Uchaguzi 2020 ACT Wazalendo: Tume ya Uchaguzi iweke hadharani majina ya Wagombea wetu waliokata rufaa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
1599648212865.png

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) IWEKE HADHARANI MAJINA YA WAGOMBEA WETU WALIOKATA RUFAA

Chama cha ACT-Wazalendo kinaitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iweke hadharani orodha ya majina ya wagombea wetu wote wa Ubunge na udiwani ambao walikata rufaa kwake.

Hitaji hilo linatokana na taarifa ya NEC kwa umma iliyotolewa jana Septemba 8, 2020.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera Charles ilisema kwamba, Tume hiyo imekubali rufaa 15 za wagombea Ubunge na kuwarejesha katika orodha ya wagombea na imekataa rufaa 15 za wagombea ambao hawakuteuliwa na pia imekataa rufaa 25 za kupinga walioteuliwa.

ACT-Wazalendo tunasema taarifa hiyo ya NEC haijitoshelezi, ina walakini na upungufu mkubwa kwa sababu haikuweka bayana majina na hata majimbo ambayo rufaa hizo tayari zimezifanyiwa kazi.

Huu ni muda muafaka kwa NEC kufanyakazi kwa weledi na uwazi mkubwa kwa kuyaweka hadharani majina yote ya wagombea waliokata rufaa, sambamba na majimbo husika ili yajulikane mapema na chama kiweze kuendelee na shughuli zake za kampeni kama tulivyopanga.

Aidha kuendelea kukaa kimya au kutokutoa taarifa zilizojitosheleza na kwa wakati kunaonyesha kuna kila dalili kwamba NEC ina nia ovu na mahsusi ya kukibeba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa gharama ya ACT -Wazalendo.

Kwakuwa uchaguzi ni mchakato wa haki, demokrasia na utawala bora, ni kazi ya NEC sasa kuonyesha kwa vitendo kwamba wanalinda haki hiyo kwa kuendesha mchakato wa uchaguzi ulio wazi, huru na haki bila upendeleo.
1599649076134.png

1599649085847.png
 
Taarifa anapelekewa aliyekata rufaa na aliyekatiwa rufaa kwa mujibu wa katiba!
Utakuwa na uhakika gani na idadi ya waliorudishwa bwashee

Isije ikawa 15 kumbe karudishwa meya jacobo mwenye media coverage kubwa

Au wakarudishwa NLD, UPDP na TLP wapinzani halisi wakawa wametemwa

Uwazi ni jambo la msingi tumwenzi marehem Ben kwa vitendo
 
Ni jukumu lao kama chama, hasa katibu mkuu wa ACT Wazalendo kulifanyia logistic,tume ina kazi nyingi za kufanya .
Wanatafuta loophole ya kufanyia siasa?
 
Vyama vya upinzani mkilegeza tu ktk hili la kukatwa kihuni kwa wagombea basi mjue hata matokeo ya kihuni yatawahusu. Huu ni mtihani ambao mnapaswa kuufaulu kwa kuukataa uhuni.
 
Taarifa anapelekewa aliyekata rufaa na aliyekatiwa rufaa kwa mujibu wa katiba!
Hujui lolote wewe. Msiwe mnapenda kuchangia hata vitu msivyovijua.

Wagombea waliokata rufaa na kushindwa huwa wanarudishwa kwa tangazo la Tume. Na mara baada ya tangazo la Tume, mgombea huwa yupo huru kuendelea na kampeni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taarifa anapelekewa aliyekata rufaa na aliyekatiwa rufaa kwa mujibu wa katiba!

Chama kilichodhamini kina haki ya kupata hiyo taarifa. Hiyo dhamana ni pulic office sio suala binafsi taarifa hizo ziwekwe wazi. Huuni mwendelezo wa kujenga kutokuaminiana bila sababu za msingi.
 
NEC wanatamani sana kuwarudisha wagombea Lakini upo mzizi katili uliojichimbia chini zaidi.

Hizi ni Dalili za kutokuwa na uchaguzi wa huru Haki na Amani.

Wanaturudisha kwenye uchaguzi wa selikali za Mitaa.

Hata sisi CCM hatupendi haya.
 
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) IWEKE HADHARANI MAJINA YA WAGOMBEA WETU WALIOKATA RUFAA

Chama cha ACT-Wazalendo kinaitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iweke hadharani orodha ya majina ya wagombea wetu wote wa Ubunge na udiwani ambao walikata rufaa kwake.

Hitaji hilo linatokana na taarifa ya NEC kwa umma iliyotolewa jana Septemba 8, 2020.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera Charles ilisema kwamba, Tume hiyo imekubali rufaa 15 za wagombea Ubunge na kuwarejesha katika orodha ya wagombea na imekataa rufaa 15 za wagombea ambao hawakuteuliwa na pia imekataa rufaa 25 za kupinga walioteuliwa.

ACT-Wazalendo tunasema taarifa hiyo ya NEC haijitoshelezi, ina walakini na upungufu mkubwa kwa sababu haikuweka bayana majina na hata majimbo ambayo rufaa hizo tayari zimezifanyiwa kazi.

Huu ni muda muafaka kwa NEC kufanyakazi kwa weledi na uwazi mkubwa kwa kuyaweka hadharani majina yote ya wagombea waliokata rufaa, sambamba na majimbo husika ili yajulikane mapema na chama kiweze kuendelee na shughuli zake za kampeni kama tulivyopanga.

Aidha kuendelea kukaa kimya au kutokutoa taarifa zilizojitosheleza na kwa wakati kunaonyesha kuna kila dalili kwamba NEC ina nia ovu na mahsusi ya kukibeba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa gharama ya ACT -Wazalendo.

Kwakuwa uchaguzi ni mchakato wa haki, demokrasia na utawala bora, ni kazi ya NEC sasa kuonyesha kwa vitendo kwamba wanalinda haki hiyo kwa kuendesha mchakato wa uchaguzi ulio wazi, huru na haki bila upendeleo.
View attachment 1564187
View attachment 1564188
Hii tume ina matatizo. Inaegemea sana upande wawajiri wao CCM. Pia wote ni makada wa CCM. Hapa hakuna uchaguzi huru na haki. Ni uchafuzi tu.
 
Utakuwa na uhakika gani na idadi ya waliorudishwa bwashee

Isije ikawa 15 kumbe karudishwa meya jacobo mwenye media coverage kubwa

Au wakarudishwa NLD, UPDP na TLP wapinzani halisi wakawa wametemwa

Uwazi ni jambo la msingi tumwenzi marehem Ben kwa vitendo
Mbona hata huyo Ben Mkapa hakuwa muwazi ndio maana mikataba ya ubinafshaji haikuwa wazi.
 
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) IWEKE HADHARANI MAJINA YA WAGOMBEA WETU WALIOKATA RUFAA

Chama cha ACT-Wazalendo kinaitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iweke hadharani orodha ya majina ya wagombea wetu wote wa Ubunge na udiwani ambao walikata rufaa kwake.

Hitaji hilo linatokana na taarifa ya NEC kwa umma iliyotolewa jana Septemba 8, 2020.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera Charles ilisema kwamba, Tume hiyo imekubali rufaa 15 za wagombea Ubunge na kuwarejesha katika orodha ya wagombea na imekataa rufaa 15 za wagombea ambao hawakuteuliwa na pia imekataa rufaa 25 za kupinga walioteuliwa.

ACT-Wazalendo tunasema taarifa hiyo ya NEC haijitoshelezi, ina walakini na upungufu mkubwa kwa sababu haikuweka bayana majina na hata majimbo ambayo rufaa hizo tayari zimezifanyiwa kazi.

Huu ni muda muafaka kwa NEC kufanyakazi kwa weledi na uwazi mkubwa kwa kuyaweka hadharani majina yote ya wagombea waliokata rufaa, sambamba na majimbo husika ili yajulikane mapema na chama kiweze kuendelee na shughuli zake za kampeni kama tulivyopanga.

Aidha kuendelea kukaa kimya au kutokutoa taarifa zilizojitosheleza na kwa wakati kunaonyesha kuna kila dalili kwamba NEC ina nia ovu na mahsusi ya kukibeba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa gharama ya ACT -Wazalendo.

Kwakuwa uchaguzi ni mchakato wa haki, demokrasia na utawala bora, ni kazi ya NEC sasa kuonyesha kwa vitendo kwamba wanalinda haki hiyo kwa kuendesha mchakato wa uchaguzi ulio wazi, huru na haki bila upendeleo.
View attachment 1564187
View attachment 1564188
Chama kinakosa orodha ya wagombea waliojaza form za kugombea, wanahaha kwa kuitaka tume iwawekee orodha hiyo....
 
Back
Top Bottom