African 'one term' presidents: Will Magufuli take a course?

African 'one term' presidents: Will Magufuli take a course?

Chadema walishinda lakini CCM waliiba kura
Potea pote. Sasa hawataiba tena? Hii excuse ya kuiba kura hata kama ina ukweli lakini imepitwa na wakati. Kama wanajua wataiba kura halafu wanaridia kufanya yale yale basi hawana maana.
 
Ulitegemea Kinana na Makamba sr watajwe kumhujumu rais na CCM?
Ushabiki au chuki kwa awamu ya sasa kusikufanye usione uhasilia wa siasa! Wewe ulitegea Dr Slaa atoke Chadema na aungane na Magufuli? Ulitegemea Lowassa atoke CCM na apokelewe Chadema kwa mbwembwe zote wakati walikuwa wanasema ni fisadi mkubwa? Wanasiasa hubadilika wanapoona maslahi yao yanatishiwa!
 
Huu ni mjadala mzuri tu wala haunà tatiźo. Binafsi nimekuwa na mawazo hayo hayo ya one term president. Sababu kubwa ni kwambà hakujiandaa na hata baada ya kushawishika kujitosa hakutarajia kushindà. Kwa sababu hizi ametumia nguvu nyingi sana kuongoza hali ambayo imemsababishia maadui wengi wa kisiasa nje na ndani ya chama chake. Mbali na kuchoka pia sidhani karma ccm asilia iko comfortable na style yake ya Uongozi. Dalili ni ukimya wa wazee wengi.
 
Ushabiki au chuki kwa awamu ya sasa kusikufanye usione uhasilia wa siasa! Wewe ulitegea Dr Slaa atoke Chadema na aungane na Magufuli? Ulitegemea Lowassa atoke CCM na apokelewe Chadema kwa mbwembwe zote wakati walikuwa wanasema ni fisadi mkubwa? Wanasiasa hubadilika wanapoona maslahi yao yanatishiwa!
Kumbe inawezekana kuwa na one term president?
 
FAO LA KUJITOA

Hao wanyonge wanaotetewa ni akina nani?

Au Lazima nchi iwe na wanyonge milele ili wasaka tonge wapate umaarufu

Mara huku DEGE eco village kigamboni, mara kule majengo hayana wapangaji?

ili mradi tu wametafuna pesa za wanyonge...Kwel laana hii itawapata kuanzia watoto mpaka wajukuu, wallahi
 
Nikweli lakini imekuwa too much to the extent sasa....
Ikisoma bandiko hilo limejaa hadithi za mapinduzi mapinduzi na kutokamilisha mihula ya uongozi.

Hadithi kama hizi zinapandikiza threats na upumbavu, why now?

KWENYE BIBILIA WAMEANDIKA ATAKAE VUMILIA HADI MWISHO NDIO ATAKAE OKOKA lakini hapa tunaona kuna mipumbavu ambayo ilizoea kuiba imeshindwa kuvumilia kusubiri matunda, maziwa na asali yameanza kuleta choko choko.


Kwa mjibu wa katiba ibara ya 15, 17, na 18 unaruhusiwa kutoa maoni lakini kwa namna gani basi, kwa namna ambayo haivunji utu wa mwingine wala kumdharisha na kukashifu.

Na ukumbuke unavyo mkashifu raisi unakuwa umemkashifu kiongozi wa taasisi ya urais jopo lake halitakubali kuendelea kukashifiwa kwa namna yoyote ile na wao watajibu kwa njia yeyote ile kutetea taasisi yao.
Mbona unaongea kitoto sana, eti "Watajibu kwa njia yoyote ile".. What a Lunacy.

Ujinga ujinga kama huu ndio umemfanya huyo Mohammed Morsi awe jela hadi leo akisubiri Kitanzi. Duniani hakuna bingwa.
 
Mkuu wewe endeleza UPUMBAVU wako huu na hii ni wiki ya pili mfululizo.Kitakachokukuta sijui Kama utakuwa na muda wa kurudi kutueleza, Kama upo JF kitambo yupo wapi jamaa alikuwa anaishi ughaibuni anaitwa TL MARANDU?, yupo wapi BAK?,yupo wapi MOKHILI FUMULAUHI?, wapo wengi tu waliojiona wanaweza kuongea pumba zozote sababu wapo Jamii forums Kila kitu kina mipaka yake, ukae ukijua hizi chokochoko wewe pamoja na waliokutuma(wanaokulipa hazitakuacha salama.

God forbid! Ninaamini kwa dhati kabisa unayedhani unamtetea hakubaliani hata kidogo na mtazamo wako wa kutisha raia wemà. Binafsi sijaona chokochoko yoyote hapo tofauti na maonì binafsi. Nadhani kauli kama hizi ķamwe haziujengi utawala huu. Badala yake zinaufanya kuonekana tofauti kabisa na nyingine zote zilizotangulia; tofauti kabisa na utamaduni wa kisiasa wa nchi hii.
 
Potea pote. Sasa hawataiba tena? Hii excuse ya kuiba kura hata kama ina ukweli lakini imepitwa na wakati. Kama wanajua wataiba kura halafu wanaridia kufanya yale yale basi hawana maana.

Hakuna kilichopitwa na wakati, CHADEMA itaendelea kushinda uchaguzi hata kama haitandangazwa mshindi. Watu wa nje pia wanaona upuuzi unaofanywa na serikali hii nao pia wameanza kuchukua hatua. Kwa mfano Benki ya Dunia imesitisha msaada wa $50 milioni kwasababu ya sheria ya kipuuzi ya takwimu, tutapiga kampeni pia watu wa nje waanze kuweka vikwazo kuhusu matukio ya uchaguzi.
 
Hakuna kilichopitwa na wakati, CHADEMA itaendelea kushinda uchaguzi hata kama haitandangazwa mshindi. Watu wa nje pia wanaona upuuzi unaofanywa na serikali hii nao pia wameanza kuchukua hatua. Kwa mfano Benki ya Dunia imesitisha msaada wa $50 milioni kwasababu ya sharia ya kipuuzi ya takwimu, tutapiga kampeni pia watu wa nje waanze kuweka vikwazo kuhusu matukio ya uchaguzi.
Hakuna nchi ya nje itakayofanya chochote! Wako kimaslahi na hawawezi kuvuruga maslahi yao kwa vitu kama hivi. Zanzibar matokeo yalibadilishwa mchana kweupe na hakuna kilichotokea! Watanzania hatuna tabia ya kusoma vitabu. Ungekuwa msomaji ungefunguka macho jinsi nchi za magharibi zinavyofanya kazi.
 
Hakuna nchi ya nje itakayofanya chochote! Wako kimaslahi na hawawezi kuvuruga maslahi yao kwa vitu kama hivi. Zanzibar matokeo yalibadilishwa mchana kweupe na hakuna kilichotokea! Watanzania hatuna tabia ya kusoma vitabu. Ungekuwa msomaji ungefunguka macho jinsi nchi za magharibi zinavyofanya kazi.

Naamini vikwazo vitafanya kazi na huku kunyimwa $50 milioni ni mwanzo tu. Sikusikia Zanzibar wakiwekewa vikwazo lakini hayo yameshapita, cha msingi sisi tumeshaanza kuwekewa vikwazo na sisi tutazidi kuwaomba wafadhili wazidi kubana. Kama Saddam na Gaddafi waliondolewa hakuna anayeshindikana.
 
Naamini vikwazo vitafanya kazi na huku kunyimwa $50 milioni ni mwanzo tu. Sikusikia Zanzibar wakiwekewa vikwazo lakini hayo yameshapita, cha msingi sisi tumeshaanza kuwekewa vikwazo na sisi tutazidi kuwaomba wafadhili wazidi kubana. Kama Saddam na Gaddafi waliondolewa hakuna anayeshindikana.
Unajua kilichofanya kina Sadam wakaondoka? Naona uko ulimwengu mwingine kabisa.
 
Watanzania ni wanafiki na malimbukeni wanaopenda mteremko kwenye kupata mafanikio....

Mlilia lia kikwete fisadi, huduma mbovu, wenye nacho wanasikilizwa kuliko wasionacho mkawa mnaomba usiku kucha atoke rais wa tofauti mkalli asiwe legellege like kikwete amepatikana mnaanza kulalamika ooh mara ivi mara kilikwenda kimerudi pumbavu kabisa.

Magufuli kanyaga mafuta twende wasikutishe.
Hahaaaa! Mkuu umenifanya nicheke. Watz tumezidi kulalamika
 
God forbid! Ninaamini kwa dhati kabisa unayedhani unamtetea hakubaliani hata kidogo na mtazamo wako wa kutisha raia wemà. Binafsi sijaona chokochoko yoyote hapo tofauti na maonì binafsi. Nadhani kauli kama hizi ķamwe haziujengi utawala huu. Badala yake zinaufanya kuonekana tofauti kabisa na nyingine zote zilizotangulia; tofauti kabisa na utamaduni wa kisiasa wa nchi hii.
Mkuu huyo Jmc06 haijaanza leo hawezi kuchangia hoja yeyote kazi yake na mwenzake TumainiEli ni kutafuta wachangiaji ndani ya JF na kuwatisha.
 
Hakuna nchi ya nje itakayofanya chochote! Wako kimaslahi na hawawezi kuvuruga maslahi yao kwa vitu kama hivi. Zanzibar matokeo yalibadilishwa mchana kweupe na hakuna kilichotokea! Watanzania hatuna tabia ya kusoma vitabu. Ungekuwa msomaji ungefunguka macho jinsi nchi za magharibi zinavyofanya kazi.
Kwa vile nchi za nje haziwezi kufanya chochote ndiyo sababu inayokipa kiburi serikali kuendelea kupindua matokeo na kufanya inavyotaka au kuna sababu zingine.
 
Afrika inajulikana kuwa na marais wanaokaa madarakani kwa muda mrefu kama, Yahya Jammeh wa Gambia, Robert Mugabe wa Zimbabwe, na Yoweri Museven wa Uganda, Kwa Afrika ni nadra sana rais kuondolewa kidemokrasia kwa sanduku la kura kabla ya kipindi chake kuisha.

Lakini kuna marais wa Afrika waliodumu madarakani kwa kipindi mfupi kati ya siku mbili hadi miaka minne au muhula mmoja kwa sababu mbalimbali kama mapinduzi ya kijeshi, kifo, uchumi, kuuawa (assassination), utawala mbovu.

Christopher Elnathan Okoro Cole wa Sierra Leone aliyekuwa Jaji Mkuu wa nchi hiyo April 1971 aliapishwa kuwa rais na siku mbili baadaye akajiuzulu na kumkabidhi madaraka waziri mkuu Siaka Stevens.

Yusuf Kironde Lule wa Uganda alikuwa rais wa Uganda kwa siku 68 tu (April 13 -June 20, 1979), wananchi walimkataa, 'he became unpopular', aliondolewa na bunge.

Robert Guei – Ivory Coast alikuwa rais kwa miezi 10 tu, December 24th 1999-october 26, 2000), alishindwa kwenye uchaguzi na Laurent Gbagbo.

Michel Djotodia alikuwa rais wa Central African Republic kwa miezi 9 tu, (March 24, 2013 - January 10, 2014) aliingia kwa kuipindua serikali, aliondolewa na umoja wa mataifa baada ya kushindwa kukomesha mauaji ya kidini.

Ernest Adegunle Oladeinde Shonekan alikuwa rais wa Nigeria kwa miezi 3 tu, (August 26, - November 1993) baada ya Gen. Ibrahim Babangida kulazimishwa kujiuzulu na wananchi, na yeye alikuja kuondolewa na jeshi sababu ilikuwa kudorola kwa uchumi.

Gen. Tito Okello aliyekuwa kiongozi ndani ya jeshi la Uganda alimpindua Milton Obote, Okello alikuwa rais wa Uganda kwa miezi 5 tu, (July 29, 1985 January 26, 1986). Aliondolewa na waasi wakiongozwa na Yoweri Museven ambaye hadi leo bado rais.

Thomas Sankara wa Burkina Faso aliingia madarakani mwaka 1983 kwa mapinduzi ya kijeshi, aliwaahidi wananchi kuleta mapinduzi ya kiuchumi, October 15, 1987 aliuawa na wajeshi.

Melchior Ndadaye wa Burundi, alikuwa rais Mhutu wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia, alidumu madarakani kwa miezi 3 tu, (July 10, 1993 - October 21, 1993). Aliuawa na wanajeshi wa Kitusti.

Mohamed Morsi alikuwa rais wa kwanza wa Misri wa kuchaguliwa kidemokrasia, aliingia madarakani June 30, 2012 baada ya nguvu ya umma kumwondoa dikteta Hosni Mubarak, wananchi waliamini kuwa labda Morsi atakuja kuwa kiongozi mzuri kwao. Baada ya Morsi kupewa madaraka alibadili katiba na kujipa madaraka yote, kila kitu aliamua yeye bila kulihusisha bunge, mahakama wala vyombo vya sheria. Aliwakamata na kuwaua wote aliokuwa wakimpinga.

"Morsi issued a temporary constitutional declaration that granted him unlimited powers and the power to legislate without judicial oversight or review of his acts, stating that such a move was necessary in order for him to protect the nation from the Mubarak-era power structure, which he called "remnants of the old regime".

Kutokana na utawala wake wa mabavu wa kutofuata sheria Morsi alishitakiwa na ilipofika May 2015 alihukumiwa kunyongwa na mahakama ya nchi yake.

Mkuu,

Wewe, Tindo na yule mwenye avatar ya yule msichana wa Pakistani nyote mna mawazo mazuri sana na nnawapenda kwa kuwa na mawazo ya kuchagiza.

Mnachokosea tu, ni namna ya kuyawasilisha mawazo yenu na sijawahi kuona mnatoa matusi wala lugha ya kashfa.

Si ninyi ambao mnafanya hivyo bali wenzenu wenye mawazo kama yenu.

Ondoeni "contents" zenye kuchochea, kukashifu, kutukana, kutisha na kukejeli serikali iliyopo madarakani.

Kwa mfano umeweka kichwa cha mada yako kikielezea viongozi wa Afrika ambao hawakudumu madarakani na ukasema " Will Magufuli take a course?

Unamaanisha kwamba je Raisi Magufuli nae atafuata mkondo?

Sasa kwa tafsiri ya hicho kichwa cha habari na yaliyomo humo ni mapinduzi, kuondolewa kwa nguvu viongozi na hata kuuawa kwa mmoja wa viongozi hao.

Na unamwambia raisi Magufuli kwamba na yeye atafuata mkondo, wamtisha raisi wako? waitishia mamlaka? je watishia taasisi ya uraisi?

Hivyo ndivyo baadhi ya wageni na wanachama wengine watakuwa wanaweza.

Usidhani ni sisi tu wanachama wa JF twasoma hapa wapo watu wengi wa rika tofauti, kazi tofauti na malengo tofauti.

Tumia njia sahihi ya kuwasilisha maoni yako bila kumkwaza mtu, kumuudhi na hata kufanya akuchukie, hatua ambazo zitajenga uadui uso lazima.

Otherwise, I like you guys and your way of thinking!
 
Back
Top Bottom