TUPACified
JF-Expert Member
- Feb 27, 2015
- 1,367
- 604
Nimeona man. Niliamua kupotezea coz kuelewa kifo cha Pac inabidi kwanza kuelewa 'the conspiracy world', halafu kumuelewa yeye mwenyewe pia.pamoja sana mkuu Tupacified kwa ufafanuzi na maelezo ya kina, binafsi nimepata kitu toka kwako
japo ni mtoto wa jana (jokes)
Wadau hapo juu wametoa michango yao kuhusiana na kifo cha 2pac na nani ali-mastermind mchezo mzima na kwa maslai ya nani? au jamaa binafsi alikuwa troublemaker hivyo alijitengenezea kifo chake yeye mwenyewe?
Maisha yake ya ku-hustle ni taswira halisi ya nyimbo zake unadhani hilo pekee inaweza kuwa ndio siri ya mafanikio yake kimuziki?
Funguka mkuu uwanja wako huu
Kwa ufupi tu, Pac alikufa kwa sababu ya mdomo wake na ushawishi wake kwa waliomskiliza. Aliwahi kukiri mwenyewe kwamba he had a 'big mouth', and that was the cause of all his troubles. Atakayeelewa hili kwanza ndio naweza kuendelea nae.
Kuhusu muziki na mafanikio yake. Pac hakuwa mtunzi, alikuwa anaelezea tu chochote anachokutana nacho katika maisha yake, chochote. Ndio maana ngoma zake nyingi ukiskiliza unaona hisia alizokuwa nazo, iwe hasira, woga, upweke, furaha, you name it. Hii ndio ilisababisha akawa na special connection na mashabiki wake na kufanya awe tushio sana kwa waliomuua. + the fact jamaa alikuwa na mizizi na damu ya harakati, na jina lake pia linamaanisha 'kiongozi' ama kitu kama hicho. So kifupi Pac alizaliwa kuongoza watu, na nguvu yake kubwa ilikuwa kwenye mdomo, kichwa chake, moyo wake. Jamaa walifanya kila namna kumzuia ila ndio kama walimchochea, mwisho wa siku he had to die.