Afa akifanya mapenzi gesti

Afa akifanya mapenzi gesti

Jana kuna mdau alileta uzi wa watu wanaozini hufa,sijui ameupata kwa MJAPANI
 
MFANYABIASHARA wa sokoni Kariakoo jijini Dar ambaye pia ni mkazi wa Kigogo Flesh, Hamad Kiponda (46), amefia nyumba ya kulala wageni akiwa na mpenzi wake Latifa Saidi (25).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi alisema tukio hilo lilitokea juzi saa saba mchana katika nyumba hiyo iitwayo Sansiro iliyoko Kiwalani kwa Gude.

Alisema kuwa kutokana na tukio hilo, Latifa alitoa taarifa polisi kwamba mpenzi wake aliishiwa na nguvu ghafla na kuanza kutokwa povu mdomoni wakati wakifanya mapenzi.

Minangi alieleza kuwa mtoa taarifa huyo aliomba msaada kwa wahudumu wa gesti hiyo, lakini Kiponda alifariki papo hapo kabla ya kupelekwa hospitali.

Chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika, wakati mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi huku Latifa akishikiliwa kwa kuhojiwa.

Source:Tanzania Daima Afa akifanya mapenzi gesti

HIYO NDIO UNGA CHUNGU MAANA VUNJA CHUNGU ILISHAPITA

Angeendelea na SITA angekuwa akinunua vitu kwa futari ya jioni hii. Kafungulia kila kitu.
 
46 - 25 = 21

Mmmh huyo si kama mwanaye kabisa!!!
 
Lazima bibie alizidisha ufundi baada ya kukaa mwezi bila hiyo kitu,jamaa kafroti halafu mpenzi akajua jamaa anaongeza korasi kumbe anamrestisha ini pisi haki ya nani...
 
Kama ameacha familia ni jambo la aibu sana, ila biblia inasema "asiye na dhambi na awe wa kwanza kurusha jiwe" wengi tunashiriki mechi za mchangani ila zamu zetu hazijafika na tuombe tusifikwe na mwisho mbaya wa namna hii maana aina ya kifo ni kiashiria cha amali ulizozitanguliza mbele ya haki.
 
Kweli king Kong III huyu mtu atuambie aliponaje, na alivyotumia alijisikiaje.
 
Uzinzi umezidi tukisema mnashinda na njaa hamfungi mnalalamika hya aibu hyo juu yenu.
 
RIP MTOA HUDUMA! BILA WAHUDUMU KAMA WEWE SISI AMBAO HATUOLEWA TUTAHUDUMIWA NA NANI??LAZIMA TUBANANE HUMOHMO:rip:
 
Amekufa kishujaa kama ditopile mzuzuri.
 
Kafa na kithibit cha kuvunja amri ya sita, cjui atajitetea je?
 
Heri ufe kuliko demu akufie gesti! Usiombe ikukute, ni balaa! Tusimcheke huyu jamaa, sisi wote ni wazinzi tu, hatujui lipi litatukuta sisi. Eeh! MUNGU baba tusamehe maovu yetu. Amina.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom