Afghanistan yakumbwa na tetemeko la ardhi la tatu ndani ya wiki moja

Messenger RNA

JF-Expert Member
Jul 24, 2022
1,103
3,023
Tetemeko jipya la ardhi limekumba magharibi mwa Afghanistan - siku kadhaa baada ya mitetemeko miwili mikubwa katika eneo hilo kuua zaidi ya watu 1,000.

Shirika la Utafiti wa Jiolojia la Marekani (USGS) linasema kuwa tetemeko hilo la ukubwa wa 6.3 lilipiga karibu na mji wa Herat. Ilikuwa katika kina cha 6.3km (maili nne).

Takriban mtu mmoja amefariki dunia, kulingana na mamlaka ya afya ya eneo hilo.

Wengine 100 wanatibiwa majeraha katika hospitali ya mkoa, Shirika la Afya Ulimwenguni lilisema.

Zaidi ya 90% ya waliofariki katika tetemeko la awali walikuwa wanawake na watoto, shirika la Umoja wa Mataifa la watoto Unicef lilisema.

Katika ripoti yake, USGS ilisema kitovu cha tetemeko la hivi karibuni kilikuwa kilomita 30 kaskazini-magharibi mwa Herat, mji wa tatu kwa ukubwa nchini Afghanistan karibu na mpaka wa Iran.

Tetemeko la ardhi la Jumamosi iliyopita lilikumba Zindajan, wilaya ya mashambani iliyo umbali wa kilomita 40 kutoka Herat.

Tetemeko hilo liliharibu nyumba zote, ambazo zilikuwa dhaifu sana kuweza kustahimili, zikiwa zimebaki vifusi.

Wanakijiji walitumia majembe na mikono mitupu kutafuta watu waliopotea.

Baada ya tetemeko hilo la ardhi, wakazi wengi walikuwa wamelala mahali pa wazi. Kundi la Taliban, ambalo limekuwa likitawala Afghanistan tangu 2021, lilisema wengi sasa wako kwenye mahema na baridi inapoanza, huenda hawataweza kuhimili hali kwa zaidi ya mwezi mmoja.

Afghanistan imekuwa ikiyumba kutokana na mzozo wa kiuchumi tangu Wataliban waingie madarakani, wakati msaada uliotolewa moja kwa moja kwa serikali ulipositishwa.

Nchi hiyo hukumbwa na matetemeko ya ardhi mara kwa mara, haswa katika safu ya milima ya Hindu Kush, kwani iko karibu na makutano ya mabamba ya mwamba ya Eurasia na India.

Mwezi Juni mwaka jana, jimbo la Paktika lilikumbwa na tetemeko la ukubwa wa 5.9 ambalo liliua zaidi ya watu 1,000 na kuwaacha makumi kwa maelfu bila makazi.
BBC Swahili
 
Kuna nchi zinapitia mabalaa, mara matetemeko mara vita, mara utawala wa mabavu...

Watu wa huko hawana hata pa kupumulia...
 
Tutawaelewaaa taratibu taratibu watoto wa mzeee jakobooo.......
A.k.A Israel
 
Back
Top Bottom