Jeshini unapotoka mafunzoni kunakuwaga na kimuhe muhe flani na munkari wa kijinga, usipojizuia unaweza kuleta madhara uraiani hasa unapochokozwa.Mataifa ambayo yana amani ndio utasikia hizi habari za adhabu Kali za RAIA kutoka kwa wanajeshi na hii ni sababu watu wamekuwa trained mda mrefu mambo ya kivita na bila kuiona vita yenyewe kwa hiyo watu wanakuwa na kihemu hemu cha demonstrate waliyojifunza .Dawa pekee ya kuondoa hii ni serikali kuhakikisha wanajeshi wenye balehe ya uwanajeshi wanashiriki utunzaji Wa amani katika katika mataifa yenye machafuko ya kisiasa.
Huo waliofanya huwezi kuuita ukatili kaka. Huyo vibaka na huyo kijana mtukutu huwezi kujua walitaka kumdhuru vipi huyo jamaa yako. Vijana watukutu na vibaka ni washenzi mno kwenye anga zao, ilikuwa ni haki yao kufanywa waliyofanywa. Usiuite ukatili mkuu.Jeshini unapotoka mafunzoni kunakuwaga na kimuhe muhe flani na munkari wa kijinga, usipojizuia unaweza kuleta madhara uraiani hasa unapochokozwa.
Rafiki zangu wawili waliwahi fanya ukatili sana.
Mmoja alimkata kibaka vidole vya mkono.
Mwingine alimvunja kijana mtukutu mguu.
Lakini kwasasa ni wapole sana na wana rank...nzuri so wametulizana
Huna unachojua usijidai mjuajiTanzania hadi ufungue kesi hio labda uende ukafungue kesi kwa kasimu bila hivyo unakusumbua tu, Mahakama inafanya kazi na Jeshi la Polisi usijifanye haujui, ushanielewa lakini au nikwambie tu ulichokiandika kipo kwenye CPA na kwenye Penal Code Ila wakikubanisha lazima wakuchangamshe damu kidogo ili uwe adabu siku nyingine usirudie kufanya ujinga, sawa na mama yako akwambie usichezee kiwembe hicho ukachezea kikakukata akiona umejikata anakuosha kwanza mabanzi ya sura km manne hivi au matano alafu ndio anakupa huduma ya kwanza ili siku nyingine usirudie kufanya ujinga wewe mtoto Mpumbavu, mwanajeshi ampi adhabu za kuchosha raia mtiifu, tembelea shule zilizo karibu na kambi za Jeshi asubuhi mtu km wewe wale watoto unaweza ukasema wanaonewa tena unaweza ukaingilia kati uwaambie jamàa waache kuwapigisha kwata wasiendelee kuburuzwa kwa kuwapigisha gwaride la kufanya kazi za usafi wa shule asubuhi asubuhi na baridi
Ilitokea wapi hii brother?
Wewe kila kitu unabisha,ulipitia malezi mabaya,wazaz wako wanashida mahalaHuo waliofanya huwezi kuuita ukatili kaka. Huyo vibaka na huyo kijana mtukutu huwezi kujua walitaka kumdhuru vipi huyo jamaa yako. Vijana watukutu na vibaka ni washenzi mno kwenye anga zao, ilikuwa ni haki yao kufanywa waliyofanywa. Usiuite ukatili mkuu.
Ukigoma kupewa adhabu hawakufanyi lolote, maana watahisi wewe ni mzaliwa wa mjini, unajielewa na unafahamu haki zako na pengine unajua sheria kabisa.Mie mwenyewe sikubali mtu anizalilishe kisa eti ni mjeda na Kuna wajeda wengine huzalilisha Hadi watu umri wa kuwazaa kabisa eti kisa mjeda. Jamani Mimi sifanyi adhabu yoyote tuone ka wataniua
Mjeda unafurahia jinsi mnavyowahenyesha raia.Hawa Jamaa usiombe uingie kwenye 18 zao, utajuta kuwafahamu.
Siku moja Tulikuwa kwenye foleni ya kuelekea mjini, kuna jamaa wa Lori akaziba geti la kuingilia pale kambi ya Abdallah Twalipo uhasibu. MP akamfuata kistaarabu kabisa "mambo vipi Kaka?" Jamaa akaitikia "Safi kabisa afande". Afande akamuuliza hapa uliposimama si unajua Kama ni getini? Mwamba kwa kujiamini kabisa akaitikia ndiyo afande ila tatizo foleni haitembei, Sina jinsi, samahani sana.
Kama kawaida ya wanajeshi kujifanya wastaarabu kwenye matukio ya aina hii. Afande akamwambia sasa ndugu kwa kuwa foleni haiendi shuka tu hapa upumzike tupige stori, foleni ikitembea utaendelea na safari yako. Dereva wa Lori kwa mbwembwe akafungua mlango ashuke eti apumzike na wanajeshi. Hapo ndiyo 'ntiti' ulipoanza!!
MP akamwambia "kaka sijasema ushuke mlangoni, shukia dirishani" lilikuwa ni tukio la kuchekesha Sana kwa sisi wapita njia ila kwa lililomtokea lilikuwa ni tukio mbaya na la kufedhehesha.
Picha linaanza,gari anayoendesha jamaa ni Scania R 420,Chuma mpya kabisa ya Transit alafu imepanda hewani Kama farasi, imebeba mafuta inaelekea nje. Gari ikisimama dereva unamwona yule kuleee ghorofani. Sasa vuta picha dereva ameambiwa ashuke kupitia dirisha badala ya mlangoni. Sisi wengine wa pembeni Tulicheka Sana maana jamaa kwanza ni bonge alafu ili ashuke kwa kutumia dirisha inabidi ajikusanye awe Kama fungu la nyanya Kisha ndiyo atoe miguu nje. Ilimchukua karibia dakika 15 kushuka. Wakati huo MP alikuwa siriazi hacheki wala haongei. Yeye anamsubiri jamaa tu ashuke wapige stori. Dereva akadondoka chini Kama mzigo wa viazi mbatata vya Mbeya..Tiii!!
Suruali yote imechanika kwenye maungio ya miguu. Aliposhuka huku kijasho kinamtoka mjeda akaanza kupiga nae stori Kama hakuna kilichotokea "naona chuma imeshakunywa wese inasepa?" Dereva kinyonge akajibu yeah inaelekea Ndola, Zambia. Wakapiga stori Mara foleni ikafunguka magari yakaanza kutembea. Afande akamwambia dereva Sasa unaweza kwenda tu maana gari zinatembea. Dereva akatoa shukrani Kisha akaelekea kwenye gari yake asepe.
Cha ajabu wakati dereva anafungua mlango Mjeda akamwambia mzee baba si tulikubaliana tunapitia dirishani? Ahahahhaha kazi ya kupanda dirishani ikaanza tena. Nina uhakika Yule dereva alimtukana mjeda matusi yote ya hapa duniani ila kimoyomoyo.. Ile siku yule dereva hataisahau kamwe maishani.
Unakumbuka kisa chochote Cha wanajeshi na adhabu zao kwa raia pindi raia akijichanganya kwenye anga zao?
Wanajeshi wengi huwa hawajui sheria atakunyanyasa akikutana na wewe ambae umelelewa kwenye misingi ya uoga uoga ila ukikomaa nae mwisho huwa wanaomba radhi na hata fidia unalipwa maana anajua kazi yake inaenda kuharibikaKumbe inawezekana kuwashtaki kunawale wa kututishia tidhia kutukosesha amani dawa Yao n ipi😀
We jidanganye, kwa taarifa yako hayo yana badaka za wakubwa hayo.Afande akileta upuuzi huo unamgomea tu, maana ni kinyume cha maadili ya kazi za jeshi. Hawezi kukufanya lolote. Hawezi kukuua na kama Akikudhuru unamfikisha kwa wakubwa wake tu , uone kama kibarua chake hakijaota nyasi.
Tatizo watu hawajui haki zao na wanaogopa magwanda. Lakini nidhamu za kijeshi zinakataza kabisa askari kuonea raia.
Sa kilometa 50 sinaishilia huko huko ata hivyo mi sifanyi nawaambia nipelekeni mahakamani kama hamtaki niueni mnile na nyama kabisaNyumbu na Msangani malori ya mchanga yalimamishwa na mp halafu dereva akaambiwa amwage mchanga 2ote halafu aujaze kwenye gari kwa viganja vyana mwingine akaambiwa amwage halafu aendeshe gari mita 50 halafu arudi kuchota mchanga koleo 1 akamwage mita 50 mpaka uishe....aliishiwa mafuta ndo akaruhusiwa kuondoka
Yule Mzee alikuwa anajifanya yupo na Vibe sana.. kiherehere kingi, mguu mmoja mpk leo kama yupo hai ule mguu haupo sawa.Babu Ndii mlimuonea mzee wa watu.
Kingekuwa kijiwe cha kawaida siyo wangesumbuliwa tu Kama ulivyoandika,bali pia wangewekewa Hadi vipisi vya bangi mifukoni na mitama wangechezea na kwenye difenda mngepanda.Askari wa Tanzania wengi - ingawa sio wote- hawana adabu, wanapenda kutumia uaskari wao kuonea watu.
Hizi habari zinanikumbusha mbali sana.
Kuna siku tulikuwa tumekaa maskani Upanga, muda wa jioni vijana wanakutana maskani. Mara paap, tukawa tumeaona askari kibao wanakuja kutoka mbali, wako doria kundi zaidi ya ishirini, wamebeba bunduki na marungu.
Basi nikawaambia madogo tuliokuwa tumekaa nao maskani, kama hamjiamini, ondokeni kabisa, wale wanakuja kutaka kututingisha hapa.
Basi kuna madogo wakaondoka, wengine tuliojiamini tukabaki.
Wakaja wakafika maskani, sisi kama kumi, wao zaidi ya ishirini. Mmoja akatuuliza "Haroo, mnafanya nini hapa?".
Basi hawakujua wanaongea na watu wa aina gani, jamaa mmoja wa maskani akamjibu "Afande hivyo ndivyo ulivyofundishwa kusalimia watu?". Ikabidi yule askari astuke kwanza. Alitegemea watu wataogopa, hakutegemea kujibiwa vile.
Sasa akaja askari mmoja, nafikiri ndiye alikuwa mkubwa wao yule, akaanza kuuliza watu, mmoja mmoja, "Wewe unakaa wapi?" Mtu anamwambia hapo, "Wewe unakaa wapi?" Mtu anamwambia hapo. Wakamfikia jamaa mmoja.Wakamuuliza "Wewe unakaa wapi?" Akajibu kwa Baba Ben.
Askari akauliza, "Kwa Baba Ben? Baba Ben gani?" Jamaa akajibu "Kwa Ben huyo huyo wa Jamhuri ya Muungano, kwani wewe unamjua Ben gani mwingine Tanzania?" (Hapo kipindi cha urais wa Ben Mkapa).
Yule Polisi akawa kastuka, kama hajaamini hivi, sasa kumbe kuna wenzake huwa walikuwa wanaenda kulinda kwa Mkapa, wakawa wamemjua yule kijana wa kwa Mkapa. Ikawa kama wanamwambia yule mkubwa wao kwamba huyu tunamjua anakaa kwa Mkapa, tunamuona tukienda kulinda pale.
Basi hapo hapo nikaona wale polisi wanabadilika mara moja, wanasema unajua wazee ni suala la kufahamiana tu, tulikuwa tunajuana tu, hamna tatizo, hamna tatizo tulikuwa tunatambuana tu.
Kuanzia siku hiyo mpaka kituoni kwao kile kijiwe walikiwekea alama ya X kisiguswe, wakasema hapa kuna watoto wa Mkapa huwa wanakaa.
Nikasema hapa ingekuwa wamewakuta watu wasio na majina wangewasumbua sana.
Nimecheka Sana asee.Kuna jamaa alitaka kuovertake msafara wa wajeda barabara ya Iringa~Dar, kabla hajamaliza kuyapita magari yao mbele gari ikatokea ikabidi abane katikati ya wajeda. Aloo walimwambia nae Kawa part ya msafara wao Hadi DSM wakati jamaa alikua anaishia Moro.
Wewe unajua nini ulichoandika kipo kwenye CPA na imeelezwa vizuri Kanuni ya Adhabu pia imeelezea adhabu zipi zitolewe kwa wanaoenda kinyume na sheria zilizowekwa kwa ulinganifu na CPA, unapoelezea sheria ujue na statue zake sio kukariri tu kwenye Kibanda Cha kashata na kahawa ukisikia hili umenasa km sumakuHuna unachojua usijidai mjuaji
Mie nimekosea sitaki kuzalilishwa waniadhibu kiutaratibu na ikiwa mwanaume namgeuzia kesi kabisa yakutaka kunibaka kabisa.Ukigoma kupewa adhabu hawakufanyi lolote, maana watahisi wewe ni mzaliwa wa mjini, unajielewa na unafahamu haki zako na pengine unajua sheria kabisa.
So wataishia kukupiga piga mkwara fulani mwisho wa siku watakuacha uondoke kwa kukupa onyo kwamba siku nyingine usirudie kufanya kosa ulilolifanya siku hiyo.
Wakuja akiona gwanda tu anakimbilia kulia na kumshika miguu mjeda mwenyewe kwamba amsamehee, na mjeda akiona hivyo ana take advantage ya kumuonesha kwamba yeye ni nani kwa kumpa adhabu ambazo zipo kinyume na sheria.