Adult Talks: Kwa kupitia ndoa yako. Unawashauri vipi ambao hawajaoa?

Ndoa bhana ni kitu tata sana wakuu!!!!mtu aoe kwa matakwa yake na si kulazimishwa.

Mimi nimeishi na mwanamke kwa miaka 8 ila nimemuacha yapata miezi 3 sasa na siku 4.tulibahatika kupata watoto 2(ke/me),ila changamoto mi nilikuwa nazo tangu mwanzo huku mwisho uvumilivu ukanishinda ikanibidi kila mmoja achukue hamsini zake.

Mwanamke hakuna unachompa akafanikiwa.ni lazima afeli,hajui kujisimamia ila haya yote niliyakubali sababu ni chaguo langu mwenyewe sikulazimishwa na mtu.

Nimemuacha sababu ya kunipangia masharti ya kurudi nyumbani kuzidi,na kuninyima unyumba kupindukia.

Nikaona tunakozidi kwenda kutakuwa kubaya zaidi,kiroho safi kaniachia wanangu na uzuri hajawahi hata kuwaandaa kwenda shule ni majukum ambayo nilikuwa na ninayafanya mwenyewe nikaona poa tu.

Niko na wanangu miezi mitatu sasa hawajawahi kuuliza mama yao yuko wapi wala anarudi lini.tunaishi nafurahi nao safi kabisa.

Cha ajabu na nilichokuja kujua nilikuwa naishi na kichwa box leo hii kaenda kuwa house maid sehemu daah!!! Kaacha wanae ambao hajawahi kuwaanda kwenda shule,kaenda kuwaandaa wa mwanamke mwenzie.

Wakuu kuoa ruksa ila angalieni mnapooa/kuolewa.hii taasisi ni pana na ngumu mno.
Aise!
 
Leta nondo mkuu
Kwanza niwaombe radhi baadhi ya Wana jf maana Kuna waliooa na wale ambayo hawajaoa ama kuolewa yawezekana maneno yangu yakawakwaza lakini ukweli ndo huo
1 enzi zile kbla ya kutoa ulifanyika uchunguzi wa kina kwa muoaji au muolewaji ili kujua tabia
2 magonjwa ya kurithi Kama ukoma kifafa na mengineyo
3 uvivu na uzinzi pia wizi
Kuhusu kuoa usikurupuke kuoa make ambae kwao Wana maswali Kama haya,
Unafanya kazi wapi na kazi gani hapo fahamu siku ukifukuzwa kazi Basi ujue make nae lazima akuache
2 una nyumba au Mali na Mambo mengine yanayoendana na kipato ujue siku ukifilisika na make huna
Jambo la mwisho kwa leo make wa kuoa haonjwi jamani na nyie Dada zetu msijirahisi kuonjesha miili yenu hapo ndio mwanzo wa kuitwa Malaya maana utaonjwa na wangapi? Kila mmoja akikuonja mwisho wa siku zinamfikia mchumba mwingine ambaye huenda angeposa anaambiwa hata Audi alishaonja mzigo Leo mkuu niishie hapo nitendelea siku nyingine ili jamii ijifunze.
 
Vijana oeni mapema,ni muhimu sana kuoa not more than 25 yrs kwa m/me na mwanamke not more than 22.

Kwa umri huo kwanza mtafyatua fasta fasta ,umri huo hakuna compliations za ujauzito ,ukigusa tu imooo na akienda kujifungua fasta tu...Mpaka mkifika 30 mshamaliza uzazi...ilichobaki ni kulea.....Hadi mtoto anaanza kujitegemea wazazi wanakuwa < 45 bado wana nguvu na kuwapa vijana wao kujijenga na kutowategemea watoto.
 
Kuna upendo,na upendo wa dhati... upendo wa kawaida una vitu vingine vya ziada vinavyosababisha ndoa kuwepo, mfano,pesa,u handsome,chura,elimu n.k,
Huu upendo huchoka hasa baadhi ya mambo yanapopungua au kuisha,baada ya miaka fulani, ndio ambao huwa wamoto wenye kuachana ,kuuana,kufumaniana n.k

Huu wa dhati hauna mwisho,unaweza kufirisika,kupata ulemavu,n.k lakini hakuna kuachana,mpaka kifo.
Usiombe mtu akose upendo wa dhati, mshua wetu kapitia misala mingi sana na bado anavumilia.
 
Code:
4/ Usioe mwanamke uliyetafutiwa au kuunganishwa nae na rafiki yako au ndugu yako yeyote yule tofauti na Mama yako mzazi....... utanishukuru baadae.

Umesema kweli
 
Nawashauri vijana kwanza wabalishe tabia,kama wana tabia mbaya zote waziache kisha waanze kutafuta wenza wenye tabia nzuri.

Lingine vijana wawahi kuoa katika raha miongoni mwa raha za dunia ni kuoa mapema yaani katika umri mdogo.
"Lingine vijana wawahi kuoa katika raha miongoni mwa raha za dunia ni kuoa mapema yaani katika umri mdogo."

Una uhakika na hili?
 
"Lingine vijana wawahi kuoa katika raha miongoni mwa raha za dunia ni kuoa mapema yaani katika umri mdogo."

Una uhakika na hili?
Mimi shahidi wa hili. Nina uhakika wa "mia fil mia".
 
Mimi shahidi wa hili. Nina uhakika wa "mia fil mia".
Yaan kijana aoe ana miaka 25 mpaka kufika miaka 65 huko si atakua ashamchoka mkewe (watakua wamechokana)
Afu kibongobongo ,kijana wa miaka 25 either anaishi kwao au ndo anaanza maisha hana kazi ya kueleweka, kipato cha kuunga unga, n vp atalipa bills?
 
Mimi huwa tunagombana na mwenzangu ila uzuri hatununiani,maswala yetu bado hatujawahi kuita watu kutusuluhisha tunamalizana wenyewe...ila msije mkajidanganya ndoa is a paradise ni mixer ya paradise na hell kidogo kidogo kikubwa kubebeana madhaifu kusameheana ukiingia uwe na mentality ya Ndoa ni mtihani kama mtihani mwingine hutapata pressure...msitishwe na hizo picha wanapost insta wengi they fake....ndoa ingia ndani ndio utaielewa...
Wasichukulie mahusiano siriaz kiivo unless watakufa siku si zao
 
Ushauri ni kwamba, ukkuklsioe au kuolewa ikiwa hujamaliza ujana. Maliza kwanza ndiyo uingie ndoani.
Hakuna kitu kinauma kaoma usaliti,usaliti ndiyo chanzo cha ndoa nyingi kuharibika.
 
Achana na ile misemo ya mtaani, kwamba kama unapata kila kitu kwenye mahusiano, basi ndoa haina umuhimu. Au wale wanaosema ukishamuweka ndani basi anaota mapembe.

Ukweli ni kwamba huwa inafikia point in this life unahitaji kusettle down. Kwamba hata kama ni kichomi au kivuruge unaamua tu kutulia nae, maana ushazurura sana. Sometime changamoto zinajitokeza mbeleni kabisa, ila wengine wanaanza nazo hizo changamoto, ila baadae zinapotea na wanatulia kwa amani.

Kuna nyumba moja niliwahi kupanga, yule baba mwenye nyumba alikuwa peace sana. Kwenye lile eneo ana nyumba mbili kubwa, moja anakaa na familia yake yenye watoto watano, nyingine ndio tulikaa sisi wapangaji. Kuhusu kodi ya nyumba, alimuachia mkewe ndio awe anachukua ili zimsaidie katika mahitaji ya nyumbani. Yeye Mzee alikuwa anasimamia gharama za uendeshaji mashamba yake na kusomesha watoto. Huyu mama mwenye nyumba alikuwa hapendi kabisa wapangaji wakike. Sometime hata kama kuna chumba kipo wazi, alikuwa anawaambia hapangishi. Alikuwa ni mlevi sana, ikitokea hujalock mlango, unaweza mkuta kajilaza chumbani kwako, hii huwa inatokea sometimes hata kama hajalewa.

Kuna siku nilikuwa napiga story na baba mwenye nyumba, akaniambia kitu kimoja "Jitahidi usije ukakosea kuchagua, kama nilivyofanya mimi baba ako"

Ofcourse mifano ipo mingi, nina broh mtoto wa baba mkubwa ambae alipataga demu kwenye harusi ya binamu. Huyo dem alikunywaga pombe mpaka akazima, ila kabla hajazima alifanya sana vituko. Broh alimsaidia at the end wakawa lovers, siku anatangaza kutaka kumuoa familia nzima iligoma, maana wanajua alipomtoa na vituko alivyofanyaga ambavyo kwa mwanamke ni fedhea. Jamaa alifosi ndoa, ila wakamwambia yakikukuta utajua mwenyewe. Leo hii ndoa yao ina zaidi ya miaka 13, wale waliokuwa wanajiona wamechagua pazuri, washaachana acha wengi tu, plus vikao vikao daily.

BACK TO THE TOPIC

Ningependa kusikia kutoka kwenu dada zangu na kaka zangu mlio kwenye ndoa. Kwamba kwa kutolea mfano ndoa yako, unawashauri nini ambao bado hawajaoa?

Share na wadogo zako, hii elimu ambayo hawatoweza ipata darasani.

Feel free to express anything, walau tuweze jifunza. Real life experience huwa ni mwalimu mzuri sana.

Thanks.

Regards.

Analyse
Ndoa ni mahusiano ya watu wawili actually mwanaume na mwanamke waliopendana, so kwakua kila mmoja wao amekua kwenye mazingira tofauti ni dhahiri kuna wkt watatofautiana kwenye mambo kadhaa cha msingi ni kwmba kabla hujaingia kwenye ndoa walau tengeneza mahusiano na huyo mwenzako yaani ifikie hatua unaona kwakweli huyu namuhitaji kimwili na kiroho muwe bonny n clyde. Then mkiingia kwenye ndoa hakikisha unaendeleza kufurahi nae, nenda nae places kuwa na vipindi vya prayers sometimes vya pamoja na usiache kula mzigo ahahahahah. Pia, hakikisha unatuliza mind kwenye maamuzi mbalimbali ya ishu zinazohusu familia na maendeleo yake aisee usipotuliza mind kwenye decisions utajikuta in big trouble sometimes though sometimes we learn the hard way. So ukiwa unamshirikisha spouse wako kwenye decisions zote za family na kama ulipatia kupata mwenza unaemhitaji utajikuta unaepuka mengi na hata kufanya mambo makubwa mengi. Kingine nenda vacation nae kuna magic sana kwenye vacation ila sio uende huku unawaza au kufanya mambo mengine yanayokua yanakufanya upo busy vacation na kumsahau mwenzako itakua haina maana.
 
Hainaga formula hiyo. Inategemea na tabia zenu wote wawili
 
Back
Top Bottom