Afande Bageni akwama tena; Ombi: Asinyongwe

Jaribio la pili la aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni (OC-CID), Christopher Bageni kujinasua na adhabu ya kunyongwa, baada ya kutiwa hatiani kwa kuwaua wafanyabiashara watatu wa madini na dereva teksi, limekwama katika Mahakama ya Rufani juzi.

Mahakama hiyo ya juu kabisa nchini, imeyaondoa mahakamani maombi aliyofungua Bageni, akitaka hukumu iliyomtia hatiani irejewe upya.

Ilieleza kuwa sababu zake za kuiomba ibadilishe hukumu hiyo hazikuwa na mashiko ya kisheria, kwani Bageni alifungua maombi mengine ya marejeo akiomba jambo lilelile.

Majaji Gerald Ndika, Mwanaisha Kwariko na Barke Sehel, waliosikiliza maombi hayo waliridhika na hoja ya Jamhuri kuwa maombi hayo yalifunguliwa nje ya muda.

Bageni na askari wenzake 12, akiwamo aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Abdallah Zombe walishitakiwa mwaka 2006 kwa mauaji ya wachimba madini watatu kutoka Mahenge, Morogoro.

Hili ni jaribio la pili la kachero huyo la kutaka uhuru, baada ya maombi yake ya kwanza kutupwa na mahakama hiyo Septemba 2019 kwa kutokuwa na mashiko kisheria.

Katika kuishawishi mahakama, Bageni, katika maombi yake ya pili aliambatanisha uamuzi wa kesi iliyowahi kuamriwa na mahakama hiyo inayoonesha kuwa mahakama inaweza kusikiliza maombi ya marejeo juu ya maombi mengine ya marejeo.

Hata hivyo, jitihada zake ziligonga mwamba juzi baada ya Mahakama ya Rufani kuibua hoja juu ya usahihi wa maombi hayo na hivyo kulazimika kuyaondoa mahakamani.

Wakili wa Serikali Mkuu, Monica Mbogo alileta pingamizi akieleza kuwa mwombaji huyo tayari alikwishafungua maombi kama hayo yaliyokwishaamriwa, hivyo hakuwa na haki ya kisheria kufungua maombi mengine kama hayo.

Bageni, ambaye hakuwakilishwa na wakili, alipingana wa wakili huyo wa Serikali akidai Serikali haikuwa na sababu za msingi.

“Maombi haya yameletwa tangu mwaka 2019 na tayari yalikuwa yasikilizwe juzi. Sasa Serikali kuja leo na pingamizi hili ni mbinu tu ya kutaka kuchelewesha usikilizwaji wa maombi haya. Hivyo naomba muone kwamba Serikali haina sababu ya msingi na myakatae,” alisema Bageni.

Hata hivyo, baada ya ufafanuzi wa mahakama kuhusu umuhimu wa kusikiliza pingamizi hilo, Bageni aliridhia na kuamua kuondoa pingamizi lake na mahakama ikalipokea pingamizi hilo la Serikali.

Kiongozi wa jopo la majaji, Jaji Ndika alieleza kuwa mbali na pingamizi hilo la Serikali, mahakama nayo ilikuwa na hoja yake ya msingi, ikitaka kwanza kujua iwapo maombi ya Bageni yaliwasilishwa ndani ya muda wa siku 60 baada ya hukumu ya kwanza kama sheria inavyotaka.Katika marejeo ya pili, Bageni alikuwa akiiomba mahakama irejee uamuzi wake wa rufaa aliyokata Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) na kuamriwa Septemba 16, 2016 na maombi yake hayo ya marejeo ya pili aliyawasilisha Oktoba 10, 2019, miaka mitatu na mwezi mmoja baadaye.

Baada ya maelezo hayo, Bageni alikiri kuwa maombi yake yaliwasilishwa nje ya muda na akaridhia yaondolewe ili akajipange upya.

“Baada ya majadiliano na mahakama, mleta maombi (SP Bageni) amekubali kuyaondoa mahakamani chini ya kanuni ya 58(1) ya Kanuni za Mahakama ya Rufani. Mjibu maombi hakuwa na pingamizi,” alisema Jaji Sehel, aliyesoma amri ya mahakama na kongeza:

“Nasi tumekubaliana na maombi ya mleta maombi. Hivyo kwa mujibu wa kanuni ya 58(1) ya Kanuni za Mahakama za Mahakama ya Rufani, tunayaondoa maombi haya.”

Haikuweza kufahamika mara moja kama Bageni alimaanisha kuwa atafungua maombi mengine au la, pale alipoomba muda wa kwenda kujipanga upya.

Kama bado anataka kuendelea na kesi hiyo, Bageni atapaswa kwanza kuwasilisha mahakamani maombi ya kibali cha kufungua maombi ya marejeo nje ya muda na kutoa sababu zitakazoishawishi mahakama kwa nini alichelewa kufungua maombi yake hayo ndani ya muda.

Juzi mahakama ilidokeza kuwa hata akifanikiwa kuishawishi ikubali afungue maombi ya marejeo nje ya muda, askari huyo atakabiliwa na kiunzi kingine cha kuishawishi mahakama kuwa ana weza kufungua maombi ya marejeo juu ya maombi mengine ya marejeo.


Mwananchi
Unamuita mfungwa afande au ni mhalifu mwenzio
 
Jaribio la pili la aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni (OC-CID), Christopher Bageni kujinasua na adhabu ya kunyongwa, baada ya kutiwa hatiani kwa kuwaua wafanyabiashara watatu wa madini na dereva teksi, limekwama katika Mahakama ya Rufani juzi.

Mahakama hiyo ya juu kabisa nchini, imeyaondoa mahakamani maombi aliyofungua Bageni, akitaka hukumu iliyomtia hatiani irejewe upya.

Ilieleza kuwa sababu zake za kuiomba ibadilishe hukumu hiyo hazikuwa na mashiko ya kisheria, kwani Bageni alifungua maombi mengine ya marejeo akiomba jambo lilelile.

Majaji Gerald Ndika, Mwanaisha Kwariko na Barke Sehel, waliosikiliza maombi hayo waliridhika na hoja ya Jamhuri kuwa maombi hayo yalifunguliwa nje ya muda.

Bageni na askari wenzake 12, akiwamo aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Abdallah Zombe walishitakiwa mwaka 2006 kwa mauaji ya wachimba madini watatu kutoka Mahenge, Morogoro.

Hili ni jaribio la pili la kachero huyo la kutaka uhuru, baada ya maombi yake ya kwanza kutupwa na mahakama hiyo Septemba 2019 kwa kutokuwa na mashiko kisheria.

Katika kuishawishi mahakama, Bageni, katika maombi yake ya pili aliambatanisha uamuzi wa kesi iliyowahi kuamriwa na mahakama hiyo inayoonesha kuwa mahakama inaweza kusikiliza maombi ya marejeo juu ya maombi mengine ya marejeo.

Hata hivyo, jitihada zake ziligonga mwamba juzi baada ya Mahakama ya Rufani kuibua hoja juu ya usahihi wa maombi hayo na hivyo kulazimika kuyaondoa mahakamani.

Wakili wa Serikali Mkuu, Monica Mbogo alileta pingamizi akieleza kuwa mwombaji huyo tayari alikwishafungua maombi kama hayo yaliyokwishaamriwa, hivyo hakuwa na haki ya kisheria kufungua maombi mengine kama hayo.

Bageni, ambaye hakuwakilishwa na wakili, alipingana wa wakili huyo wa Serikali akidai Serikali haikuwa na sababu za msingi.

“Maombi haya yameletwa tangu mwaka 2019 na tayari yalikuwa yasikilizwe juzi. Sasa Serikali kuja leo na pingamizi hili ni mbinu tu ya kutaka kuchelewesha usikilizwaji wa maombi haya. Hivyo naomba muone kwamba Serikali haina sababu ya msingi na myakatae,” alisema Bageni.

Hata hivyo, baada ya ufafanuzi wa mahakama kuhusu umuhimu wa kusikiliza pingamizi hilo, Bageni aliridhia na kuamua kuondoa pingamizi lake na mahakama ikalipokea pingamizi hilo la Serikali.

Kiongozi wa jopo la majaji, Jaji Ndika alieleza kuwa mbali na pingamizi hilo la Serikali, mahakama nayo ilikuwa na hoja yake ya msingi, ikitaka kwanza kujua iwapo maombi ya Bageni yaliwasilishwa ndani ya muda wa siku 60 baada ya hukumu ya kwanza kama sheria inavyotaka.Katika marejeo ya pili, Bageni alikuwa akiiomba mahakama irejee uamuzi wake wa rufaa aliyokata Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) na kuamriwa Septemba 16, 2016 na maombi yake hayo ya marejeo ya pili aliyawasilisha Oktoba 10, 2019, miaka mitatu na mwezi mmoja baadaye.

Baada ya maelezo hayo, Bageni alikiri kuwa maombi yake yaliwasilishwa nje ya muda na akaridhia yaondolewe ili akajipange upya.

“Baada ya majadiliano na mahakama, mleta maombi (SP Bageni) amekubali kuyaondoa mahakamani chini ya kanuni ya 58(1) ya Kanuni za Mahakama ya Rufani. Mjibu maombi hakuwa na pingamizi,” alisema Jaji Sehel, aliyesoma amri ya mahakama na kongeza:

“Nasi tumekubaliana na maombi ya mleta maombi. Hivyo kwa mujibu wa kanuni ya 58(1) ya Kanuni za Mahakama za Mahakama ya Rufani, tunayaondoa maombi haya.”

Haikuweza kufahamika mara moja kama Bageni alimaanisha kuwa atafungua maombi mengine au la, pale alipoomba muda wa kwenda kujipanga upya.

Kama bado anataka kuendelea na kesi hiyo, Bageni atapaswa kwanza kuwasilisha mahakamani maombi ya kibali cha kufungua maombi ya marejeo nje ya muda na kutoa sababu zitakazoishawishi mahakama kwa nini alichelewa kufungua maombi yake hayo ndani ya muda.

Juzi mahakama ilidokeza kuwa hata akifanikiwa kuishawishi ikubali afungue maombi ya marejeo nje ya muda, askari huyo atakabiliwa na kiunzi kingine cha kuishawishi mahakama kuwa ana weza kufungua maombi ya marejeo juu ya maombi mengine ya marejeo.


©Mwananchi

Huyu Mshenzi nashangaa kwanini rais mpaka sasa hajadondoka wino apigwe kitanzi ,yeye na zombe wameua wanafamilia watatu na kuwapora mil 200 pamoja na madini na kuwasingizia ni majambazi.
 
Nishawahi kusumbuana naye huyu
Alikuwa mkuda balaa bila kuwa na tag
Angenimaliza Hahaha

Sjui alingia vp mkenge kwenye kesi hii
Maana alikuwaga anasimamia Sana kazi
Yake,ukitaka kmpeleka kule hapokei
Labda kama alikuja badilika

Ova
Baada ya kila sijaelewa
 
Bageni na askari wenzake 12, akiwamo aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Abdallah Zombe walishitakiwa mwaka 2006 kwa mauaji ya wachimba madini watatu kutoka Mahenge, Morogoro.
Nilimkuta siku moja Morogoro sehemu moja inaitwa Moseka amefunga vishikizo vya shati vimepishana 🤣 ✍️
 
Nishawahi kusumbuana naye huyu
Alikuwa mkuda balaa bila kuwa na tag
Angenimaliza Hahaha

Sjui alingia vp mkenge kwenye kesi hii
Maana alikuwaga anasimamia Sana kazi
Yake,ukitaka kmpeleka kule hapokei
Labda kama alikuja badilika

Ova
Nishawahi kusumbuana naye huyu
Alikuwa mkuda balaa bila kuwa na tag
Angenimaliza Hahaha

Sjui alingia vp mkenge kwenye kesi hii
Maana alikuwaga anasimamia Sana kazi
Yake,ukitaka kmpeleka kule hapokei
Labda kama alikuja badilika

Ova
Mkuu angalia chanel ya hiyo case ndo utajua aliingiaje,
Hii ilianzia juu kwa wakubwa wake wa kazi maboss zake kina zombe,
So ni either uwe nasi ule mema ikitiki,
Au utukatae tukupoteze.
 
Ilinisikitisha sana hiyo taarifa na walimuua dereva wa taxi wa sinza pale ndio watu wakastuka yule dereva sio jambazi ila wapo wafanyabiashara wa madini wa mahenge kwa kipindi kirefu wakija anakua njema kumbe manjagu walikua wanawalia timing wawaue wote huko mahenge walikaa kimya mpaka Sinza ilipolipuka nao wakajitokeza...
 
Nishawahi kusumbuana naye huyu
Alikuwa mkuda balaa bila kuwa na tag
Angenimaliza Hahaha

Sjui alingia vp mkenge kwenye kesi hii
Maana alikuwaga anasimamia Sana kazi
Yake,ukitaka kmpeleka kule hapokei
Labda kama alikuja badilika

Ova
ndio uweke akiba ya maneno,maisha haya yana mambo mengi mno.

sio unahukumu kindezi mtu unayemjua kama hao wapuuzi wengine.

polisi wana visa vingi vya kujifunza,lakini hili la bagemi ni ukiritimba tu.
 
Mkuu angalia chanel ya hiyo case ndo utajua aliingiaje,
Hii ilianzia juu kwa wakubwa wake wa kazi maboss zake kina zombe,
So ni either uwe nasi ule mema ikitiki,
Au utukatae tukupoteze.
Hivi nani walikuwa ma boss zake na Zombe!?
 
Mkuu,waerevu kwenye jeshi la polisi ni wa kuhesabu.
Si nasikia wanafanya kazi kwa amri!? Sasa huo uwerevu utatoka wapi!? Na hata kama ni mwerevu lakini Kesha pewa amri ya kipumbavu,hata yeye nafsi inakua inamsuta,lakini afanyeje,lazima atekeleze amri aliyopewa na Wakubwa zake!! Au siyo hivyo!?
 
Back
Top Bottom