AI sio kitu kipya, tangu 2011 nilikuwa nina simu yangu samsung ilikuwa na features nyingi za AI, hata ile app ya Shazam ni AI, hata google chrome inatumia AI.
AI ni kitu general sana, inabidi kuichambua hiyo AI unayozungumzia ipo katika mfumo upi au kusaidia kazi ipi.
Kuna watu ni ngumu kuwafanya waelewe, ni bora kuwaacha tu.
AI ni mitambo kufanya kazi kama binadamu, kwa hiyo hakuna nchi duniani ambayo haitumii AI.
Simu ni AI, computer ni AI.
Ukienda kiwanda cha bia karibu kila inafanywa na AI.
Chupa inatembea kwny conveyor belt inapita kwny kitu kinaitwa EBI(Empty Bottle Inspection) inakaguliwa, inaenda kwenye mtambo unaitwa Filler, inajazwa liquid, inafunikwa kizibo na machine, inaenda kwenye Labler, inawekewa lable.
Inaenda kwny AI inaitwa FBI, yaani Full Bottle Inspection, inakaguliwa, kama haijajaa vizuri inawekwa pembeni.
Kiwanda kizima cha TBL wanaweza kuingia watu watano tu na production ikafanyika, kazi nyingi zinafanywa na mitambo yenye akili kama binadamu, lakini ni Akili bandia.
Ndio maana ya AI, Artificial Intelligence.
Kilichopo wanataka kuboresha zaidi, kazi nyingi zaidi zifanywe na mitambo.
Wabongo hatutaki, kwamba tutakosa kazi.