BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,119
Mahakama ya Mkoa wa Vuga, leo tarehe 31/10/2023 imemhukumu mshtakiwa MOH'D ALI HASSAN (35) Mkazi wa Jumbi Uwandani Unguja kutumikia kifungo cha miaka 30 Chuo cha Mafunzo (jela) kwa kosa la Kuingilia kinyume na maumbile.
Awali mshtakiwa huyo alimuingilia kinyume na maumbile mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 06 jambo ambalo ni kosa, kinyume na kifungu cha sheria 133 (a) cha sheria ya adhabu namba 6/2018 Sheria ya Zanzibar.
Akisoma maelezo ya hukumu hiyo, Hakimu wa mahakama hiyo Mhe. TAKI ABDALLAH amesema Mahakama imejiridhisha na ushahidi uliotolewa mbele ya mahakama ambao haukuwa na chembe ya shaka ambapo umemtia hatiani mtuhumiwa kwa makosa hayo.
Jumla ya mashahidi watano (05) walitoa ushahidi mahakamani hapo.
Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakamani tarehe 21/08/2023 ambapo ilipewa kesi namba 127/2023.
Awali mshtakiwa huyo alimuingilia kinyume na maumbile mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 06 jambo ambalo ni kosa, kinyume na kifungu cha sheria 133 (a) cha sheria ya adhabu namba 6/2018 Sheria ya Zanzibar.
Akisoma maelezo ya hukumu hiyo, Hakimu wa mahakama hiyo Mhe. TAKI ABDALLAH amesema Mahakama imejiridhisha na ushahidi uliotolewa mbele ya mahakama ambao haukuwa na chembe ya shaka ambapo umemtia hatiani mtuhumiwa kwa makosa hayo.
Jumla ya mashahidi watano (05) walitoa ushahidi mahakamani hapo.
Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakamani tarehe 21/08/2023 ambapo ilipewa kesi namba 127/2023.