Afrika inapaswa kuombwa msamaha na kulipwa fidia kwa madhara ya ukoloni

souljah meditater

JF-Expert Member
Oct 15, 2012
2,146
2,098
slave-ship-diagram.jpg

Ikumbukwe kwamba waafrika wengi walichukuliwa kinguvu na kimabavu kwenda nchi za ulaya na uarabuni kwa lengo la kutumikishwa kufanya kazi ili kuongeza uzalishaji wa mataifa hayo husika.

Tambua THEY DID NOT TAKE SLAVES but they took Doctors, architects, enterprenuers, astronomers, fathers, mothers, daughters, sons, brothers, sisters and e.t.c AND MADE THEM SLAVES.

Kipindi hicho madini na vito ndio ulikuwa utajiri wa dunia hivyo walifika Afrika na kuchukua mali zetu pamoja na ndugu ambao walikuwa chanzo kikubwa cha maendeleo yao.

Inasikitisha kuona waafrika wengi wanaumizwa na utumwa wa waisraeli uliofanyika misri miaka mingi iliyopita na kusahau utumwa wa mababu na bibi zetu ambao madhara yake yanatuumiza mpaka sasa.

Kiukweli hatuhitaji kuomba misaada nchi za ulaya ila tunatakiwa kudai haki yetu ya kulipwa fidia kwa matokeo ya biashara ya utumwa waliotufanyia waafrika.
 
Sema inatakiwa tuwashukuru kwa kututawala na kutuelimisha na ikibidi waje kututawala tena maana hawa watawala wa kiafrika ndiyo more worse
Mkwepa kodi unatamani kuja kutawaliwa tena ukiamini afrika hakukuwa na elimu unawashukuru wakoloni kwa kutuelimisha, tambua hata utawala unaoendelea sasa afrika ni mfumo wa matokeo ya utawala wa kikoloni i.e. afrika kulikuwa kuna utawala wetu tofauti na huu uliorithishwa
 
Mkwepa kodi unatamani kuja kutawaliwa tena ukiamini afrika hakukuwa na elimu unawashukuru wakoloni kwa kutuelimisha, tambua hata utawala unaoendelea sasa afrika ni mfumo wa matokeo ya utawala wa kikoloni i.e. afrika kulikuwa kuna utawala wetu tofauti na huu uliorithishwa
Natamani sana mkuu kutawaliwa na mkoloni mzungu kuliko mkoloni mweusi
 
View attachment 352916


Kiukweli hatuhitaji kuomba misaada nchi za ulaya ila tunatakiwa kudai haki yetu ya kulipwa fidia kwa matokeo ya biashara ya utumwa waliotufanyia waafrika.


Na hii ndiyo ilifaa kuwa madai sahihi!
La kwanza kuombwa radhi kwa madhila na pili kupitia UN nchi za Afrika kwa Ummoja wao walifaa wafungue madai haya!

Nadhani siyo wazo baya Tanzania kupitia EAC wakaanzisha mchakato huu kwa kuwaomba wanachama wa jumuia hii kuwa kitu kimmoja na kuiweka kwenye Protocol ya Jumuia kuwa Nchi zote zilizotawala Jumuia kuomba radhi kimaandishi na public na kuanzisha mchakato wa Fidia!
 
Na hii ndiyo ilifaa kuwa madai sahihi!
La kwanza kuombwa radhi kwa madhila na pili kupitia UN nchi za Afrika kwa Ummoja wao walifaa wafungue madai haya!

Nadhani siyo wazo baya Tanzania kupitia EAC wakaanzisha mchakato huu kwa kuwaomba wanachama wa jumuia hii kuwa kitu kimmoja na kuiweka kwenye Protocol ya Jumuia kuwa Nchi zote zilizotawala Jumuia kuomba radhi kimaandishi na public na kuanzisha mchakato wa Fidia!
Sure man ikiwa yaliyowakuta Hiroshima na Nagasaki imeonekana wana haki ya kulipwa iweje letu waafrika libaki historia isiyo na fidia? Nafikiri misimamo hii ingeweza kusimamiwa na Mugabe na hayati Gaddafi wengine wengi bado vibaraka wanagwaya
 
Bora Trump aingie madarakani maana kasema waafrika tunahitaji kutawaliwa 100 yrs. Yaani marais wetu wanaziibia serikali zao na kupeleka hela ulaya. Viva Magufuli
 
Bora Trump aingie madarakani maana kasema waafrika tunahitaji kutawaliwa 100 yrs. Yaani marais wetu wanaziibia serikali zao na kupeleka hela ulaya. Viva Magufuli
Trump ni mlopokaji na sera zake zimejaa fitina na ubaguzi.. yap ka viva magu tambua inawezekana waafrika kujiongoza bila kuziibia serikali zao
 
Waafrika hawana ubavu wa kudai fidia wala nini kwa wakoloni kwasababu ukoloni mamboleo unaendelea
 
Waafrika hawana ubavu wa kudai fidia wala nini kwa wakoloni kwasababu ukoloni mamboleo unaendelea
Yah kwa sababu ya utumwa wa kifikra suala la ukoloni limechukuliwa poa hivyo wengi hawajali wala kuwaza nini kilitokea historia inafundishwa kama hadithi za kusadikika ndo maana mpaka sasa ukoloni mamboleo unaendelea ila tunaona ndo maisha ya usasa na hakuna anayejali
 
Ngoja Donald Trump anakuja tutarudi kama zamani jeuri na ubabe vyote vitaisha kwa Hawa viongozi Wa Africa.
 
Hao wenzetu walio chukuliwa huko mabara ya ulaya na arabuni wana shukuru mara elfu kulikoni sisi tulio jitawala
 
Hao wenzetu walio chukuliwa huko mabara ya ulaya na arabuni wana shukuru mara elfu kulikoni sisi tulio jitawala
Sisi bado hatujajitawala ndo maana utumwa na ukoloni bado unaendelea afrika hao waliochukuliwa utumwani walitamani sana kurudi ukitaka kujua hili fuatilia movement za kina marcus mosiah garvey na wanaharakati wengine wa blackstar ship
 
Back
Top Bottom