Samahani kama nitawakwaza dada zangu wa Kiafrika. Kila ninapotazama picha za wanawake wa siku hizi naona mtindo wa nywele ni zile zilizokaangwa au zile zinazoonekana kama singa za mkia wa farasi. Mfano ni hii picha ya mgombea urais mtarajiwa wa Kenya Martha Karua.
Wanawake wa Kiafrika wana nywele nzuri tu (natural) lakini naona kuna complex na hisia kuwa nywele za kiulaya ulaya ndizo zinazopendeza zaidi.
Ukiangalia picha za walimbwende wengi Dar utakuta ni hizi nywele za kupachikia au nywele zilizokaangwa. Mara chache sana nakutana na mabinti wenye nywele fupi za asili na zinapendeza kwamba I have to take a double look. Kama nilivyosema samahani kama nitawakwaza dada zangu kwa topic hii.