Abdul Nondo amewapiga "KO" maofisa Uhamiaji

Abdul Nondo amewapiga "KO" maofisa Uhamiaji

Yani kweli huyu Abdul Nondo serikali imempaisha kiasi hiki?? Kweli imekosa kazi ya kufanya
 
Mbona povu linakutoka sana hata wewe unaweza ambiwa peleka vyeti vyako mamlaka husika wana hakibhoyo kisheria.
 
Wiki kadhaa zilizopita niliandika ya kwamba sakata la Abdul Nondo litawavua nguo serikali na jeshi la polisi na hakika inaenda kutimia. Leo mwandishi mzoefu Luqman Maloto ameandika machache kuhusu sakata hilo.

Idara ya Uhamiaji ilimtaka Abdul Nondo athibitishe uraia wake kwa kuwasilisha cheti chake cha kuzaliwa, vyeti vya wazazi wake, babu zake na bibi zake. Lilikuwa agizo la hovyo mno.
Hata hivyo, historia ipo na inaishi. Mpaka sasa maofisa hao wameshachapwa KO (Knock Out) na Abdul.

UNONDO WA ABDUL UBABANI

Unondo wa Abdul upande wa baba yake unaelezwa vizuri na Sheikh Khamis Hababi wa Kigoma Ujiji. Sheikh huyu anaijua vizuri familia ya Abdul Nondo.

Sheikh Hababi anasema: "Huyu Kijana (Abdul Nondo) ni Mjukuu Wa mzee Omar Athuman Kagobe. Mzee Kagobe ni mwanajeshi wa zamani (veteran) aliyepigana vita kuu ya pili ya dunia, na ndiye aliyeileta TANU Kigoma. Wakati wa kudai uhuru Nyerere alipofika Kigoma amewahi kufikia kwa mzee Kagobe mara mbili akiwa na Bibi Titi na Sheikh Suleiman Taqadir. Nyerere alikula, kunywa na kusaidiwa nauli na familia ya kina Abdul Nondo.
"Nyumbani kwa Sheikh Kagobe ndipo alipofikia pia Sheikh Abdallah Saleh Al Farsy mara mbili na Sheikh Hassan bin Amir.

"Bibi yake mdogo Nondo ndiye Mama yake Sherry Taki, aliyekuwa mjumbe wa Kamati kuu ya CCM, na mama huyu ndiye aliyemuuliza Nyerere kama atawanyang'anya Wahindi, waarabu na Wazungu majumba na Mashamba, baada ya Uhuru. Nyerere akasema hapana, Utawala wa TANU hautofanya hivyo (ingawa alifanya hivyo baada ya uhuru)."

TAFAKURI

Kwahiyo Uhamiaji wanaposema Nondo si raia wanamaanisha Babu yake (mzee Kagobe) si raia. Mtu aliyepigana vita kuu ya dunia hakua raia? Mtu aliyeintroduce TANU Kigoma (ambayo ndio CCM leo) hakuwa raia. Mtu aliyemlisha na kumlaza Nyerere mara mbili nyumbani kwake hakua raia? Kwamba Nyerere alikuwa akipewa msaada na mtu asiye raia.

Bibi yake mdogo Abdul, mama Sherry Taki nae hakuwa raia, licha ya kuwa mjumbe wa kamati kuu ya CCM? Yani CCM iliruhusu mtu asiye raia kuwa mjumbe wa kamati kuu?
Ni wazi alama ya uraia wa kijana huyu haiwezi kufutika kamwe katika historia. Familia ya kijana huyu imechangia uhuru wa nchi hii, imechangia kuzaliwa kwa taifa hili, imechangia kuzaliwa kwa TANU na hatimaye CCM.

UNONDO WA ABDUL UMAMANI

Unondo wa Abdul upande wa mama yake unaelezwa kinagaubaga na Maalim Razaq Seleman.
Anasema: "Huyu kijana (Nondo) mama yake ni wa ukoo Mzee Haruna Taratibu aliyesisi TANU Dodoma. Mzee Taratibu alisaidia kuanzishwa kwa TANU kipindi ambacho watu wengi hasa wafanyakazi walikua wanaogopa kujihusisha na siasa. Kati ya mwaka 1954 hadi 1958 kilikua kipindi kigumu mno katika harakati za kudai uhuru.
"Mwalimu Nyerere mwenyewe aliwahi kusema 'Hicho kilikuwa kipindi kigumu sana katika historia ya Chama chetu na ni watu wachache sana walikuwa na ujasiri wa kujiunga na chama na kukifanyia kazi.'

"Mmojawapo wa watu waliokua na ujasiri huo ni mzee Taratibu (babu yake mdogo Nondo upande wa mama). Mwaka 1953, Haruna Taratibu, alikuwa na umri wa miaka 23 tu, akifanya kazi Public Works Department (PWD) Dodoma kama fundi mwashi (mason). Pamoja na umri wake mdogo alijaribu kuunda chama cha wafanyakazi kwa kuwahamasisha na kuwakusanya vibarua walioajiriwa katika kazi za ujenzi (wengi wakitokea Kigoma).

"Kwa sababu ya harakati hizo za kutaka kuanzisha chama cha wafanyakazi, Taratibu alionekana na wakoloni kama mtu mkorofi na mzusha vurugu. Hata hivyo Taratibu hakufanikiwa kuanzisha chama hicho na matokeo yake akapewa uhamisho kwenda Singida kama adhabu.
"Mwandishi Nguli wa Historia, Mohamed Said katika kitabu ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)...: (Phoenix Publishers, Nairobi, 2002) ukurasa wa 216, anaeleza kuwa mzee Taratibu alivutiwa sana na harakati za MAUMAU nchini Kenya na alizoea kufuatilia matukio yake katika gazeti lake alilokuwa akilipenda sana, ''Baraza', gazeti la Kiswahili la kila wiki kutoka Kenya.

"Ilikuwa katika Novemba 1954 wakati Taratibu alipokuwa akipekuapekua gazeti hilo ndipo alioposoma habari kuhusu TANU. Taratibu aliuliza pale Singida mjini kama kuna tawi la TANU. Taratibu alifahamishwa kuwepo kwa tawi la TANU pale mjini na katibu wake alikuwa mzee mmoja kwa jina la Mzee Kinyozi.

"Taratibu alikata kadi yake toka kwa huyo mzee na akawa mwanachama wa TANU. Asubuhi iliyofuata Taratibu aliingia ofisini kwake na akaiweka kadi yake ya uanachama wa TANU yenye rangi nyeusi na kijani juu ya meza yake, kila mtu aione. Ofisa Mzungu wa PWD Singida hakuweza kuvumila ufedhuli kama ule, alishauri Taratibu apewe uhamisho kurudi Dodoma alikotoka, kabla hajaeneza sumu yake kwa Waafrika wengine.

"Kwa kifupi mzee Taratibu alijitoa kwa hali na mali kuianzisha TANU bila hofu ya kushughulikiwa na serikali ya kikoloni, licha ya kwamba alikuwa mfanyakazi. Hatimaye alichaguliwa kuwa mjumbe wa sejretarieti na kamati ya siri ya TANU (kwa pendekezo la Oscar Kambona), na baadae alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa TANU kanda ya kati, Rais akiwa Alexander Kanyamara, Katibu Abdu Mohamed Mwamba, Mweka Hazina Omari Suleiman, huku Binti Maftah Karenga, Bakari Yenga, Maalim Khalfan, Idd Waziri na Said Suleiman wakichaguliwa wajumbe."

TAFAKURI

Leo mjukuu wa mzee huyu aliyepigania uhuru anaambiwa si raia.
Mimi kama kawaida yangu nacheka. Ona nacheka tena. Yaani nacheka mno. Nacheka zaidi dogo anavyowagonga KO watu wakubwa wasiotumia 'hikma' na weledi kwenye kazi zao. Eti vyeti vya kuzaliwa vya babu na bibi zako wa upande wa mama na baba. Nina siku nyingi sijasonya!!!!!

MAELEZO YA PICHA

Kutoka kushoto ni Idd Faiz Mafongo, Sheikh Mohamed Ramiya, Mwalimu Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro na Haruna Taratibu wakiwa stesheni ya reli Dodoma mwaka 1955.
Ndimi Luqman MALOTO
Nadhani hiyo tarehe 20 watahairisha, uamiaji hawana akili kabisa. Wanafanya kazi yao kisiasa sana tena bila hata hofu. Utakuta Bashite kawapa hiyo assignment!!
 
Hao uhamiaji watangukia puaaaa

Ova
 
Jambo linapoongonzwa na mtu ambaye hata f4 alizungusha unategemea nini
 
Good nimeipenda kumbe kigoma hatukuwahi kuwa nyumba lakini mbona tunaonekana km wananchi wa ziada ???
 
Kwa huyu mtoto ndio ule msemo "cha kurithi huzidi"huyu anafauata nyayo za babu zake ila yy atawazidi
 
Ujue watanzania akili zetu ndogo sana. Kila sehemu nondo tu. Hivi uhamiaji walisema abdu sio raia? Ninachojua wale ni askari wanahoji lolote wanalojisikia kutaka kujiridhisha nalo. So msifanye kazi za askari nyie.acha wafanye kazi zao kwa uhuru. Akithibitika niraia ama sio raia wewe inakuhusu nn. Badala ya kukaa jf na kupiga majungu why msitumie huo mda kutafuta hela
 
Ujue watanzania akili zetu ndogo sana. Kila sehemu nondo tu. Hivi uhamiaji walisema abdu sio raia? Ninachojua wale ni askari wanahoji lolote wanalojisikia kutaka kujiridhisha nalo. So msifanye kazi za askari nyie.acha wafanye kazi zao kwa uhuru. Akithibitika niraia ama sio raia wewe inakuhusu nn. Badala ya kukaa jf na kupiga majungu why msitumie huo mda kutafuta hela
Wewe unafanya nini huku, muda uliotumia kuandika kama mtafutaji hela si ungekuwa umeshaingiza buku7?
Hatukatai wanatakiwa wahoji lakini wanahoji nini ndio SWALI hapo?
Tuanzie na wewe vyeti vya kuzaliwa baba yako na mama yako kama si WAFANYAKAZI unavyo au wanavyo?
Vyeti vya kuzaliwa bibi na babu yako upande wa mama yako unavyo au wanavyo ?
Vyeti vya kuzaliwa bibi na babu yako mzaa baba unavyo au wanavyo ?
Kama huna kwanini uone watu hawana akili kuwashangaa hao UHAMIAJI kuhoji vitu ambavyo kiuhalisia havina maana?
Nyinyi ndio mnao sababisha viongozi tuliowaweka madarakani kutuonea na kutukandamiza kisa eti ni kiongozi wakati wewe ndio umemuweka pale,tuna haki ya kupinga, kuhoji na kutoa maoni kama mambo yanayoendelea ni ya KIPUUZI kama yalivyo mawazo yako.
 
Wiki kadhaa zilizopita niliandika ya kwamba sakata la Abdul Nondo litawavua nguo serikali na jeshi la polisi na hakika inaenda kutimia. Leo mwandishi mzoefu Luqman Maloto ameandika machache kuhusu sakata hilo.

Idara ya Uhamiaji ilimtaka Abdul Nondo athibitishe uraia wake kwa kuwasilisha cheti chake cha kuzaliwa, vyeti vya wazazi wake, babu zake na bibi zake. Lilikuwa agizo la hovyo mno.
Hata hivyo, historia ipo na inaishi. Mpaka sasa maofisa hao wameshachapwa KO (Knock Out) na Abdul.

UNONDO WA ABDUL UBABANI

Unondo wa Abdul upande wa baba yake unaelezwa vizuri na Sheikh Khamis Hababi wa Kigoma Ujiji. Sheikh huyu anaijua vizuri familia ya Abdul Nondo.

Sheikh Hababi anasema: "Huyu Kijana (Abdul Nondo) ni Mjukuu Wa mzee Omar Athuman Kagobe. Mzee Kagobe ni mwanajeshi wa zamani (veteran) aliyepigana vita kuu ya pili ya dunia, na ndiye aliyeileta TANU Kigoma. Wakati wa kudai uhuru Nyerere alipofika Kigoma amewahi kufikia kwa mzee Kagobe mara mbili akiwa na Bibi Titi na Sheikh Suleiman Taqadir. Nyerere alikula, kunywa na kusaidiwa nauli na familia ya kina Abdul Nondo.
"Nyumbani kwa Sheikh Kagobe ndipo alipofikia pia Sheikh Abdallah Saleh Al Farsy mara mbili na Sheikh Hassan bin Amir.

"Bibi yake mdogo Nondo ndiye Mama yake Sherry Taki, aliyekuwa mjumbe wa Kamati kuu ya CCM, na mama huyu ndiye aliyemuuliza Nyerere kama atawanyang'anya Wahindi, waarabu na Wazungu majumba na Mashamba, baada ya Uhuru. Nyerere akasema hapana, Utawala wa TANU hautofanya hivyo (ingawa alifanya hivyo baada ya uhuru)."

TAFAKURI

Kwahiyo Uhamiaji wanaposema Nondo si raia wanamaanisha Babu yake (mzee Kagobe) si raia. Mtu aliyepigana vita kuu ya dunia hakua raia? Mtu aliyeintroduce TANU Kigoma (ambayo ndio CCM leo) hakuwa raia. Mtu aliyemlisha na kumlaza Nyerere mara mbili nyumbani kwake hakua raia? Kwamba Nyerere alikuwa akipewa msaada na mtu asiye raia.

Bibi yake mdogo Abdul, mama Sherry Taki nae hakuwa raia, licha ya kuwa mjumbe wa kamati kuu ya CCM? Yani CCM iliruhusu mtu asiye raia kuwa mjumbe wa kamati kuu?
Ni wazi alama ya uraia wa kijana huyu haiwezi kufutika kamwe katika historia. Familia ya kijana huyu imechangia uhuru wa nchi hii, imechangia kuzaliwa kwa taifa hili, imechangia kuzaliwa kwa TANU na hatimaye CCM.

UNONDO WA ABDUL UMAMANI

Unondo wa Abdul upande wa mama yake unaelezwa kinagaubaga na Maalim Razaq Seleman.
Anasema: "Huyu kijana (Nondo) mama yake ni wa ukoo Mzee Haruna Taratibu aliyesisi TANU Dodoma. Mzee Taratibu alisaidia kuanzishwa kwa TANU kipindi ambacho watu wengi hasa wafanyakazi walikua wanaogopa kujihusisha na siasa. Kati ya mwaka 1954 hadi 1958 kilikua kipindi kigumu mno katika harakati za kudai uhuru.
"Mwalimu Nyerere mwenyewe aliwahi kusema 'Hicho kilikuwa kipindi kigumu sana katika historia ya Chama chetu na ni watu wachache sana walikuwa na ujasiri wa kujiunga na chama na kukifanyia kazi.'

"Mmojawapo wa watu waliokua na ujasiri huo ni mzee Taratibu (babu yake mdogo Nondo upande wa mama). Mwaka 1953, Haruna Taratibu, alikuwa na umri wa miaka 23 tu, akifanya kazi Public Works Department (PWD) Dodoma kama fundi mwashi (mason). Pamoja na umri wake mdogo alijaribu kuunda chama cha wafanyakazi kwa kuwahamasisha na kuwakusanya vibarua walioajiriwa katika kazi za ujenzi (wengi wakitokea Kigoma).

"Kwa sababu ya harakati hizo za kutaka kuanzisha chama cha wafanyakazi, Taratibu alionekana na wakoloni kama mtu mkorofi na mzusha vurugu. Hata hivyo Taratibu hakufanikiwa kuanzisha chama hicho na matokeo yake akapewa uhamisho kwenda Singida kama adhabu.
"Mwandishi Nguli wa Historia, Mohamed Said katika kitabu ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)...: (Phoenix Publishers, Nairobi, 2002) ukurasa wa 216, anaeleza kuwa mzee Taratibu alivutiwa sana na harakati za MAUMAU nchini Kenya na alizoea kufuatilia matukio yake katika gazeti lake alilokuwa akilipenda sana, ''Baraza', gazeti la Kiswahili la kila wiki kutoka Kenya.

"Ilikuwa katika Novemba 1954 wakati Taratibu alipokuwa akipekuapekua gazeti hilo ndipo alioposoma habari kuhusu TANU. Taratibu aliuliza pale Singida mjini kama kuna tawi la TANU. Taratibu alifahamishwa kuwepo kwa tawi la TANU pale mjini na katibu wake alikuwa mzee mmoja kwa jina la Mzee Kinyozi.

"Taratibu alikata kadi yake toka kwa huyo mzee na akawa mwanachama wa TANU. Asubuhi iliyofuata Taratibu aliingia ofisini kwake na akaiweka kadi yake ya uanachama wa TANU yenye rangi nyeusi na kijani juu ya meza yake, kila mtu aione. Ofisa Mzungu wa PWD Singida hakuweza kuvumila ufedhuli kama ule, alishauri Taratibu apewe uhamisho kurudi Dodoma alikotoka, kabla hajaeneza sumu yake kwa Waafrika wengine.

"Kwa kifupi mzee Taratibu alijitoa kwa hali na mali kuianzisha TANU bila hofu ya kushughulikiwa na serikali ya kikoloni, licha ya kwamba alikuwa mfanyakazi. Hatimaye alichaguliwa kuwa mjumbe wa sejretarieti na kamati ya siri ya TANU (kwa pendekezo la Oscar Kambona), na baadae alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa TANU kanda ya kati, Rais akiwa Alexander Kanyamara, Katibu Abdu Mohamed Mwamba, Mweka Hazina Omari Suleiman, huku Binti Maftah Karenga, Bakari Yenga, Maalim Khalfan, Idd Waziri na Said Suleiman wakichaguliwa wajumbe."

TAFAKURI

Leo mjukuu wa mzee huyu aliyepigania uhuru anaambiwa si raia.
Mimi kama kawaida yangu nacheka. Ona nacheka tena. Yaani nacheka mno. Nacheka zaidi dogo anavyowagonga KO watu wakubwa wasiotumia 'hikma' na weledi kwenye kazi zao. Eti vyeti vya kuzaliwa vya babu na bibi zako wa upande wa mama na baba. Nina siku nyingi sijasonya!!!!!

MAELEZO YA PICHA

Kutoka kushoto ni Idd Faiz Mafongo, Sheikh Mohamed Ramiya, Mwalimu Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro na Haruna Taratibu wakiwa stesheni ya reli Dodoma mwaka 1955.
Ndimi Luqman MALOTO
Wewe ndo Japhety wa fesibuku?

Hongera kwa harakati za uandishi.
 
Ila inawezekana mimi uelewa wangu ni mdogo, Je kuwa raia wa nchi fulani ni lazima babu na bibi yako wawe raia wa nchi hiyo??? mfano nikizaliwa tu na baba mtanzania je sipaswi kuwa mtanzania????

Tu-assume tu kuwa hata kama mababu wa Nondo hawakuwa watanzania je inahusiana nn na Nondo mwenyewe???
Ukishaanza kutumika hizo logic zote unasahau, hapa inabidi wamtumie dogo ujumbe kwamba asije tena
 
Ujue watanzania akili zetu ndogo sana. Kila sehemu nondo tu. Hivi uhamiaji walisema abdu sio raia? Ninachojua wale ni askari wanahoji lolote wanalojisikia kutaka kujiridhisha nalo. So msifanye kazi za askari nyie.acha wafanye kazi zao kwa uhuru. Akithibitika niraia ama sio raia wewe inakuhusu nn. Badala ya kukaa jf na kupiga majungu why msitumie huo mda kutafuta hela
Uko uhamiaji?
 
Sidhani kama kunaudhalilishaji ila sasa tunajuwa ya sirini yakuwa kijana Nondo anatoka ktk moja familia ya waasisi wa Taifa letu hivyo nikumrudisha kundini na siku moja atatoka. Hakuna wakulaumu
 
Hii nchi ya kwetu sote hakuna mwenye hatimiliki, haya mambo yana mwisho na mwisho wake umekaribia.
 
Binafsi hiyo historia ya kulishwa Nyerere haijanivutia maana haijibu hoja ya vyeti vya hao mababu. Ninachokiona na ambacho Abdul Nondo kuwakaba nacho ni hao uhamiaji kila mmoja alete mezani vyeti vya bibi na babu zao ndipo na Abdul nae apeleke. Bila wao kuleta kama mbwai na iwe mbwai hapeleki vyeti hapo
 
Wewe unafanya nini huku, muda uliotumia kuandika kama mtafutaji hela si ungekuwa umeshaingiza buku7?
Hatukatai wanatakiwa wahoji lakini wanahoji nini ndio SWALI hapo?
Tuanzie na wewe vyeti vya kuzaliwa baba yako na mama yako kama si WAFANYAKAZI unavyo au wanavyo?
Vyeti vya kuzaliwa bibi na babu yako upande wa mama yako unavyo au wanavyo ?
Vyeti vya kuzaliwa bibi na babu yako mzaa baba unavyo au wanavyo ?
Kama huna kwanini uone watu hawana akili kuwashangaa hao UHAMIAJI kuhoji vitu ambavyo kiuhalisia havina maana?
Nyinyi ndio mnao sababisha viongozi tuliowaweka madarakani kutuonea na kutukandamiza kisa eti ni kiongozi wakati wewe ndio umemuweka pale,tuna haki ya kupinga, kuhoji na kutoa maoni kama mambo yanayoendelea ni ya KIPUUZI kama yalivyo mawazo yako.
Safi sana jibu hili linamfaa mtu mwenye akili za panzi kama huyu
 
Back
Top Bottom