Aibu JK azindua kidaraja Morogoro

Aibu JK azindua kidaraja Morogoro

tatizo ni kwamba tuanadharau na kulalamikia kila jambo litakalofanyika na CCM na serikali yake,lakini kama tungekuwa na watu waishio mazingira hayo kulikozinduliwa daraja,wao ndio wangetueleza umuhimu wa hilo daraja kwao,

lakini pia uwepo wa Mh Raisi labda ni ktk kuwaonyesha wanachi kuwa ile ahadi niliyoitoa sasa nimeitekeleza so kulikuwa na haja yeye mwenyewe mtoa ahadi kuwepo na mtambue kuwa kuna baadhi ya vijiji hawajahi waona maraisi wao tangu kitambo sana,sasa huu ulikuwa mda mwafaka kwa wapiga kura kumwona kiongozi wao

kwa upande wangu napongeza kwani nikikumbuka nyumbani pale KIHELEZO-KIDODI-LUHEMBE hata tukipewa daraja la mambao tu tutashukuru daima,kwani mpaka sasa ni miaka zidi ya 50 tunapita mto MSOWERO,MTO KIHELEZO na MTOLUHEMBE kwa kuogelea na mkumbuka mwenyekiti wangu TOBE MZIGO aliyekufa kwa kusombwa na maji ya MTOMSOWERO mungu amlaze mahali panapo stahili

so kiukweli kwa sisi tunaoishi vijijini tunatambua umuhimu wa hivyo vidaraja mnavyovidharau

HONGERA MH RAISI uje ha hapa Kihelezo hii mito mitatu inatusumbua sana,sisi hata mkiweka mimbao kwetu ni ukombozi wa khali ya juu
 
Mkuu hicho "kidaraja" kimekuwa msaada mkubwa sana huko, si umeona hata majina yenyewe ya vijiji vilivyounganishwa "nacho"?

Mkuu huko ndiko kwetu, ni kweli hilo daraja ni muhimu sana kwetu hasa wakati wa masika, huo Mto- Mbozi huwa unafurika sana na kuleta madhara makubwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na vifo. Kuhusu majina hayo usishangae, hayana ubaya wowote MTOMBOZI ni huo mto ambao daraja limejemgwa, unaitwa Mto wa Mbozi, kumbe imeunganishwa na kuwa MTOMBOZI, kuhusu MATOMBO, sawa ni jina linalotokana na jiwe moja hapo Matombo ambalo lina sura kama ya binadamu na alama mbili zinazofanana na chuchu(maziwa). Kwa lugha ya asili ya watu wa maeneo haya, chuchu (maziwa)ni MATOMBO. Kumbe majina haya mawili yanachota uasilia wa maeneo hayo: mto na hilo jiwe.
 
Hasara ya kuishi mjini.nenda uko kijijini kulikozinduliwa iko kidaraja alafu wambie haya uliyoandika kama watakuelewa.Mkuu adha walioipata mpaka wamejengewa iko unachokiita kidaraja wanamshukuru mwenyezi mungu.Nenda kwengine kaone
JAMANI TUSIPINGE KILA KITU

Tatizo sio kwenda kuzindua daraja, Tatizo ni gharama za kuzindua ni kubwa kuliko thamani ya kadaraja kenyewe. Hebu fikiri msafara wa rais kutoka Dar na posho za wafuasi wake zoote, halafu linganisha na thamani ya kadaraja kenyewe. Halafu utakuta huko mtombozi au matombo hakuna madawati mashuleni, zahanati hazina dawa, nyumba za walimu nk halafu unakwenda kuwauzia sura kwa gharama kubwa hivyo. Kwa nini asiende mkuu wa mkoa kuzindua, hizo fedha za misafara zikafanya kazi nyingine hapo hapo au hata kusaidia kadaraja ktk vijiji vingine?
 
tatizo ni kwamba tuanadharau na kulalamikia kila jambo litakalofanyika na CCM na serikali yake,lakini kama tungekuwa na watu waishio mazingira hayo kulikozinduliwa daraja,wao ndio wangetueleza umuhimu wa hilo daraja kwao,

lakini pia uwepo wa Mh Raisi labda ni ktk kuwaonyesha wanachi kuwa ile ahadi niliyoitoa sasa nimeitekeleza so kulikuwa na haja yeye mwenyewe mtoa ahadi kuwepo na mtambue kuwa kuna baadhi ya vijiji hawajahi waona maraisi wao tangu kitambo sana,sasa huu ulikuwa mda mwafaka kwa wapiga kura kumwona kiongozi wao

kwa upande wangu napongeza kwani nikikumbuka nyumbani pale KIHELEZO-KIDODI-LUHEMBE hata tukipewa daraja la mambao tu tutashukuru daima,kwani mpaka sasa ni miaka zidi ya 50 tunapita mto MSOWERO,MTO KIHELEZO na MTOLUHEMBE kwa kuogelea na mkumbuka mwenyekiti wangu TOBE MZIGO aliyekufa kwa kusombwa na maji ya MTOMSOWERO mungu amlaze mahali panapo stahili

so kiukweli kwa sisi tunaoishi vijijini tunatambua umuhimu wa hivyo vidaraja mnavyovidharau

HONGERA MH RAISI uje ha hapa Kihelezo hii mito mitatu inatusumbua sana,sisi hata mkiweka mimbao kwetu ni ukombozi wa khali ya juu

Kaka nasikitika kwa waliokufa kwa kusombwa na maji kwa kukosa daraja, Mungu awalaze pema peponi. Lakini pia vitu vingine na nyie muache uvivu na ufinyu wa fikra. daraja la mambao mpaka mletewe na serikali? Huo ni uvivu na ugonjwa mbaya sana, mnahitaji maombezi Mungu awanusuru na hilo tatizo. Kweli kuna madaraja makubwa ambayo yanahitaji nguvu ya serikali, lakini sio kila daraja mnakaa, mnakufa mkisubiri serikali ije kuwajengea daraja la mambao, huko kwenu hamna miti? hata diwani anaweza kuwakusanya wanakijiji wakafanya katika mtindo wa kujiletea maendeleo. Miaka 50 hamna hata daraja la mbao? na unathbutu kuja JF kujieleza. Aibu sana. Acheni Uvivu na Uzembe. JF is place of Great Thinkers na sio Wazembe na wavivu kiasi hiki.
 
Mkuu huko ndiko kwetu, ni kweli hilo daraja ni muhimu sana kwetu hasa wakati wa masika, huo Mto- Mbozi huwa unafurika sana na kuleta madhara makubwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na vifo. Kuhusu majina hayo usishangae, hayana ubaya wowote MTOMBOZI ni huo mto ambao daraja limejemgwa, unaitwa Mto wa Mbozi, kumbe imeunganishwa na kuwa MTOMBOZI, kuhusu MATOMBO, sawa ni jina linalotokana na jiwe moja hapo Matombo ambalo lina sura kama ya binadamu na alama mbili zinazofanana na chuchu(maziwa). Kwa lugha ya asili ya watu wa maeneo haya, chuchu (maziwa)ni MATOMBO. Kumbe majina haya mawili yanachota uasilia wa maeneo hayo: mto na hilo jiwe.

Nimekupata Mkuu, ufafanuzi mzuri huo.
 
Endeleeni kupiga mbizi huko kwingine. Na tukiwawekea daraja mtaweza kulipia kupita, mana siku izi nasikia salenda, kigamboni, madaraja yote hata kimara ubungo na kwingineko yatalipiwa, sorce', tetesi kigamboni.tanzania zaidi ya uijuavyo
 
Kaka nasikitika kwa waliokufa kwa kusombwa na maji kwa kukosa daraja, Mungu awalaze pema peponi. Lakini pia vitu vingine na nyie muache uvivu na ufinyu wa fikra. daraja la mambao mpaka mletewe na serikali? Huo ni uvivu na ugonjwa mbaya sana, mnahitaji maombezi Mungu awanusuru na hilo tatizo. Kweli kuna madaraja makubwa ambayo yanahitaji nguvu ya serikali, lakini sio kila daraja mnakaa, mnakufa mkisubiri serikali ije kuwajengea daraja la mambao, huko kwenu hamna miti? hata diwani anaweza kuwakusanya wanakijiji wakafanya katika mtindo wa kujiletea maendeleo. Miaka 50 hamna hata daraja la mbao? na unathbutu kuja JF kujieleza. Aibu sana. Acheni Uvivu na Uzembe. JF is place of Great Thinkers na sio Wazembe na wavivu kiasi hiki.

Nasikitika sana kwa sababu hufahamu mito yenyewe ilivyo,kama ungekuwa unaifahamu hiyo mito wala usingetutukana sisi wapogoro

kama huwa unakwenda kilombero kununua mchele ama unarafiki huwa anakwenda huko mwambie atembele kijiji cha KIGODOBASI ma KINEPA mweleze apige picha mito atakayokutana nayo na akuletee utashangaa

mito hiyo inaupana wa mita 50 na urefu kwenda chini ni zaidi ya mita 6,so pindi mito ijaaapo ndipo tabu inapoanzia,sisi kwa kuogelea sio kazi ni wazima sana,
tatizo ni pale unapokuwa na mgonjwa kwani tunategema hospitali ya kiwanda cha miwa K1 ma K2.na hata vituo vya polisi pia tunategemea huko,pindi kukiwa na shida ya mito kujaa ni tabu sana

kwa hiyo mkuu mpaka nimeamuwa kutaja maeneo hayo tambuwa kuwa hayo maeneo yanahitaji mkono wa serikali

kwa mfano MTO MSINDAZI kule mashambani tumeudhibiti kwa kuweka magogo mawili(tunamiti hapa ni mirufu sana) ndio tumetumia lakini kwa hiyo mito mitano hata hiyo miti haiwezi kufua dafu
 
Endeleeni kupiga mbizi huko kwingine. Na tukiwawekea daraja mtaweza kulipia kupita, mana siku izi nasikia salenda, kigamboni, madaraja yote hata kimara ubungo na kwingineko yatalipiwa, sorce', tetesi kigamboni.tanzania zaidi ya uijuavyo

tulisha zoea ni kitu cha kawaida kwetu kuogelea tena kwa stahili tofauti,hata wasipo tuwekea madaraja haina shida

mbona hata pale malinyi-ulanga kuna mto unaitwa MTOFURUA walimu tulikuwa n awaliobaki wanaendelea kupiga mbizi kufuata mahitaji muhimu,kwa hiyo haina shida kwetu kupiga mbizi tulisha zoea
 
FF, linalosemwa si umuhimu wa daraja! Ni thamani/hadhi ya daraja na cheo cha rais. Hapa ni vitu viwili tofauti. Vijijini hata lingekuwa la miti as long as linasaidia usafiri na kuvuka kwa watu ni kitu cha muhimu sana, ila mtu kama president wa nchi pengine wangemtafutia mradi mwingine mkubwa badala ya kadaraja kama anavvyosema mreta hoja.
Hilo tu ni jibu tosha kabisa.
 
Inaelekea hili daraja ni kiungo muhimu kweli kweli. Ila am happy now instead of boarding a flight to US, the whole convoy now goes to visit our villages and open the development programs we have set in those places.
 
Sasa wewe Yo Yo ulitaka JK afanye kazi gani????. hakuna cha kuzindua kikubwa inabadi ajichanganye kwenye hako hako.
 
Wewe acha kuwa na mawazo mgando, kilichofanyika sio hisani bali ni wajibu wa serikali kwa mujibu wa mkataba wetu kabla hatujawachaguwa. na ukumbuke huo sio msaada bali ni kodi zetu wenyewe.
Watu wenye mawazo kama yako ni mzigo kuwa nao kwa Dunia ya leo.

Mkuu hili ndio tatizo tulionalo watu wanashindwa kutofautisha wajibu na majukumu ya serekali wanaona kama favour hivi wakifanyiwa kitu.
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Watu hawabezi daraja,kinachoibua hoja hapa ni uzito wa mtu/msafara ulioenda kufungua na gharama za msafara huo! naunga mkono kwamba angefungua Nw,RC ama DC tu, gharama zikapungua na kuelekezwa pahala pengine
 
"mtombozi", "matombo".....majina yaliisha huko?

Haahaaa🙂 Hata mie majina hayo yamenifanya nisahau kuangalia hicho kiitwacho KIDARAJA!

Naona Walugulu wana utani na watumiaji kiswahili sote....Haya majina ukiwa na wakwe au watoto wako kuyataja yanafanya domo liwe zito kwa kiasi kikubwa!
 
Mkuu...sio kadaraja....huo ni mradi uligharimu mamilioni ya fedha za watanzania....mradi umekamilika mkuu wa nchi ameenda kuweka baraka ili kesho msiseme mradi ulikuwa na kasoro hata daraja halina kiwango. Raisi ameshaona ameridhika....
 
Back
Top Bottom