Mbinu wanayotumia X na Instagram ni kuwa na ID nyingi halafu wanajifanya ni Umma.
Ukitaka kusoma hisia za Wananchi kasikilize mikutano ya mtandaoni.
Mbinu multiple IDs wameitumia JF pia, wamejaza watu wakiandika habari moja mara 10 ili kujaza nafasi.
Mbinu hiyo wanaifanya kwa kuifungia JF technically, ili wao waendelee nayo Umma ukiwa hauna access
Wasichokitambua ni hisia za Wananchi. Walitumia mbinu za kuwaweka mahabusu viongozi wa CHADEMAikawa ni baraka kwao maana wangekuwa nje OCT29 sijui ingekuwaje. Je, walizuia kilichotokea?
ACT hawana msimamo tangu Zitto alipoambatana na Kamati ya Mkandala kutengeneza marejeo feki ya Katiba.
Z'bar huwasikii wanagaiwa keki! si Mansour, si OMO wala Jusa. Wametulia maana waliambiwa ''ni wakati wetu''. Maalimu huko aliko sijui anajisikia.
Maalim aliasisi 'HAKI SAWA'' lakini ACT ya leo si ile ya Maalimu. Mchinjita yupo Bungeni , Dorothy anasema hataki maridhiano ni vurugu tupu. Hawa ACT si wa kuwasikiliza hata nukta
Wasubiri nusu mkate na OMO keshapeleka majina!
JokaKuu