99.9% ya Wananchi wanamkubali Rais Samia Suluh Hassan

99.9% ya Wananchi wanamkubali Rais Samia Suluh Hassan

Msijali wakuu,

Huyu jamaa kaandika kinyume chake ili asiwaudhi machawa wa mama kina the sank the falacy
Mama ndio tumaini la watanzania katika kuwaletea maendeleo, mama ametoa nuru katika mioyo ya watanzania, kwa Sasa mama Hana mpinzani anayeweza kushindana Naye popote pale
 
Nyie ndo mnapotosha au mnafanya ccm watu waione vilaza kwanini mnafanya hivi
 
Zaburi 12:1-5

[1]BWANA, uokoe, maana mcha Mungu amekoma,
Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.
[2]Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe,
Wenye midomo ya kujipendekeza;
Husemezana kwa mioyo ya unafiki;
[3]BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza,
Nao ulimi unenao maneno ya kiburi;
[4]Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda;
Midomo yetu ni yetu wenyewe,
Ni nani aliye bwana juu yetu?
[5]Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge,
Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji,
Sasa nitasimama, asema BWANA,
Nitamweka salama yeye wanayemfyonya
Asante allypipi kwa kutuwekea Zaburi hii nilikua sijaisoma mda
 
kuna uzi umetoka ukidai mama hakubaliki baada ya ccm kushupaza shingo kuona uzi wa jambo ilo wameamua kurudisha majibu haraka haraka huku minyoo ya tumbo ikiwa imeshiba
 
Ngoja waje chawa wengine, lucas, the sunk njooni muandike essay hapa uwanja ni wenu
 
Mama anakubalika sana, tena sana tu wala usitumie nguvu nyingi asiyetaka ajinyonge kama hawezi anywe sumu au kama vipi burundi sio mbali,
Hongera sana samia
Ikiwezekana uwe wa maisha tu,

Staki povu, kama umechukia inama au pita kimya kimya
 
Hiyo ipo wazi machoni na akilini mwa mamilioni ya watanzania ambao wameonyesha upendo wa kipekeee kwa mh Rais wetu kwa namna wanavyomkubali, hata Mimi huku niliko kiukweli mh Rais wetu anakubalika sijapata kuona,

watu wanaimani kubwa Sana na mh Rais wetu, watu wanasema wanahitaji mh Rais aendelee kutuongoza Kama Rais kutokana na namna alivyo gusa maisha yao.

Kama kwetu wakulima ndio hutwambii kitu juu ya mh Rais wetu kwa namna alivyogusa na kukonga nyoyo zetu baada ya kutoa Ruzuku katika mbolea na kupelekea kushuka kwa Bei ambayo Ni tofauti na msimu uliopita
Huo ndio ukweli,kila mwananchi,anamuunga mkono,Rais wetu.
 
Nimetembea sehemu nyingi sana Tanzania, kwenye mikusanyiko ya watu wanampongeza Rais Samia kwa kuwa na uongozi thabiti. Mpaka jana, kulikuwa na maonyesha ya biashara ya kina mama wa kila kabila, kila dini na wa kila rangi. Maonyesho hayo yanaoitwa Women Galla.

Wanawake walileta mpaka vyakula wanavyouza mitaani(mama ntilie, huku wanaiwata mama lishe) na bidhaa mbalimbali nk. waliniambia tumefanya biashara tunamshukru Mungu, na tunamshukuru Mh. Rais Samia. Kina mama wajasiriamali waliniambia wapo hapo jana ikiwa ni siku 4 na pia wakamshukuru sana Meya wa mji huo kwa kuandaa tamasha hilo.

Na wakazi wa mji huo pia walifurahi nakusema ni ubinifu haujawahi kutokea, na kuwaletea wasanii wa Mama Kimbo, waliniambia huu ni ubunifu wa hali ya juu hasa kufanyika katikati ya mji. Vijana wengi pia walishukuru kwa kupata kazi ya usalama wa eneo husika, walipata ajira.

Pia vijana wa bodaboda, bajaji, guta ya pikipiki kwa wingi wao walishukuru sana kwa kupata abiria. Wenye maguta walikuwa wakipata bidhaa za wafanyabiashara. Bila kuwasahau wenye biashara ndogo ndogo na wenye michezo ya watoto kama magari ya watoto, mabembea nk. nao walishukuru sana.
Punguza kuota mchana
 
Back
Top Bottom