Tume ya Katiba
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,896
- 1,866
Mkuu habari ya mujini wakati anashindwa kujibu maswali ya msingi anayoulizwa na Watanzania? Alikuja hapa jamvini akaanzisha uzi na watu wengi wakauliza maswali mengi ya msingi akajibu baadhi tu na kisha akakikimbia kujibu maswali mengine chungu nzima. Ni kipi kinachomfanya achague maswali yepi ni ya kuyajibu na mengine kuyapotezea? Kama hana majibu si aseme tu sina majibu badala ya kukimbia? Haya maswali yataendelea kuulizwa atayakimbia mpaka lini?
Mkuu wangu hata kujibu hayo machache ni credit, si viongozi wengi wana ujasiri wa kuface hadhira na kujibu maswali yao. Pia kiongozi makini kama ZZK hawezzi kukurupuka kujibu maswali ambayo anahitaji muda kuyatafakari na kutafutia majibu yake, lakini ukumbuke kuwa yapo maswali mengine hayana majibu.
Nakuhimiza ndugu, fuatilia kwa karibu mikutano ya ACT na soma vyema sera na katiba ya ACT kisha fananisha na vyama vingine utagundua kuwa kuna tofauti kubwa sana. Juzi nimeshangaa sana kwa Mbowe kusema hatokubali JK kujiongezea muda wa kuongoza, wakati katika katiba yao ya chama hakuna ukomo wa uongozi...........