Mbona sijaona Kinana mahali popote kwenye hiyo site? Hebu weka specific link.
Leokweli,
Sasa nimemuona Kinana pamoja na MP. wa Masasi Bw. Marope. Kama na Kinana naye yumo kwenye hizi biashara za kuuza nchi, basi tumekwisha.
Hivi ni kwa nini hizi kampuni zinazosema zina-invest TZ zote zinaweka watu wenye nguvu sana ndani ya CCM kuwa ni maDirector wao? Wana nia gani wanapofanya hivyo? Hivi huko ndio kuajiri wazawa au ni kununua influence?
mhhh.. ama kweli bado safari ndefu! Wasi wasi ni kwamba at the end watz tutakuja kufa mapema kutokana na stress tunazo zipata kila siku, kwani kila kukicha gazeti, vyombo vya habri, mitandao unakutana na habari za kutia machungu tuuuu.. hakuna habari njema kwa watz hata kidogo!
Kweli Kinana ndo Chairperson, nimetemebelea hiyo link na nimemwona, Mrope naye yumo! Wa-Tz huu umaskini wetu hautakoma kwa kuwa na Watawala wa aina hiyo, hata tupewe bajeti yote ya nchi ya Marekani.
Tujiulize, hivi Kinana ana pesa gani za kumfanya awe Mwenyekiti wa KAmpuni hii kama si UKUWADI tu? Hii inanikumbusha title ya Kitabu cha Marehemu Prof Chachage "MAKUWADI WA SOKO HURIA" Huu ndo ukweli, Watawala wetu wamgeuka Makuwadi wakiikuwadia TZ kwa "Wawekezaji" kwa gharama ya nchi na watu wetu. Na ni hawahawa Wawekezaji ndo watatoa mapesa ya kuisadia CCM ibaki madarakani 2010 ikiwa kama tutafanikiwa kubana EPA zote.
Watanzania tuamke.
Huwezi ukaingia UBIA na makampuni ya nje ya kinyonyaji na wakati wewe ni kiongozi halafu udai eti unaruhusiwa!
Hata hiyo mikataba waliyopata na kupewa pesa na TANESCO ZA KUCHIMBA MAFUTA AMBAYO HATA HAYAMSAIDII MTANZANIA!
Ni Violation of WORK ETHICS NA HAWASATAHILI KABISA kuwa na share kwenye makampuni ambayo yameununua UHAI WA MTANZANIA KWA BEI CHEE KWA KUPITIA VIONGOZI MAFISADI WENYE KUJALI MASLAHI YAO ZAIDI.
Hivyo viongozi hao wote wana la kujibu na MIKATABA YOTE IVUNJWE KWANI HAIMSHIRIKISHIA MWANANCHI WALA HATA MKUU WA NCHI ALIYEKO SASA.
Mkuu kwani TANESCO wanajishughulisha na kuchimba mafuta? au ulitaka kuhamia kwa TPDC japo hiyo isingekuwa subject of our discussion.Kuhusu kutomsaidia mtanzania ni kigezo gani unachotumia kupima kama mkataba umemsadia au haujamsaidia mtanzania?
1. Mhh Hili La Kinana Kuwa Mwenyekiti Wa Board Ya Artumas Sidhani Kama Ni Issue Sana Unless Kama Kuna Kitu Kingine Kinachoonyesha Artumas Kupata Upendeleo Usiostahili Kwavile Tu Kinana Ni Mwenyekiti Wa Board.ikumbukwe Kwamba Pius Msekwa Alikuwa Mwenyekiti Wa Board Ya Vodacom Akiwa Bado Ni Spika Na Hakuna Lolote Ambalo Vodacom Walifaidika Directly Kwakuwa Na Spika Kama Mwenyekiti.
2.kama Ilivyo Kwa Ajira Zozote Ni Haki Ya Raia Yoyote Ambaye Ana Uwezo Ikiwa Ataombwa Kukubali Au Kukataa Kuwa Mkurugenzi Na Hivyo Hata Kuwa Mwenyekiti Wa Kampuni Yoyote Ile.hivyo Ni Haki Ya Kiraia Kwa Kinana Kuwa Mkurugenzi Katika Kampuni Yoyote Ile Kama Ilivyohaki Kwa Mtanzania Yoyote Yule Kuajiriwa Katika Artumas.
3.katika Mikataba Yote Ambayo Tanesco Imeingia Na Makampuni Yanayozalisha Umeme Hakuna Mkataba Ambao Pengine Una Nafuu Zaidi Kama Wa Artumas.katika Mkataba Wa Artumas Hakuna Capacity Charge Na Pia Rate Wanayocharge Kwa Umeme Wao Ni Nafuu Zaidi Pengine Kuliko Rate Zinazochajiwa Na Aggreko,iptl,songas Na Dowans/richmond.
4.katika Gesi Inayozalishwa Na Artumas Kwenye Maeneo Yote Ya Mnazi Bay Na Maeneo Ya Jirani Almost 98% Ni Gesi Na 2% Tu Ndiyo Liquid In The Form Ya Maji Na Mafuta Ya Diesel.kwahiyo Si Sahihi Kwamba Unaweza Kufanya Commercial Drilling Ya Mafuta Pale.
Tafadhali Sina Details Za Kipengere Kwa Kipengere Cha Mkataba Wa Artumas Na Tanesco Lkn Kwa Kifupi Hiyo Ndiyo Habari Yenyewe.
jibu Zuri, Ninaona Kila Kampuni Inamwakilishi Wake Jamboforums Siku Hizi, Wewe Bwana Ndiye Legal Officer Wa Artmas?
its good to have locals in the big investment deals but the questions remain valid, why only politicians? If any one is there for intrest of locals he supposed to call for share and list his company in stock exchange so that majority of Tanzanian can have a chance to take a stake,,,but they go limited so they can benefit themselve.
Looking at artumus is a listed icompany in oslo stock exchange, but is not that financially high, which I believe the same company if was listed in Dar stock Exchange would have given a chance for all Tanzanian to participate and get a stake.
This is the same for Mining, Angloashanti is listed in Ghana and south africa why not Tanzania, we need these chances unless the problem will never end.
Is just a matter of a clear prequest to investors and having a risk free sound polices
Watz ndo kwanza tunaanza kuamka kutoka usingizi mzito!
Talking of listed companies..hiyo lugha unaijua wewe na wachache wenye interest ya kujua...
Tatizo kubwa kwetu watz...we never bother to seek for info and knowledge so that we can take advantage of opportunities...
Hao opportunists - wao angalu they get to know of the opportunities by virtue of their positions..na mara nyingi wanakuwa approached na " kuombwa" wachukue shares..in return watoe protection na kufungua milango!
Kazi tunayo!
IPOs kibao zilikuwepo...watz bado tulipigwa bao... maana hatujui maana ya ku participate na faida zake. Hata hapa kwenye JF sidhani ni watz wengi wenye kujua uzuri wa alternative media kama hii..hata wenye access ya internet utashangaa wanajibidiisha zaidi kutembelea sites za ngono badala ya kutafuta maarifa!
TUTASAIDIKA VIPI?