ACT ni mbadala wa CHADEMA au CCM?

CCJ ilikufa hivihivi kwa dhambi ya kuwakana waanzilishi,na huu ndo unafiki wenyewe,sasa hapo transparency iko wapi?

kwa hiyo unang'ang'ania zito awepo? nimeshakuambia zito hayupo act mbona mgumu sana kuelewa?
 
Kwa siasa za Tanzania chama chochote kinachotaka kuingia madarakani hasa kwa siku za karibuni nadhani mpinzani wake mkuu ni CCM na wala sio chama kingine chochote,je ACT imewekeza nguvu nyingi kushindana na CDM au CCM? kwanini hata sehemu moja ACT haioni kama CCM ni tishio?
 
unataka majina ili uyafanyaje mkuu? au mnataka muanze propaganda zenu za udini na ukanda

kwa hiyo majina mnapeana kiundugu eeeh watanzania wengine mbona mnatubagua hivi kwanini jamani,Tutaanzaje propaganga za ukanda kama chama kina Sura ya kitaifa? kama kipo kikanda na kikabila tutasema tu sasa we unataka tukae kimya wakati kipo kikanda,ndio maana mnaambiwa hicho ni cha coward traitors
 
kwa hiyo majina mnapeana kiundugu eeeh watanzania wengine mbona mnatubagua hivi kwanini jamani,Tutaanzaje propaganga za ukanda kama chama kina Sura ya kitaifa? kama kipo kikanda na kikabila tutasema tu sasa we unataka tukae kimya wakati kipo kikanda,ndio maana mnaambiwa hicho ni cha coward traitors

nimekuambia viongozi wake ni wasomi makini unataka kujua majina yao ya nini mkuu?
 
Dah! nani amezungumzia suala la kuanzisha uzi? nimekuambia Babu anakijua chama cha ACT usijitoe ufahamu kamanda.

Uwe na uelewa unasema nikamuulize Dr Slaa wakati tupo hapa tunajadili.Mi hiyo habari ya Slaa na kalenga inanihusu nini,mimi kama mtanzania mwenye haki ya kujiunga chama chochte naweza kumuuliza yeyote na hapa nimemuuliza mleta uzi kwa sababu kwa mazingira ya hapa ndio anayejua kila kitu sasa kwa nini nianze kuzunguka wakati mtu wa kumuuliza yupo.
 
Sasa ndio useme ni cha nani, Nani kiongozi wake sio kuongozwa na hisia coz ccj kilipo anza mashabiki km wewe walisema cha Sitta na ndio mwenyekiti wake wkt waliokianzisha wengine kwa majina mengine..Hata wewe waweza anzisha chama ukakisajili ukitegemea baadae umfuate mtu fulani mwenye nguvu ili akibebe chama km mwenyekiti.Sasa km wewe unaushahidi ni cha udini na ukigoma tujuze huyo kiongozi wake mdini na mkabila sio kuongozwa kwa hisia na utupe na source.

CCJ ilianzishwa na majina ya waanzilishi yalikuwa kwenye makabrasha kwa msajiri wa vyama vya siasa walisema ni chama cha sita walikuwa na sababu zao japo hawakuwa na ushahidi, sasa hujanijibu swali langu ktk uanzishwaji wa chama cha siasa ili chama kipate usajiri ni criteria gani zinatakiwa ziwe-met.......maana ulisema chama hakina mwanzilishi(maana ni illegally registered-some thing like you have raised PO) usikimbie hoja yangu swala la mimi ku-prove beyond reasonable doubt juu ya mwanzishaji na udini na ukanda wake vitakuja baada ya wewe kuupa mjadala legality-kuwa ni chama halali ama si halali, maana sitaki kuthibisha allegations zangu wakati umesha-raise question of doubt kwenye uhalali wa chama, we should ascertain the PO raised before determining the merit of the case itself.
 
Umeona mkuu,mimi hata bendera yao sijaiona lkn nikiishaona manunguniko yametangulia huwa sijihangaishi kuuliza,
najua nyuma kuna nyota.

Umeshazoea kulishwa matango pori hata bendera ya USA ina nyota, hayo malalamiko yanatolewa na vilaza wa Chadema.
 
kwa hiyo unang'ang'ania zito awepo? nimeshakuambia zito hayupo act mbona mgumu sana kuelewa?
Mimi nimekupa taarifa,kuhusu ccj ulitakiwa kuipokea au kuikataa,
mimi nawatakia kila la kheri,ninchowahasa msijilinganishe na cdm katu,na kwa sasa hakuna mbadala wa CDM,Kama unabisha niambie ni chama gani kimethubutu kuwawajibisha viongozi wake wakuu ambao wanaonekana kuvuruga vyama vyao kikaweza mbali na cdm,ccm ilijaribu ikashindwa,cha kwenu mnachoita mbadala bado kipo kwenye hatua za awali zinazoitwa kanyaga twende(MENDE,PAPASI ,MCHWA) Ndani hamjajuana mtajiitaje mbadala hata miezi 6 hamjatimiza?
Nakushauri ktk hatua hizi za mwanzo hata wewe mwenyewe usijiamini unaweza kuwa msaliti wa chama kesho.
 
Kwa siasa za Tanzania chama chochote kinachotaka kuingia madarakani hasa kwa siku za karibuni nadhani mpinzani wake mkuu ni CCM na wala sio chama kingine chochote,je ACT imewekeza nguvu nyingi kushindana na CDM au CCM? kwanini hata sehemu moja ACT haioni kama CCM ni tishio?

Ningekuwa na chuo kikuuu changu ningekutunuku PH ya heshima kwa kutoa hoja ya mashiko amabyo nami nimekuwa nikiwauliza sana hao nyang'au
 
Umeshazoea kulishwa matango pori hata bendera ya USA ina nyota, hayo malalamiko yanatolewa na vilaza wa Chadema.

mi nawashangaa sana hawa vilaza . bendera ya USA ina nyota. kwa hiyo USA ni nchi ya kiislamu?
 
wakuu,
baada ya chama kikuu cha upinzani nchini chadema kupoteza uelekeo na kusambaratika, hatimae chama mbadala wa chadema kimepatikana.
Chama hiki makini na mkombozi wa watanzania ni act.
Act ni chama makini sana na viongozi wake ni wasomi hawajakimbia shule wala kupata division zero kwenye mitihani yao,
sera kuu ya act ni maendeleo kwa vijana wote wa tanzania.
Act ni chama cha watanzania wote hakina ubaguzi wa kidini, kikabila wala kikanda kama vyama vingine
naomba serikali iboreshe daftari la kudumu la mpiga kura haraka ili vijana wajiunge na chama chao makini wanachokipenda cha act.
Naomba kuwakilisha hoja.
lumumba mbona mnahangaika sana mlishapoteza kubali maumivu 2015, hakuna cha ccm wala mkewe act, 2015 ni kichapo tu
 
kwa hiyo majina mnapeana kiundugu eeeh watanzania wengine mbona mnatubagua hivi kwanini jamani,Tutaanzaje propaganga za ukanda kama chama kina Sura ya kitaifa? kama kipo kikanda na kikabila tutasema tu sasa we unataka tukae kimya wakati kipo kikanda,ndio maana mnaambiwa hicho ni cha coward traitors

Mbona kuna vyama kama Chausta,DP,SAU,NRA hamuvizungumzi wala hamutaki kujua viongozi wake? endeleeni kukipa majina mabaya haisaidii mnachofanya ni sawa na kumpiga chura teke.
 
Muulize Babu Slaa anakijua alikipigia debe alipokuwa anamtambulisha mgombea wenu Kalenga.

mkuu. dr slaa anakijua vizuri sana hiki chama na anakiogopa sana. hawa vilaza wake waende wakamuulize babu yao
 
Back
Top Bottom