Abdul Nondo amewapiga "KO" maofisa Uhamiaji

Abdul Nondo amewapiga "KO" maofisa Uhamiaji

Wiki kadhaa zilizopita niliandika ya kwamba sakata la Abdul Nondo litawavua nguo serikali na jeshi la polisi na hakika inaenda kutimia. Leo mwandishi mzoefu Luqman Maloto ameandika machache kuhusu sakata hilo.

Idara ya Uhamiaji ilimtaka Abdul Nondo athibitishe uraia wake kwa kuwasilisha cheti chake cha kuzaliwa, vyeti vya wazazi wake, babu zake na bibi zake. Lilikuwa agizo la hovyo mno.
Hata hivyo, historia ipo na inaishi. Mpaka sasa maofisa hao wameshachapwa KO (Knock Out) na Abdul.

UNONDO WA ABDUL UBABANI

Unondo wa Abdul upande wa baba yake unaelezwa vizuri na Sheikh Khamis Hababi wa Kigoma Ujiji. Sheikh huyu anaijua vizuri familia ya Abdul Nondo.

Sheikh Hababi anasema: "Huyu Kijana (Abdul Nondo) ni Mjukuu Wa mzee Omar Athuman Kagobe. Mzee Kagobe ni mwanajeshi wa zamani (veteran) aliyepigana vita kuu ya pili ya dunia, na ndiye aliyeileta TANU Kigoma. Wakati wa kudai uhuru Nyerere alipofika Kigoma amewahi kufikia kwa mzee Kagobe mara mbili akiwa na Bibi Titi na Sheikh Suleiman Taqadir. Nyerere alikula, kunywa na kusaidiwa nauli na familia ya kina Abdul Nondo.
"Nyumbani kwa Sheikh Kagobe ndipo alipofikia pia Sheikh Abdallah Saleh Al Farsy mara mbili na Sheikh Hassan bin Amir.

"Bibi yake mdogo Nondo ndiye Mama yake Sherry Taki, aliyekuwa mjumbe wa Kamati kuu ya CCM, na mama huyu ndiye aliyemuuliza Nyerere kama atawanyang'anya Wahindi, waarabu na Wazungu majumba na Mashamba, baada ya Uhuru. Nyerere akasema hapana, Utawala wa TANU hautofanya hivyo (ingawa alifanya hivyo baada ya uhuru)."

TAFAKURI

Kwahiyo Uhamiaji wanaposema Nondo si raia wanamaanisha Babu yake (mzee Kagobe) si raia. Mtu aliyepigana vita kuu ya dunia hakua raia? Mtu aliyeintroduce TANU Kigoma (ambayo ndio CCM leo) hakuwa raia. Mtu aliyemlisha na kumlaza Nyerere mara mbili nyumbani kwake hakua raia? Kwamba Nyerere alikuwa akipewa msaada na mtu asiye raia.

Bibi yake mdogo Abdul, mama Sherry Taki nae hakuwa raia, licha ya kuwa mjumbe wa kamati kuu ya CCM? Yani CCM iliruhusu mtu asiye raia kuwa mjumbe wa kamati kuu?
Ni wazi alama ya uraia wa kijana huyu haiwezi kufutika kamwe katika historia. Familia ya kijana huyu imechangia uhuru wa nchi hii, imechangia kuzaliwa kwa taifa hili, imechangia kuzaliwa kwa TANU na hatimaye CCM.

UNONDO WA ABDUL UMAMANI

Unondo wa Abdul upande wa mama yake unaelezwa kinagaubaga na Maalim Razaq Seleman.
Anasema: "Huyu kijana (Nondo) mama yake ni wa ukoo Mzee Haruna Taratibu aliyesisi TANU Dodoma. Mzee Taratibu alisaidia kuanzishwa kwa TANU kipindi ambacho watu wengi hasa wafanyakazi walikua wanaogopa kujihusisha na siasa. Kati ya mwaka 1954 hadi 1958 kilikua kipindi kigumu mno katika harakati za kudai uhuru.
"Mwalimu Nyerere mwenyewe aliwahi kusema 'Hicho kilikuwa kipindi kigumu sana katika historia ya Chama chetu na ni watu wachache sana walikuwa na ujasiri wa kujiunga na chama na kukifanyia kazi.'

"Mmojawapo wa watu waliokua na ujasiri huo ni mzee Taratibu (babu yake mdogo Nondo upande wa mama). Mwaka 1953, Haruna Taratibu, alikuwa na umri wa miaka 23 tu, akifanya kazi Public Works Department (PWD) Dodoma kama fundi mwashi (mason). Pamoja na umri wake mdogo alijaribu kuunda chama cha wafanyakazi kwa kuwahamasisha na kuwakusanya vibarua walioajiriwa katika kazi za ujenzi (wengi wakitokea Kigoma).

"Kwa sababu ya harakati hizo za kutaka kuanzisha chama cha wafanyakazi, Taratibu alionekana na wakoloni kama mtu mkorofi na mzusha vurugu. Hata hivyo Taratibu hakufanikiwa kuanzisha chama hicho na matokeo yake akapewa uhamisho kwenda Singida kama adhabu.
"Mwandishi Nguli wa Historia, Mohamed Said katika kitabu ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)...: (Phoenix Publishers, Nairobi, 2002) ukurasa wa 216, anaeleza kuwa mzee Taratibu alivutiwa sana na harakati za MAUMAU nchini Kenya na alizoea kufuatilia matukio yake katika gazeti lake alilokuwa akilipenda sana, ''Baraza', gazeti la Kiswahili la kila wiki kutoka Kenya.

"Ilikuwa katika Novemba 1954 wakati Taratibu alipokuwa akipekuapekua gazeti hilo ndipo alioposoma habari kuhusu TANU. Taratibu aliuliza pale Singida mjini kama kuna tawi la TANU. Taratibu alifahamishwa kuwepo kwa tawi la TANU pale mjini na katibu wake alikuwa mzee mmoja kwa jina la Mzee Kinyozi.

"Taratibu alikata kadi yake toka kwa huyo mzee na akawa mwanachama wa TANU. Asubuhi iliyofuata Taratibu aliingia ofisini kwake na akaiweka kadi yake ya uanachama wa TANU yenye rangi nyeusi na kijani juu ya meza yake, kila mtu aione. Ofisa Mzungu wa PWD Singida hakuweza kuvumila ufedhuli kama ule, alishauri Taratibu apewe uhamisho kurudi Dodoma alikotoka, kabla hajaeneza sumu yake kwa Waafrika wengine.

"Kwa kifupi mzee Taratibu alijitoa kwa hali na mali kuianzisha TANU bila hofu ya kushughulikiwa na serikali ya kikoloni, licha ya kwamba alikuwa mfanyakazi. Hatimaye alichaguliwa kuwa mjumbe wa sejretarieti na kamati ya siri ya TANU (kwa pendekezo la Oscar Kambona), na baadae alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa TANU kanda ya kati, Rais akiwa Alexander Kanyamara, Katibu Abdu Mohamed Mwamba, Mweka Hazina Omari Suleiman, huku Binti Maftah Karenga, Bakari Yenga, Maalim Khalfan, Idd Waziri na Said Suleiman wakichaguliwa wajumbe."

TAFAKURI

Leo mjukuu wa mzee huyu aliyepigania uhuru anaambiwa si raia.
Mimi kama kawaida yangu nacheka. Ona nacheka tena. Yaani nacheka mno. Nacheka zaidi dogo anavyowagonga KO watu wakubwa wasiotumia 'hikma' na weledi kwenye kazi zao. Eti vyeti vya kuzaliwa vya babu na bibi zako wa upande wa mama na baba. Nina siku nyingi sijasonya!!!!!

MAELEZO YA PICHA

Kutoka kushoto ni Idd Faiz Mafongo, Sheikh Mohamed Ramiya, Mwalimu Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro na Haruna Taratibu wakiwa stesheni ya reli Dodoma mwaka 1955.
Ndimi Luqman MALOTO
Nyambeya, HIVI KOCHA MAXIMO NI MTANZANIA KWA SABABU TU ALIFUNDISHA TAIFA STARS?
 
Naona serikali inataka kujivua nguo katikati ya uwanja wa mpira na mashabiki wakiwa wamejaa!
 
Hebu shusha na historia ya ubibini na ubabuni kwa mkulu
 
9BCD434D-2BC1-400F-BBF9-92547424C835.jpeg
Hii tz imejaa viongoz shithole si kidogo
Anza hapa!
 
kumbe ndiyo maana yule kijana nijasiri mno,ametoka ukoo wa wapigania uhuru
 
Sasa hiyoo historia yote ya nini na majina mbona hayafanani kwa hiyo mnasema abdul nondo ni ccm pure ndio aache kuichokonoa na peleka hii historia uhamiaji maybe watamfikiria
 
Naona Jamaa anazidi kupata umaarufu
 
Tatizo siyo Uhamiaji tatizo ni jiwe na michanga inayolizunguka jiwe wanatoa amri kandamizi ili kuwafunga watu midomo.

Tazama hawajui hata historia ya mtu kumbe anatoka kwenye familia ya waliofia nchi hii na chama chao tawala.

Wenyewe wakiulizwa hata majina tu ya babu zao wanakuja na majina ya babu na bibi Feki . Shame on you CCM
 
Tabia ya Uhamiaji kuanza kuwaharass wote wanaoonekana kuishambulia Serikali ya CCM haijaanza leo wala juzi. Wote mnajua walichofanya kwa Jenerali Ulimwengu, Bashe, yule Padre etc. Kidogo na Manji nae wampe hilo zigo. Ni upumbavu na ulofa wanachokifanya na fedheha kubwa sana kwa mkuu wa kitengo kile kukubali kupokea maagizo kutoka juu bila kutafakari athari zake.

Hata Magufuli mwenyewe sina uhakika kama ana birth certificate ya Babu, Bibi, Mjomba na Shangazi zake. Nchi ya ajabu sana hii.
 
Back
Top Bottom