Afukuzwa kazi kwa kunuka mdomo

Afukuzwa kazi kwa kunuka mdomo

K 4 LIFE

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2015
Posts
2,567
Reaction score
419
Kuna jamaa moja amepoteza kazi yake baada ya kunuka mdomo kwa muda mrefu, alikua hana utaratibu wa kupiga mswaki.
 
Sawa tu afukuzwe harufu mbaya ya mdomo inakera wafanyakazi wenzake na wateja.
 
Harufu mbaya ya mdomo noma sana,huwa nashindwa kuelewa ni mtu anakuwa hajielewi au?
Hata kama ni ugonjwa kwanini asihangaikie tiba?
Mimi kama mtu ananuka mdomo nampotezea mazima,siwezi kujikosesha amani.

Umenichekesha sana nifah hilo neno mazima umenikumbusha mbali sana.
 
Last edited by a moderator:
Watu wengi wanajua kunuka mdomo ni kwa sababu ya kutokupiga mswaki. Inaweza ikawa kweli lakini sio kwa wote. Kuna watu wanapiga mswaki hata kila baada ya masaa lakini bado tu. Watu kama hao unakuta zile tonsils zinamifuko mikubwa ambayo inahifadhi chakula na mwisho wake ni harufu mbaya mdomoni. Wengi huondolewa tonsils kwa hiyo issue na anapona kabisa. Kikubwa jamaa aende kwa daktari wa ENT. Ear, nose and throat apate msaada
 
Na-comment kiuchokozi tu: Pengine mdomo wake unanuka kutokana na matusi anayomwaga hadharani tena basi bila aibu.
 
Mh!hii hatari nahisi namimi ajira yangu iko mashakani maana na mimi nanuka domo hatari sometimes natumia domo langu kufukuza mbu nyumbani kwangu! na nimeshafanya tiba nyingi tu naambiwa sijui gesi tumboni,vidonda vya tumbo etc na kuhusu mswaki mbona niko vyema meno yanaakisi tabasamu la mwana mfalme lakini harufu bhana!
saidieni tafadhali kabla huu ugonjwa wa kufukuza wanuka mdomo haujasambaa!
 
Mbona hilo ni tatizo dogo tu ? Kama kuna mwingine mwenye tatizo hilo Awe anakata kipande cha Tango anaweka mdomoni wakati wa kulala kinakaa hadi asubuhi baada ya siku 7 tatizo litaisha na ajitahidi kila akipiga mswaki asugue ulimi
 
Mbona hilo ni tatizo dogo tu ? Kama kuna mwingine mwenye tatizo hilo Awe anakata kipande cha Tango anaweka mdomoni wakati wa kulala kinakaa hadi asubuhi baada ya siku 7 tatizo litaisha na ajitahidi kila akipiga mswaki asugue ulimi
Domo kunuka tupo hapa haya hilo tango nini sayansi yake? (japo naona kuna hatari ya choking hapo)
 
Pia atumie kuchemsha karafuu yale maji anasukutua kila mara. Inasaidia na pia dawa za meno hutumia karafuu pia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom