Mkuu,
Wewe, Tindo na yule mwenye avatar ya yule msichana wa Pakistani nyote mna mawazo mazuri sana na nnawapenda kwa kuwa na mawazo ya kuchagiza.
Mnachokosea niu namna ya kuyawasilisha mawazo yenu na sijawahi kuona mnatoa matusi wala lugha ya kashfa.
Si ninyi ambao mnafanya hivyo bali wenzenu wenye mawazo kama yenu.
Ondoeni "contents" zenye kuchochea, kukashifu, kutukana, kutisha na kukejeli serikali iliyopo madarakani.
Kwa mfano umeweka kichwa cha mada yako kikielezea viongozi wa Afrika ambao hawakudumu madarakani na ukasema " Will Magufuli take a course?
Unamaanisha kwamba je Raisi Magufuli nae atafuata mkondo?
Sasa kwa tafsiri ya hicho kichwa cha habari na yaliyomo humo ni mapinduzi, kuondolewa kwa nguvu viongozi na hata kuuawa kwa mmoja wa viongozi hao.
Na unamwambia raisi Magufuli kwamba na yeye atafuata mkondo, wamtisha raisi wako? waitishia mamlaka? je watishia taasisi ya uraisi?
Hivyo ndivyo baadhi ya wageni na wanachama wengine watakuwa wanaweza.
Usidhani ni sisi tu wanachama wa JF twasoma hapa wapo watu wengi wa rika tofauti, kazi tofauti na malengo tofauti.
Tumia njia sahihi ya kuwasilisha maoni yako bila kumkwaza mtu, kumuudhi na hata kufanya akuchukie, hatua ambazo zitajenga uadui uso lazima.
Otherwise, I like you guys and your way of thinking!