshindwa kuwakamata wahusika wa uchomaji wa makanisa?
Au sasa tuanze kuamini yanayozungumzwa sana, tena sana mitaani kwamba kuna mkono wa serikali katika matukio yote mawili, na polisi kazi yake ni kuilinda tu serikali kwa maovu hayo?
Ukiona mtu anachukia Polisi na vyombo vya dola ujuwe huyo ni mhalifu sugu.
Anaweza kuwepo polisi mmoja mmoja aliyekosa wajibu kama ilivyo kwa mchungaji, askofu, sheikh na Imam kukosa wajibu wake lakini hiyo haina maana kwamba nyumba za ibada makanisa na misikiti sio mahali patakatifu.
Ingependeza kama wewe mwenyewe ungetoa mfano wa ushiriki wako wa kutoa ushirikiano kwa polisi.... ulikwenda kituo kipi cha polisi, kwa kesi ipi na ulikutana na nani kwa ushaidi upi, na kunyimwa haki yako.
kusimulia hadithi za wengine ndiko kunatupeleka hadi kwenye magomvi mengi kama ya kidini na kikabila.
Mhalifu sugu angekuwa uraiani!?
unajua mwizi anapopigwa na wananchi, polisi hajui amkamate nani ikiwa mwizi huyo amekufa au amefariki.
Sasa kwa hili la makanisa ile ni kama riot imetokea, inaweza nkuwa vibaka,au hao uamsho ambao wamekanusha pia inawezekana ni vikosi kazi mbaya vya serikali ,ili kuwadhibiti watu flani kwa kuwasingizia, ila wazanzibari ni wamoja hivyo hilo limefeli, la ulimboka hatujui kinachoendelea kwani waliokuwa na dr katika hatua za mwanzo wapo, mawasiliano yapo, maana kama simu ya uli ilipotea data za simu yake zinakuwepo katika kampuni ya simu ,alimpigia nani alipigiwa na nani kwa wakati huo aliotoweka.
Huwezi kupata mazungumzo lakini wapi na wapi alipiga na kupokea simu utaweza kuzijua namba zilizohusika kama cdm wana mshiko ndani ya makampuni ya simu wanaweza kujua alizungumza na kupigiwa na namba ipi au zipi.
ukitaka kucheka tafuta cv za makamanda wa polisi, ni vichekesho, sio kosa lao. Ni uelewa mdogo + njaa =zezeta.jeshi la polisi la kina chagonja na kova unategemea nini? Ni jeshi la ma-nyinyiemu!
sio rahisi kuandika jambo zuri dhidi ya jeshi la polisi kama unalichukia, post imejaa kulichukua jeshi lote na kila afisa wa jeshi sio fear hata kidogo.
Ni juzi tu polisi walikuja kuniokoa mimi na familia yangu tulipovamiwa na majambazi wakafanikiwa kumuua mmoja na kukamata wawili.
Unajua mwizi anapopigwa na wananchi, polisi hajui amkamate nani ikiwa mwizi huyo amekufa au amefariki.
Sasa kwa hili la makanisa ile ni kama riot imetokea, inaweza nkuwa vibaka,au hao uamsho ambao wamekanusha pia inawezekana ni vikosi kazi mbaya vya serikali ,ili kuwadhibiti watu flani kwa kuwasingizia, ila WaZanzibari ni wamoja hivyo hilo limefeli, la Ulimboka hatujui kinachoendelea kwani waliokuwa na Dr katika hatua za mwanzo wapo, mawasiliano yapo, maana kama simu ya Uli ilipotea data za simu yake zinakuwepo katika kampuni ya simu ,alimpigia nani alipigiwa na nani kwa wakati huo aliotoweka.
Huwezi kupata mazungumzo lakini wapi na wapi alipiga na kupokea simu utaweza kuzijua namba zilizohusika kama CDM wana mshiko ndani ya makampuni ya simu wanaweza kujua alizungumza na kupigiwa na namba ipi au zipi.
vyombo vya usalama vikiamua vinaweza tatizo ni vile vinafanya kazi kwa mashinikizo/maagizo kutoka juu kwa manufaa ya walio juu(viongozi wa juu serikalini)
mhalifu sugu angekuwa uraiani!?
sina imani na jeshi la polis
Ukipata matatizo halafu uwe hauna hela ya kuwahonga polisi utajuta kuzaliwa. Mimi nawachukia polisi na nikipata matatizo nitatoa hela kununua huduma kwa vile huduma pale haitolewi bure, kuingia ndio bure kutoka hadi utoe helaunajua ng'ombe haoni umuhimu wa mkia wake mpaka akiukata nzi wakianza kumsumbua ndo ataukumbuka nina maana kwamba wapo wasiouona umuhimu wa jesh la polisi mpka matatizo yawakute ndo watawakumbuka na kujua umuhimu wake.
iliwachukua miaka 10 majasusi wa CIA kumnasa na kumuua Osama Bin Laden.
Iliwachukua miezi kadhaa hadi tarehe 31 Mei 2012 kwa Jeshi la polisi kumkamata aliyemuua Mwenyekiti wa chadema Arumeru. Muuaji Alikuwa kakimbilia Singida.
Wahalifu wote wana mbinu zao hakuna muda maalum kwa chombo cha dola wa kumkamata mhalifu. Ni mapema sana kusema polisi wameshindwa kuwasaka na
kuwanasa.