Adhabu gani inamfaa mwanamke huyu?

Adhabu gani inamfaa mwanamke huyu?

Pillato

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2021
Posts
333
Reaction score
310
Ulianza mahusiano naye akiwa tayari ana mimba ya mwezi mmoja,wakati huo wewe hukujua lolote kuhusu mimba,miezi mitatu baadaye mtu wake anakuja kugundua kwamba Demu wake ana anachepuka nawewe,anambwaga yeye pamoja na mimba yake.

Demu anakusimulia kila kitu anakuomba pesa ili akachomoe mimba kwa madai kwamba hana uwezo kujihudumia yeye akiwa na mimba pamoja na mtoto atakayezaliwa,Unamshauri asitoe mimba utamsaidia kila kitu,demu anakubali na kushukuru sana, Baada ya kukubali nawewe unachomeka haja ya moyo wako, unamwambia bibie "mtoto akishafikisha miaka mitatu itabidi nikuoe, Demu anakubali na kuendelea kushukuru.

Mtoto anazaliwa sura kama ya baba yake, baada ya kutimiza miaka mitatu unamwambia bibie," Mtoto keshatimiza umri ambao tulishakubaliana kuoana inabidi nije kwenu nijitambulishe rasmi tuanze maisha ya ndoa, Anakujibu "Samahani najua nitakukwaza sana suala la kuoana haliwezekani kwasasa, baada baba yake mtoto kugundua mtoto ni wake alikuja tukamaliza tofauti zetu, na tumekubaliana kuoana mwakani, kilichonifanya nikubali kurudiana naye ni kitu kimoja tu sipendi kuzaa watoto kwa baba tofauti,nilikubali kuoelwa na wewe kwasababu sikuwa na namna nyingine.

Ukweli ni kwamba nakupenda sana na nathamini sana msaada wako,nakushukuru sana kwa moyo wako wa upendo please usiniache,sipo tayari kuachana nawewe hata nikiolewa, bila wewe pengine ningeshakufa nikitoa mimba hata nisingekufa lakini huyu mtoto asingekuwepo, Sina cha kukulipa zaidi ya kukuombea kwa Mungu.

Ni ndefu sana nisikuchoshe, Utafanya nini?
 
Jilaumu wewe wala mwanamke Hana makosa uliamua kubeba dhambi ya mtu sasa inakutafuna mwenyewe Kwa ushauri jitibu jeraha ulilolipata na kuanza maisha mapya.

Nikuulizee sorry ivi uliwezaje kuishi naye uku ukijua kuwa mimba ni ya mwingine najua utasema mapenzi au ni upoyoyo nakushauri jifunzee kutumia akili zaidi kwenye mahusiano usiache hisia na Moyo wako ukuongozee wanawake ndyo wanaotumia hisia
 
Manina wallahiiii ☹️☹️☹️

13DA8D54-5E0E-4DDA-958A-012457417F5D.jpeg
 
Jilaumu wewe wala mwanamke Hana makosa uliamua kubeba dhambi ya mtu sasa inakutafuna mwenyewe Kwa ushauri jitibu jeraha ulilolipata na kuanza maisha mapya.

Nikuulizee sorry ivi uliwezaje kuishi naye uku ukijua kuwa mimba ni ya mwingine najua utasema mapenzi au ni upoyoyo nakushauri jifunzee kutumia akili zaidi kwenye mahusiano usiache hisia na Moyo wako ukuongozee wanawake ndyo wanaotumia hisia
Nimekuelewa mkuu,Ila mhusika sio mimi
 
Hakuna kitu kinatesa kama mtu akukosee lakini usilalamike wala kuonyesha chuki.
Onyesha kuwa hujaumia na uko sawa.
Muonyeshe upendo lkn kidogokidogo anza kujiondoa katika maisha yake.

Hii kitu itamuumiza hakuna mfano.
Nakubaliana na wewe 100%
 
Back
Top Bottom