PostGE2025 ACT Wazalendo: Mchakato wa uchaguzi uliharibiwa na tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC). Tutakwenda mahakamani

PostGE2025 ACT Wazalendo: Mchakato wa uchaguzi uliharibiwa na tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC). Tutakwenda mahakamani

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Mwizukulu wa Buganda

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2024
Posts
638
Reaction score
1,771
Chama cha ACT Wazalendo kimesema kimejipanga kuchukua hatua za Kisheria kwa kile wanachodai kuwa ni kudai haki ya ushindi walioupata katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

Kauli hiyo imetolewa na Mnadhimu wa Kambi rasmi ya Upinzani katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Profesa Omar Fakih, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Chama hicho eneo la Vuga, mjini Zanzibar.

Amesema katika uchaguzi huo, Chama chao kilipata ushindi kwenye jumla ya Majimbo 32 ya Ubunge, Uwakilishi na Udiwani, lakini wanadai Matokeo hayo yaliporwa, hivyo watafuata taratibu za Kisheria kudai haki yao.

 
Kwani zanzibar wanahusu matokeo ya uchaguzi kupingwa mahakamani
 
Back
Top Bottom