Abdul Kambaya ajiondoa CHADEMA

Abdul Kambaya ajiondoa CHADEMA

CHADEMA ni vema iwe makini inaposajili wanachama wapya.

Kwa mfano Mh. Kambaya kaja na watu wake 600 sasa hao wataitii CHADEMA au Mh. Kambaya?

Pili, unasajili wanachama wapya na kuwapa Vyeo wakati akina Yericko wanasota tu kwenye mwambao wa Bahari ya Hindi unadhani watawafurahia?

Halafu huu utaratibu wa kusajili vikundi umeanza lini na kwa sheria gani?

Mungu awabariki CHADEMA!
Katiba yao inasema chadema ni kikoba atakayeleta mpunga hauwachwi rejea lowassa na sumaye bwashee!
 
Inasikitisha Sana

Kambaya anazurura na kikundi chake kufanya Sanaa sasa ataenda kumtapeli Zitto

Ila kwa Chongollo hatathubutu!
Chongolo ndiye kamtuma kwenda kujaribu kuingia chumbani kaishia sebuleni kapewa maji ya kunywa kisha kaonyeshwa mlango wa kutokea
 
Siku chache tu Bw.Kambaya na wenzake walikimbia CUF na kwenda Chadema wakidai ndio chama chenye uhakika wa kushika dola, akapita mikoa yote ya pwani kuisema vby serikali ya CCM, wengine tunaojua siasa tukawa tunamcheka tu, Leo amerudi tena kwa waandishi wa habari na kutangaza kuihama CCM.

Ujumbe wangu kwa Kambaya ni huu.

1. Nchi hii vyama vya siasa ukiondoa CCM ni biashara
2.CCM ndio mkombozi wa kweli wa watanzania, hatukatai kina mapungufu yake lakini yanatatulika.
3.Huwezi kuwa kambale mbele ya Sugu, Lema, Msigwa, Lissu, Heche na Wenje, hao akili zao wote ni ubunge tu ili maisha yaende mbele.Kutukana kote serikali wanataka kwenda bungeni kutanua.
4.Kambaya achana na siasa, mwacheni mama apige kazi na atimize malengo yake.
5.Wenzako akina Katani waliyaona haya wakarudi CCM mapema, sasa wanapambana wakiwa ndani ya chama.
6.Utahangaika vyama vyote lkn unapoteza muda wako.
7.Kama chama cha siasa kilichokuwa cha ukweli na kilibeba matumaini ya watu kilikuwa ni NCCR Mageuzi ya marehemu prof Abdulrhaman Babu.Kiko wap sasa hivi.
8.Narudia tena, hakuna chama wala mwanasiasa wa upinzani mwenye nia ya kweli ya kuleta mabadiliko hapa nchini zaidi ya CCM.Hakuna, hakuna, hakuna.
Kama CCM waliwahi kutuletea Rais kama Jiwe na wewe bado unabinuka kukisifu hicho chama basi jua tatizo linaanzia kwako
 
Kambaya alijiunga Chadema baada ya kusikia kuwa jamaa sasa hivi walishaanza kupokea ruzuku.

Sasa alipofika huko akakuta mwenyekiti ashachagua genge lake la kutafuna nao ruzuku za chama, huku Kambaya akiwa nje ya list.

Baada ya kuona hivyo kijana akaamua kuchukua maamuzi ya kujitoa.
So umeona kumbe chama hakihitaji mtu style yake, aende akaanzishe chama chake kama Zito
 
CHADEMA ni chama cha mtu na familia yake....

Hahojiki..

Kambaya njoo CCM....tukutane huku Mandi nikupe kadi....
Kwani lazima kila mtu kujiunga CDM? Kama hukipendi chama kaa pembeni tu hakuna wa kuja kukulazimisha
 
Back
Top Bottom