Ahukumiwa maisha jela baada ya kubaka

Superintendent kimura

JF-Expert Member
Feb 24, 2023
222
908
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa imemuhukumu kifungo cha maisha na fidia ya Tsh. milioni 5 Kijana mwenye umri wa miaka 19 Calvin Kahonga baada ya kumkuta na hatia ya kumbaka Mtoto mdogo mwenye umri wa miaka minne.

Siku ya tukio Calvin alikwenda nyumba anayoishi Mtoto huyo na kumbaka wakati Mama wa Mtoto alipokwenda kuchota maji na Calvin alipomaliza kufanya tukio hilo alikimbia, Mama wa Mtoto aliporejea aligundua Mtoto wake hayupo sawa ndipo akaenda kutoa taarifa katika ofisi ya Serikali ya Kijiji na taratibu za kumkamata Calvin zikafanyika.

Calvin alipopewa nafasi ya kujitetea Mahakamani hapo aliiomba Mahakama impunguzie adhabu kwasababu Mama yake mzazi ni Mlemavu wa mikono na anamtegemea kwa kila kitu lakini Wakili Baton Mayage akaomba Mahakama impe adhabu kali kwakuwa kosa hilo ni la pili na aliwahi kumlawiti Mtoto.

Calvin ambaye ni Mkazi wa Pawag, Isimani Mkoani humo amewahi kuhukumiwa kuchapwa viboko 12 akiwa na umri wa miaka 18 mwaka jana baada ya Mahakama ya Wilaya kumkuta na hatia ya kumlawiti Mtoto wa miaka mitatu.

Kesi hiyo imesimamiwa na Mawakili wa Serikali Ruben Lubango na Baton Mayage na ilikuwa na Mashahidi watatu ambao ni Mtoto, Mama na Daktari ambapo akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mkuu Said Ally Mkasiwa amesema Mtuhumiwa amekutwa na hatia kutokana ushahidi uliotolewa Mahakamani hapo hivyo anastahili adhabu hiyo.
#MillardAyoUPDATES
20231016_175816.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku ya tukio Calvin alikwenda nyumba anayoishi Mtoto huyo na kumbaka wakati Mama wa Mtoto alipokwenda kuchota maji na Calvin alipomaliza kufanya tukio hilo alikimbia, Mama wa Mtoto aliporejea aligundua Mtoto wake hayupo sawa ndipo akaenda kutoa taarifa katika ofisi ya Serikali ya Kijiji na taratibu za kumkamata Calvin zikafanyika.
Something is missing, nani alishuhudia akitenda kitendo au aliacha harufu njiani
 
Back
Top Bottom