Verified
Senior Member
- Apr 11, 2013
- 117
- 380
Ni jambo la aibu kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali kutumia muda wa takriban dakika tatu kuelezea tofauti kati ya woman, Lady na Gentleman na kusema kwamba anashindwa kujua kama Halima Mdee ni Lady au Gentleman.
Kwa kweli kuangalia Bunge ni kichefuchefu tupu na hizi Ndioooooooooooo zao!!
Kwa kweli kuangalia Bunge ni kichefuchefu tupu na hizi Ndioooooooooooo zao!!
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, ameshindwa kutambua jinsia ya Mbunge wa Kawe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Halima Mdee, kutokana na kuingilia mazungumzo yake.
Sintofahamu hiyo iliibuka juzi jioni, bungeni Dodoma, wakati wa kikao cha mjadala wa bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria, ambapo Mdee alichangia kwamba Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), isipobadilisha mfumo uliowezesha kupatikana mabaraza ya Katiba watakwenda kuwashitaki kwa wananchi.
"Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo msiliweke kichama, hebu tuangalia maslahi ya taifa, kama ninyi hamtaki kubadilisha huu mfumo tukigawana hapa sisi tutoke twende kwa wananchi na kuwaeleza hoja hii hapatatosha," alisema Mdee.
Akifafanua hoja hiyo ambayo iliibuliwa pia na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, ilimfanya AG kutoa ufafanuzi ambapo wakati anaendelea kuzungumza sauti ya Mdee ilisikika.
Kitendo cha Mdee kuzungumza wakati AG akiendelea kutolea ufafanuzi hoja ya mabaraza ya katiba, kilimfanya ahoji jinsia ya Mbunge huyo, kutokana na baadhi ya makabila mengi nchini wanawake huheshimu pale mwanaume anapoongea.
"Unajua kule kwetu mwanaume akisimama na kuzungumza wanaume wanasikiliza, kinamama au wasichana wanafunga midomo..lakini sasa mimi ninapozungumza ndugu yangu Mdee unafunua mdomo sijui nikuweke kwenye kundi gani la ‘Lady au Gentlemen," alisema AG Werema.
Kauli hiyo iliibua vicheko miongoni mwa wabunge, huku Mdee mwenyewe akiangua kicheko sambamba na kuzunguka kwenye kiti alichokikalia.