CPU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 3,863
- 686
Swala sio kuona kawaida . . . . . swala ni kupima uzito wa wanachokisusia na kujua je ni kwa faida ya nani????
Baada ya hapo ndo mtu unajua utakapojisikia vibaya ni kwasababu umesababisha wakususie au kwasababu hawataki kukuunga mkono?? Vyovyote vile ndugu/jamaa/na marafiki wanatakiwa waondoe ubinafsi kwenye maamuzi yao. Hata kama kuna kitu hakikuwafurahisha kama hakimuumizi yeyote wangekuwepo then waondoke....kwani inawagharimu nini?
Hiyo bluu ni kauli hatari sana. Inaashiria kwamba lisemwalo na ndugu/jamaa/rafiki n.k. either liwe kweli au lisiwe kweli YOU DONT CARE!!! THEY MUST STICK TO WHAT YOU WANT, LIWE BAYA AU ZURI HALIWAHUSU!!! Ni aina fulani ya kuwafukuza ndugu zako. Tena ukiunganisha na hiyo red ndo inakamilika kabisa.
Mfano, umeambiwa mume/mke unaetaka kufunga nae ndoa anavuta bangi, anasafirisha mihadarati, ni kiongozi wa genge la ujambazi, ana wapenzi wengi n.k. then ukaambiwa ufanyie kazi hizi habari kabla hujafunga nae ndoa, wewe unaita ubinafsi.
Na kuonyesha jeuri unaitisha harusi, huku ukitaka ndugu wahudhurie???!!
Hapo kwenye black umesema KAMA KUNA KITU HAKIKUWAFURAHISHA hao ndugu (automatically kinaudhi) then unasema HAKIMUUMIZI YEYOTE??? How come is this possible???