Aibu kubwa kwa polisi - hadi sasa wachoma makanisa Zenj na waliomteka Ulimboka hawajakamatwa!

Leo hii ni karibu miezi miwili na nusu tangu makanisa yachomwe huko Zanzibar na 'watu wasiojulikana'. Na vile vile ni karibu wiki tatu tangu Dr Ulimboka akamatwe na 'watu wasiojulkana na kupigwa vibaya.

Matukio yote mawili jeshi letu la polisi lilidai kuwa lingefanya uchunguzi wa kina na kuwakamata wahusika na kuwapeleka katika vyombo vya sheria, lakini hata mtu mmoja hajakamatwa.

Hii jamani siyo aibu kubwa kwa jeshi letu la polisi ambalo juzi tu waziri wao, Dr Nchimbi alijidai ni jeshi makini na kwamba yoyote asiyeliamini ana matatizo?

Zanzibar ni sehemu ndogo sana na watu wachache ambao wengi wanajijua. Inakuwaje hadi sasa polisi imeshindwa kuwakamata wahusika wa uchomaji wa makanisa?

Au sasa tuanze kuamini yanayozungumzwa sana, tena sana mitaani kwamba kuna mkono wa serikali katika matukio yote mawili, na polisi kazi yake ni kuilinda tu serikali kwa maovu hayo?

Vyombo vya usalama vikiamua vinaweza tatizo ni vile vinafanya kazi kwa mashinikizo/maagizo kutoka juu kwa manufaa ya walio juu(viongozi Wa juu Serikalini)
 
Anaweza kuwepo polisi mmoja mmoja aliyekosa wajibu kama ilivyo kwa mchungaji, askofu, sheikh na Imam kukosa wajibu wake lakini hiyo haina maana kwamba nyumba za ibada makanisa na misikiti sio mahali patakatifu.

Ingependeza kama wewe mwenyewe ungetoa mfano wa ushiriki wako wa kutoa ushirikiano kwa polisi.... ulikwenda kituo kipi cha polisi, kwa kesi ipi na ulikutana na nani kwa ushaidi upi, na kunyimwa haki yako.

kusimulia hadithi za wengine ndiko kunatupeleka hadi kwenye magomvi mengi kama ya kidini na kikabila.

Haaahaaa! Polisi nikatafute nini MAMA POROJO? Unafikiri matatizo yanayoikumba Afrika yanaanzishwa na nani? Anyway kitu ambacho najivunia bila shaka wala wasiwasi ni kuwa mimi sio mkabila wala mdini. My life talks for itself...MAMA POROJO, siasa hizi za maji taka zinatupotezea muda. Imefika wakati sasa tuanze kulete hoja na hamasa za kujenga uchumi. kama nguvu tunazotumia kupigana vikumbo kwenye siasa tungezitumia kwenye kujenga nchi, unafikiri tungekuwa wapi?
 
Last edited by a moderator:
Mhalifu sugu angekuwa uraiani!?

Ndio maana anakuwa mhalifu sugu. Angekuwa jela huo uhalifu angeufanya saa ngapi? umesahau, kuna mmoja kakataa hata dhamana ili akawatembelee wenzake jela?
 
unajua mwizi anapopigwa na wananchi, polisi hajui amkamate nani ikiwa mwizi huyo amekufa au amefariki.

Sasa kwa hili la makanisa ile ni kama riot imetokea, inaweza nkuwa vibaka,au hao uamsho ambao wamekanusha pia inawezekana ni vikosi kazi mbaya vya serikali ,ili kuwadhibiti watu flani kwa kuwasingizia, ila wazanzibari ni wamoja hivyo hilo limefeli, la ulimboka hatujui kinachoendelea kwani waliokuwa na dr katika hatua za mwanzo wapo, mawasiliano yapo, maana kama simu ya uli ilipotea data za simu yake zinakuwepo katika kampuni ya simu ,alimpigia nani alipigiwa na nani kwa wakati huo aliotoweka.

Huwezi kupata mazungumzo lakini wapi na wapi alipiga na kupokea simu utaweza kuzijua namba zilizohusika kama cdm wana mshiko ndani ya makampuni ya simu wanaweza kujua alizungumza na kupigiwa na namba ipi au zipi.

kwa technology ya sasa hata mazungumzo ya sauti yanapatikana, lakini sasa kama serikali imehusika nani anathubutu kutoa huo ukweli? Nchi ilishaoza hii. Hakuna system inayofanyakazi sawa sawa, tunaishi kwa rehemua za mwenyezi mungu tena kwakuwa watz ni waoga.
 
Ukidhani unaimani na jeshi la polisi basi ujue una matatizo makubwa tu! ndiyo maana Kova watu wana mwambia hatuna imani na wewe yeye ana lazimisha 'ohhh mimi lazima tu nita fanya uchunguzi" kama hatuna imani na wewe tutawezaje kuwa na imani na matokeo ya uchunguzi wako? Jshi la polisi lijiweke wazi kwamba wao wako kwa maslai ya serikali basi, unafifki hausaidii.
 
sio rahisi kuandika jambo zuri dhidi ya jeshi la polisi kama unalichukia, post imejaa kulichukua jeshi lote na kila afisa wa jeshi sio fear hata kidogo.

Ni juzi tu polisi walikuja kuniokoa mimi na familia yangu tulipovamiwa na majambazi wakafanikiwa kumuua mmoja na kukamata wawili.

unajua ng'ombe haoni umuhimu wa mkia wake mpaka akiukata nzi wakianza kumsumbua ndo ataukumbuka nina maana kwamba wapo wasiouona umuhimu wa jesh la polisi mpka matatizo yawakute ndo watawakumbuka na kujua umuhimu wake.
 
Unajua mwizi anapopigwa na wananchi, polisi hajui amkamate nani ikiwa mwizi huyo amekufa au amefariki.

Sasa kwa hili la makanisa ile ni kama riot imetokea, inaweza nkuwa vibaka,au hao uamsho ambao wamekanusha pia inawezekana ni vikosi kazi mbaya vya serikali ,ili kuwadhibiti watu flani kwa kuwasingizia, ila WaZanzibari ni wamoja hivyo hilo limefeli, la Ulimboka hatujui kinachoendelea kwani waliokuwa na Dr katika hatua za mwanzo wapo, mawasiliano yapo, maana kama simu ya Uli ilipotea data za simu yake zinakuwepo katika kampuni ya simu ,alimpigia nani alipigiwa na nani kwa wakati huo aliotoweka.

Huwezi kupata mazungumzo lakini wapi na wapi alipiga na kupokea simu utaweza kuzijua namba zilizohusika kama CDM wana mshiko ndani ya makampuni ya simu wanaweza kujua alizungumza na kupigiwa na namba ipi au zipi.

Bado taarifa za "KIINTELIGISIA HAZIJAWAFIKIA RASMI" zikisha wafikia watatoa tamko endelea kusubiri
 
Walioweka vinasa sauti chumbani kwa Dr Slaa pale dodoma ni miaka mi4 sasa hawajakamatwa, waliowajeruhi Hainess Kiwia na Machemli karibu mwaka unapita, achilia mbali matukio kibao ya wizi na ujambazi.

Jeshi la polisi la Tz ni kitengo cha propaganda cha chama cha Mapinduzi a.k.a mabwepande na chama kinawalipa kwa kuwaacha wapokee rushwa wapendavyo, wapeane ajira kindugu na kushirikiana na majambazi bila kuchukuliwa hatua yoyote. Wako active kuzuia maandamano wanayodhani yanatishia uhai wa CCM.
Utendaji kazi wa polisi wetu ni sawa na ahadi za Kikwete, vyote havitekelezeki.
 
unajua ng'ombe haoni umuhimu wa mkia wake mpaka akiukata nzi wakianza kumsumbua ndo ataukumbuka nina maana kwamba wapo wasiouona umuhimu wa jesh la polisi mpka matatizo yawakute ndo watawakumbuka na kujua umuhimu wake.
Ukipata matatizo halafu uwe hauna hela ya kuwahonga polisi utajuta kuzaliwa. Mimi nawachukia polisi na nikipata matatizo nitatoa hela kununua huduma kwa vile huduma pale haitolewi bure, kuingia ndio bure kutoka hadi utoe hela
 
iliwachukua miaka 10 majasusi wa CIA kumnasa na kumuua Osama Bin Laden.

Iliwachukua miezi kadhaa hadi tarehe 31 Mei 2012 kwa Jeshi la polisi kumkamata aliyemuua Mwenyekiti wa chadema Arumeru. Muuaji Alikuwa kakimbilia Singida.

Wahalifu wote wana mbinu zao hakuna muda maalum kwa chombo cha dola wa kumkamata mhalifu. Ni mapema sana kusema polisi wameshindwa kuwasaka na

kuwanasa.


Pole sana kwa mawazo mgando: kwa upande wa zanzibar, tafuta ripoti ya kanisa katoliki iliyotolewa na baraza la maaskofu katoliki tanzania. humu jamvini ipo, (makanisa 23 yameshachomwa tangu mwaka 2003) na hakuna aliyekamatwa wala kushtakiwa mpaka sasa. Ishu ya Ulimboka labda uwe kipofu na kiziwi kuweza kuelewa. Polisi imeoza nani asiyejua. kama hauamini endesha gari lako ovyo alafu wakukamate...uone walivyooza...
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom