AG Kumshtaki Tundu Antipas Lissu

AG Kumshtaki Tundu Antipas Lissu

Lissu ni mtaalam wa sheria za mazingira, na si mtaalam wa sheria za katiba, upo hapo ? kwa minajili hiyo basi utajua Lissu ni limbukeni wa sheria, na ni mpayukaji tu, kwa nyie mnaopenda hata mmeisha ingia upofu


Kwenye taaluma ya sheria hakuna mtu ambaye ni mtaalam wa eneo moja tu. Kunaweza kuwepo mgawanyiko tu wa masuala ya kisheria ya kushughulikia. Sheria ya Katiba ni somo la wanasheria wote kama ilivyo kwa sheria ya jinai, sheria ya ushahidi, sheria ya utawala, sheria ya dhara (tort) na nyingine. Hakuna sheria ya mazingira kama somo bali ukishakuwa mwanesheria (shahada moja kwenda juu) unakuwa na tools of analysis, skills of statutory interpretation na jurisprudence ambavyo kwavyo unaweza kushughulika na sheria yoyote, ikiwemo hiyo ya mazingira, ya SUMATRA, ya Dawasco na yoyote ile very effectively na ndiyo maana hakuna wakili anayeshindwa kusimamia kesi inayohusu sheria yoyote ile.

Tunaweza kujadili mambo kwa ushabiki na kwa jazba lakini ni vizuri tuepuke kupotosha yale ambayo hatuyajui.
 
Lissu ni mtaalam wa sheria za mazingira, na si mtaalam wa sheria za katiba, upo hapo ? kwa minajili hiyo basi utajua Lissu ni limbukeni wa sheria, na ni mpayukaji tu, kwa nyie mnaopenda hata mmeisha ingia upofu


Kwenye taaluma ya sheria hakuna mtu ambaye ni mtaalam wa eneo moja tu. Kunaweza kuwepo mgawanyiko tu wa masuala ya kisheria ya kushughulikia. Sheria ya Katiba ni somo la wanasheria wote kama ilivyo kwa sheria ya jinai, sheria ya ushahidi, sheria ya utawala, sheria ya dhara (tort) na nyingine. Hakuna sheria ya mazingira kama somo bali ukishakuwa mwanesheria (shahada moja kwenda juu) unakuwa na tools of analysis, skills of statutory interpretation na jurisprudence ambavyo kwavyo unaweza kushughulika na sheria yoyote, ikiwemo hiyo ya mazingira, ya SUMATRA, ya Dawasco na yoyote ile very effectively na ndiyo maana hakuna wakili anayeshindwa kesi inayohusu sheria yoyote ile.

Tunaweza kujadili mambo kwa ushabiki na kwa jazba lakini ni vizuri tuepuke kupotosha yale ambayo hatuyajui.
 
lakini uteuzi wa wakuu wa wilaya, mikoa ambao pia ni wabunge inahitaji uwe umesoma constitutional law?
[/QUOTE]
Kwani kuna ubaya gani kwa wabunge kuwa DCs au RCs?
 
Ni kutokana na kauli yake ya dharau kwa majaji wa mahakama kuu na kuwataja kwa majina wahusika katika sakata la Ulimboka!

Kikatiba hawezi kufanya hivo maana wabunge wana kinga wawapo bungeni! hawawezi kushitakiwa kwa chochote wanachosema wakiwa bungeni! na hata hivo lisssu hawatuhumu hao watekaji kama yeye, alilitaja gazeti la mwanahalisi kama ndio chanzo cha habari hiyo! hivo kama ni kushitaki serikali ianze kulishitaki gazeti la mwanahalisi kwanza!
 
Kwani kuna ubaya gani kwa wabunge kuwa DCs au RCs?[/QUOTE]
hii ni kinyume na katiba kwa kuwa mkuu wa mkoa na wilaya ni watumishi wa umma! sasa watumishi wa umma hawaruhusiwa kushiriki siasa hasa kuchaguliwa kwenye post za kisiasa kama ubunge ndio maana hata kama wewe umeajiriwa serikalini ukitaka kugombea ubunge ubunge sharti ujiuzulu kama alivofanfa aliekuwa mkuu wa mkoa wa kilimanjaro monica mbega alipoenda kugombea ubunge Iringa
 
Lissu nadhani wakati mwingine huwa narukwa kidogo na fahamu, kwani kwa kauli yake ya leo juu ya kuwadharau majaji ni wazi kabisa amepotoka, na hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kumtetea Lissu labda awe na moyo wa chuma

[/
I know a judge with low integrity and questionable moral value. Any one should ask how that judge got the appointment. The other is the current AG. What he shows explicitly is Kurya's arrogance and no professionalism.
 
Tatizo bungeni watu wengi upande wa serikali ni wanafiki toka Ag ni mpuuzi mtupu hamna kitu!
 
Tundu Lisu ni Jembe na hakika kawasemea watumishi wazuri wenye sifa na waliobobea wa idara za mahakama wanaoshindwa kuteuliwa kuwa majaji kwa sababu ya uswahiba wa JK na watu wachache wasio na sifa za kuwa majaji.Pia AG na mawaziri wameshindwa kujibu hoja za Lisu ipasavyo kwa mfano katika uteuzi wa majaji wa hivi karibuni AG na Waziri walishindwa nini kutaja kikao cha Tume ya Mahakama kilikaa lini na kupendekeza majina ya wataoteuliwa kuwa majaji.? Ni ukweli kuwa JK anatembea na majina ya wateule wake kwenye briefcase ili kwamba nafasi inapotokea iwe jeshini anaotayari kwenye briefcace anajaza, iwe DC,RC anamajina tayari kutoka kwake, RIZ na SALAMA. Kwa ujumla ni upuuzi mtupu.
 
Lissu nadhani wakati mwingine huwa narukwa kidogo na fahamu, kwani kwa kauli yake ya leo juu ya kuwadharau majaji ni wazi kabisa amepotoka, na hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kumtetea Lissu labda awe na moyo wa chuma


Tatizo la Lissu huwa anasema moja kwa moja kuwa "mfalme yuko uchi" badala ya utamadumi wetu mzuri ambapo angejidai kusema "mfalme amevaa suti imembana vizuri kweli"
 
Lissu nadhani wakati mwingine huwa narukwa kidogo na fahamu, kwani kwa kauli yake ya leo juu ya kuwadharau majaji ni wazi kabisa amepotoka, na hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kumtetea Lissu labda awe na moyo wa chuma

Ebu jichunguze wewe kama una akili timamu maana kila unalijitahidi kuweka kwenye hii forum ni tofauti na wengine.
 
Kwani kuna ubaya gani kwa wabunge kuwa DCs au RCs?[/QUOTE]
Duh! Huyu nae ni Senior Expert Member wa JF!
 
Lissu asiposema ukweli kwani nani atasema ukweli? ata Sam Abacha alinyongwa kwa kusema ukweli na baadae ukweli ulkuja kudhihirika zaidi,mh Lissu endelea tu ccm wanaitaji nyundo imara kama ya kwako iyo.Rejea kauli ya Nchemba "wamejazana bungeni hapa kama wanavyokaa sebuleni wakiwa nyumbani",Mwagama (m/kiti) akacheka haaaaaaah,sasa kati ya cdm na ccm nani kaleta undugu bungeni?
 
Huyu Tundu Lissu is a very pathetic mwanasheria anawaaibisha sana wenzake. Yeye mwanasheria lakini hata kanuni za bunge lake hazijui vizuri. Nadhani anatakiwa kwanza ajipange kwa kupitia kanuni za bunge kwakuwa mara nyingi anachemka chemka kwa kupenda kutokea kwenye front page za magazeti.
 
Kwani kuna ubaya gani kwa wabunge kuwa DCs au RCs?[/QUOTE]

DCs & RCs ni sehemu ya serikali, ndio wawakilishi wa rais kwenye sehemu walizo. Wabunge ni wawakilishi wa wananchi katika kutunga sheria na kuisamamia/kuishauri serikali. Ndio maana mawaziri/naibu waziri pamoja na kwamba ni wabunge, hawaulizi maswali bungeni ila wanajibu from the executive branch. Sasa DCs na RCs wanakuwa wapi? executive, au wabunge wa kawaida? Haya ni masalia ya mfumo wa chama kimoja.
 
lissu ni mtaalam wa sheria za mazingira, na si mtaalam wa sheria za katiba, upo hapo ? Kwa minajili hiyo basi utajua lissu ni limbukeni wa sheria, na ni mpayukaji tu, kwa nyie mnaopenda hata mmeisha ingia upofu


we gamba nini? Vitisho vya kitoto hivyo!
 
Lissu nadhani wakati mwingine huwa narukwa kidogo na fahamu, kwani kwa kauli yake ya leo juu ya kuwadharau majaji ni wazi kabisa amepotoka, na hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kumtetea Lissu labda awe na moyo wa chuma


ndugu yangu acha ushabiki kwa sababu aliyesema ni tundu lissu wa chadema, na ni vyema mkachanbua na kutathimini ipasavyo alichosema tundu lissu.kama mtu kasikiliza hotuba hiyo, ,hawezi kusema kwa kutamka kama ulivyosema wewe.Hoja aliyosema tundu lissu ina mantiki na wala wakuwadharau majaji, wewe unayesema hivyo ndo unawakumbatia udhaifu wao.majaji si miungu ni binadamu kama wengine.Mhimili huu una maadili yake na uteuzi wake una vigezo muhimu, lakini kwa sasa kumeibuka maswali kwenye uteuzi huo, na kuhoji kama kweli vigezo vilizingatiwa.Kigezo ni weledi, uzoefu, uadilifu na umri.Kuna baadhi ya majaji weledi wao kwenye hukumu zao umekuwa na mawaswali mengi.na kuhoji kama vigezo vilizingatiwa.Pia inatia shaka kama ni kwanni rais ateue jaji ambaye umri wake wa kustaafu umefika, hapa swali la umri linakuwa halikuzigatiwa.maswali yanakuwa kuwa," anapewa fadhila ya kupata marupurupu ya kustaafu bila kuwa na muda aliofanya kazi uanotosha ipasavyo.na je kwenye uteuzi huo hakukuwa na wanazuoni wakisheria wenye umri mzuri wakuteuliwa ili kupewa nyazifa hizo?Juzi kuna mdada alikuwa na fanya kazi kwenye law firm ya riz ameteuliwa kuwa jaji,watu wengi walikuwa na maswali mengi kuhusu hilo.Kwahiyo tundu lisu kama mbunge na pale kulikuwa mahala pa kupitisha bajeti hiyo ya utendaji huo, hakuwa na kosa kuhoji hayo.Sisi watanzania tunakosea sana kukaa kimya kutohoji masuala yanayokera wananchi kama hayo, na pia wanaofichua kero hizo husakamwa wasifanye kwa giriba na hila kama hizo.Hoja ni vyema muhimili wa mahakama uwe na uadilifu kama mihimili mingine.Na kero zilizopo kutozihoji kwa kuwa ni majaji watadharauliwa ni kuficha uozo ambao rais anaufanya na kwa mamlaka aliyopewa kusimamia.Tuache ushabiki wa kivyama kwenye masilahi umma, mahakama ni muhimili muhimu sana.
 
Kwani kuna ubaya gani kwa wabunge kuwa DCs au RCs?[/QUOTE]

Tatizo la upofu wa kutopenda kujisomea, au kujieleimisha.Sheria ya vyama vingi nakataza mfanyakazi wa serikali kuwa mwanasiasa.Kuwa rc au dc kwa mujibu wa katiba ya ccm ni mjumbe wa vikao vyote vya chama.Sherai ya vyama vingi inakataza na kutamka wazi kuwa ni marufuku mfanyakazi wa serikali kuwa mwanasiasa, na kama akitaka kufanya hivyo aache kazi ya serikali akafanye kazi ya chama.Rcs na dcs ni wafanyakazi wa serikali hivyo ni kinyume cha sheria .
 
Hoja ya Mh. Lissu ni kwamba Raisi kateuwa baadhi ya majaji ambao hawakupendekezwa na Tume ya Ajira ya Mahakama. Waziri wa Sheria ansema yeye ni mmoja kati ya wajumbe wa Tume hiyo na kwamba ana uhakika kwamba hamna hata jaji mmoja aliyeteuliwa nje ya mapendekezo ya Tume. Mh Lissu hakutoa ushahidi wowote wa kuthibitisha tuhuma hiyo. Sasa hili linahitaji ujuzi gani kubainisha kwamba Mh. Lissu aliteleza.

Kwamba baadhi ya majaji walioteuliwa hivi karibuni hawana uwezo wa kuchambua ushahidi na kutoa uamuzi wenye mashiko ni hoja ambayo imetolewa kabla ya wakati wake. Nasema hivyo kwa sababu ni muda mfupi sana toka uteuzi huo ufanyike na kwa kumbukumbu zangu hamna hata mmoja kati yao aliekwisha toa hukumu.

Kama ni suala la kuchelewa kutoa maamuzi hilo sio lazima litokane na ujuzi bali inawezekana liikawa linatokana na uvivu. MH Lussu kama mtunga sheria angeshauriana na wenzake juu ya umhimu wa kirekebisha sheria ili kuwabana majaji watoe hukumu kwa wakati. Najua kwa mujibu wa sheria ya sasa wanalazimika kuandika hukumu ndani ya siku 90 toka wamalize kusikiliza shauri. Sheria hata hivyo iko kimya kama ni nini kitatokea kama hukumu isiposemwa ndani ya mda huo. Je hakimu atapoteza mamlaka ya kuandika hukumu na kutakiwa afanye taratibu za kuongeza muda wa kuandika hukumu kama kuna sababu ya msingi sheria iko kimya. Na hili limekuwa tatizo la miaka mingi toka enzi za Ema na Lay.
 
Back
Top Bottom