AG Kumshtaki Tundu Antipas Lissu

ndugu yangu acha ushabiki kwa sababu aliyesema ni tundu lissu wa chadema, na ni vyema mkachanbua na kutathimini ipasavyo alichosema tundu lissu.kama mtu kasikiliza hotuba hiyo, ,hawezi kusema kwa kutamka kama ulivyosema wewe.Hoja aliyosema tundu lissu ina mantiki na wala wakuwadharau majaji, wewe unayesema hivyo ndo unawakumbatia udhaifu wao.majaji si miungu ni binadamu kama wengine.Mhimili huu una maadili yake na uteuzi wake una vigezo muhimu, lakini kwa sasa kumeibuka maswali kwenye uteuzi huo, na kuhoji kama kweli vigezo vilizingatiwa.Kigezo ni weledi, uzoefu, uadilifu na umri.Kuna baadhi ya majaji weledi wao kwenye hukumu zao umekuwa na mawaswali mengi.na kuhoji kama vigezo vilizingatiwa.Pia inatia shaka kama ni kwanni rais ateue jaji ambaye umri wake wa kustaafu umefika, hapa swali la umri linakuwa halikuzigatiwa.maswali yanakuwa kuwa," anapewa fadhila ya kupata marupurupu ya kustaafu bila kuwa na muda aliofanya kazi uanotosha ipasavyo.na je kwenye uteuzi huo hakukuwa na wanazuoni wakisheria wenye umri mzuri wakuteuliwa ili kupewa nyazifa hizo?Juzi kuna mdada alikuwa na fanya kazi kwenye law firm ya riz ameteuliwa kuwa jaji,watu wengi walikuwa na maswali mengi kuhusu hilo.Kwahiyo tundu lisu kama mbunge na pale kulikuwa mahala pa kupitisha bajeti hiyo ya utendaji huo, hakuwa na kosa kuhoji hayo.Sisi watanzania tunakosea sana kukaa kimya kutohoji masuala yanayokera wananchi kama hayo, na pia wanaofichua kero hizo husakamwa wasifanye kwa giriba na hila kama hizo.Hoja ni vyema muhimili wa mahakama uwe na uadilifu kama mihimili mingine.Na kero zilizopo kutozihoji kwa kuwa ni majaji watadharauliwa ni kuficha uozo ambao rais anaufanya na kwa mamlaka aliyopewa kusimamia.
Tuache ushabiki wa kivyama kwenye masilahi umma, mahakama ni muhimili muhimu sana.
Asante kwa hoja
Soma na hili kituko cha Werema;
Alipoulizwa kuhusu utekelezaji wa hatua hiyo jana, Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema alisema kuwa siyo lazima kwa Watanzania kufahamu hilo.
"Nilipozungumza jana (juzi) sikuzungumza na Watanzania bali nilizungumza na Bunge, hivyo siyo lazima Watanzania kufahamu jambo hilo na wala sioni sababu za kwa nini liandikwe magazetini,'' alisema Jaji Werema.


source Mwananchi .
Lissu sasa matatani ; Sunday, 15 July 2012 10:28 a friend

Alafu watu wengine wanaleta maoni ya kubwabwaja na kumuunga mkono mtu kama huyu na kumsifia eti msomi!
Kwa kauli kama hii anafaa kuwajibishwa maana anasahau kuwa aliyemteua ameajiriwa na watanzania na kwamba Mh.Lissu na Bunge ndiyo watanzania wenyewe wawapo Bungeni.Ila labda kauli na Mbiu ya kuwa Raisi ni Dhaifu ndiyo inayompa Jeuri.
 
ccm ni kama mfa maji,hawaishi kutapatapa.kifo lazima tu hata hata wakitumia hawa wanasheria uchwara kama werema.
 
Lissu ni mtaalam wa sheria za mazingira, na si mtaalam wa sheria za katiba, upo hapo ? kwa minajili hiyo basi utajua Lissu ni limbukeni wa sheria, na ni mpayukaji tu, kwa nyie mnaopenda hata mmeisha ingia upofu Kupenda balaa! jamaa hawataki hata ufafanuzi!

Yaani kupenda balaa! watu hataki hata ufafanuzi! Duh!
 
Ni kutokana na kauli yake ya dharau kwa majaji wa mahakama kuu na kuwataja kwa majina wahusika katika sakata la Ulimboka!


Atashtakiwa kwenye mahakama ipi?
Mbunge hawezi kushitakiwa kwa kauli anazosema akiwa Bungeni(immunity of the parliamentarians in the parliament).
Ref: Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 100.
 
Lissu nadhani wakati mwingine huwa narukwa kidogo na fahamu, kwani kwa kauli yake ya leo juu ya kuwadharau majaji ni wazi kabisa amepotoka, na hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kumtetea Lissu labda awe na moyo wa chuma


kwanui wao ni m,iungu
 
Cjapata kuona mwanasheria dhaifu kama werema, halafu ameanza kuwa mshabiki zaidi kuliko mtaalamu! Maneno ya Tundu ndo wanayosema watu wengi mtaani!
 
Hilo tu! Amshtaki kwa hela na gharama toka mfukoni mwake binafsi sio kwa kodi za wananchi wa Tz!
 
sidhani kama ni habari za ukweli, ni uzushi tu. Hotuba ya kambi ya upinzani ipo sawa tu. Halafu kumbuka mihimili hii huwa haingiliani
 
Lakini kuweza kujua kama mwanasheria fulani ni bora kuliko mwingine ni jambo gumu sana. Yawesekana ukamuona mtu mwenye kipaji cha kuongea sana mbele ya public kuwa bora kuliko mtu mwenye kipaji cha kuaandika sana na kufanya uchambuzi wa kimaandishi. Majaji wengine ukiwaleta Bungeni waanze kulumbana katika kuchangia hoja unaweza kuwaona hawajui. Lakini baadhi ya hao wenye vipaji sana vya kuongea ukija katika uwezo wa kuandika kwa utuliivu na kujenga hoja inaweza kuwa tofauti. Mnakosea sana kumhukumu mh. AG. kwamba ni kilaza kwa vipimo vyenu vya malumbano Bungeni.

Mimi kwa maoni yangu tungeepuka kujadili nani anajua kuliko nani na badala yake tukajadili uthabiti wa hoja. Tutakuwa hatuwatendei haki waheshimiwa AG na Tundu Lissu tukiwahukumu kama wanajua sana au hawajui sana
 
Lakini kuweza kujua
kama mwanasheria fulani ni bora kuliko mwingine ni jambo gumu sana.
Yawesekana ukamuona mtu mwenye kipaji cha kuongea sana mbele ya public
kuwa bora kuliko mtu mwenye kipaji cha kuaandika sana na kufanya
uchambuzi wa kimaandishi. Majaji wengine ukiwaleta Bungeni waanze
kulumbana katika kuchangia hoja unaweza kuwaona hawajui. Lakini baadhi
ya hao wenye vipaji sana vya kuongea ukija katika uwezo wa kuandika kwa
utuliivu na kujenga hoja inaweza kuwa tofauti. Mnakosea sana kumhukumu
mh. AG. kwamba ni kilaza kwa vipimo vyenu vya malumbano Bungeni.

Mimi kwa maoni yangu tungeepuka kujadili nani anajua kuliko nani na
badala yake tukajadili uthabiti wa hoja. Tutakuwa hatuwatendei haki
waheshimiwa AG na Tundu Lissu tukiwahukumu kama wanajua sana au hawajui
sana

tunawahukumu kwa kauli zao. hata hao majaji wasioweza kuzungumza bungeni hawakatazwi kuandaa na kupanga hoja zao vizuri kabla ya kuziongea bungeni!
 
ladda ww akili zako hazitoshi, kwa sababu unaongea usichokifahamu, nenda tazama hukumu kama utaona hukumu kama za akina justice lugakingira, justice mwalusanya mfalila au kurudisha kesi bungeni ndio unaona poa
 
Lakini kuweza kujua kama mwanasheria fulani ni bora kuliko mwingine ni jambo gumu sana. Yawesekana ukamuona mtu mwenye kipaji cha kuongea sana mbele ya public kuwa bora kuliko mtu mwenye kipaji cha kuaandika sana na kufanya uchambuzi wa kimaandishi. Majaji wengine ukiwaleta Bungeni waanze kulumbana katika kuchangia hoja unaweza kuwaona hawajui. Lakini baadhi ya hao wenye vipaji sana vya kuongea ukija katika uwezo wa kuandika kwa utuliivu na kujenga hoja inaweza kuwa tofauti. Mnakosea sana kumhukumu mh. AG. kwamba ni kilaza kwa vipimo vyenu vya malumbano Bungeni.

Mimi kwa maoni yangu tungeepuka kujadili nani anajua kuliko nani na badala yake tukajadili uthabiti wa hoja. Tutakuwa hatuwatendei haki waheshimiwa AG na Tundu Lissu tukiwahukumu kama wanajua sana au hawajui sana

Utakacho waza, ndicho utakacho andika,ulicho andika ndicho utakacho sema. Amini ndugu yangu, hapo AG hatuna. Ila sema yupo hapo kwa kulipana fadhila. Atahukumiwa kwa haki kulinga na matendo yake.
 
Nilidhani wabunge wana Parliamentary privilege. Hawawezi kushitakiwa kwa mambo wanayoongea ndani ya bunge, no?

Kwani mwasheria mkuu yupo pale kulinda na kufafanua sheria za nchi na katiba yake?yuko pale kulinda maslahi ya serikali na chama cha magamba.K.imsingu ni pofu wa kisheria , nachela kusema na shak na ujaji alioupata, na pia ujuzi wa taaluma yake.We ni mdau tu wa JF unafahamu hivyo je yeye kwa nini asifahamu hilo?kama atafungua kwa hisia za kisiasa , itakuwa kesi haina mashiko , sababu lisu alisema hivyo akiwa ndani ya bunge.Angeweza kushitakiwa kwenye kamati ya maadili na sheria ya nunge na si mahakama za kisheria.Hiyo ni katiba ya nchi ndo inayosema hivyo.Mjinga sana huyu bwana
 
Mimi nadhani changamoto yako ingeishia kusema kwamba hamna majaji wanaoweza kuandika hukumu kama judge Mwalusanya na Lukakingira ungeeleweka na hoja yako kupewa uzito. Lakini kuhoji kama akili zangu hazinitoshi kutokana na kutoa hoja tofauti na wewe naona ni kutumia kipaji chako kunidhalilisha kwa sababu unajua fika kwamba moderator, kama yupo, hajaweka mechanisms za kuwalinda wachaniaji dhaifu katika fani ya matusi kama mimi kudhalilishwa na wababe wa matusi.

Kuhusu hoja yake ya uwezo wa majaji wa sasa na wa zamani labda ungeniambia kwanza umeshasoma hukumu ngapi za majaji wa sasa na wa zamani zilizoripotiwa na zisizoripotiwa. Na je majaji wote wa zamani walikuwa na uwezo sawa na hao majaji uliowataja?

Siwezi hata siku moja kutia shaka juu ya umahiri mkubwa waliokuwanao majaji uliowataja enzi za ujaji wao katika kuchambua sheria na ushahidi na hatimaye kutoa maamuzi yaliyobebwa na hoja zinazoshawishi. Hoja yangu ni kwamba hata kwa majaji tulionao leo wapo majaji mabingwa wanaoweza kuandika hukumu nzuri sawa na pengine kuzidi za majaji uliowataja. Na zamani pia walikuwepo majaji waliokuwa wanaandika huku za kawaida tu labda tofauti ni idadi ambayo inaweza kuwa kubwa zaidi kwa sasa kuliko zamani. Moja ya sababu pia inaweza kuwa wingi wa majaji kwa sasa ukilinganisha na zamani na kuongezeka zaidi kwa watu wanaosoma fani ya sheria kiasi cha kuifanya fani hiyo sio rare profesional sana kama ilivyokuwa hapo zamani.

Bahati mbaya sijui mwenzangu (kama ni mwanasheria) ulisoma miaka gani? Miaka tuliosoma sisi, achilia mbali miaka waliosoma akina jaji Mwalusanya, kulikuwa na kitivo kimoja tu cha sheria nchi nzima ambacho kilikuwa kinachukua wanafunzi sio zaidi ya 50 kutoka Tanzania. Utakuta kwamba watu walikuwa wanashinda na points za division 1 na sio mtu kapata division gani.
 
GeniusBrain ni bure kabisa na ni kinyume cha Nickname yake. Ndio maana tunasema watu wapate basic education aweze kuchanganua mambo. Au keshaahidiwa pesa ya chakula leo kuja na mada zisizoikuwa na mashiko? Huku kwenye JF kuna watu wa ajabu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom