Panapo majaliwa 2030 nitatimiza miaka 40 umri amabao utaniruhusu kugombea urais. Nikiukwaa urais nitafanya mabadiliko makubwa ya muundo wa serikali na sera zake.
Ili kuyapata mabadiliko haya nitaunda jopo la wataalamu 16 (8 toka Zanzibar na 8 toka Tanganyika) litakaloandika katiba mpya kwa niaba ya watanzania.
Natamani kuliona Tanzania nitakayiongoza ikiwa na:-
1. Serikali ndogo yenye mawaziri 5 na manaibu waziri 5.
2. Cheo cha makamu wa rais nitakifuta. Rais akiachia madaraka kwa sababu yoyote ile nafasi yake itajazwa kwa uchaguzi kama wafanyavyo Namibia.
3. Wabunge watakuwa 2 tu kwa kila mkoa. Mmoja mwanamke na mmoja mwanaume. Watapatikana kwa kugombea kama inavyofanyika hivi sasa. Kutakuwa na kura za kumpata mbunge wa kike na kura za kumpata mbunge wa kiume.
4. Nitafuta kitu kinachoitwa pension. Ili kutenda haki na kujenga usawa kwa wazee wote kila mtu atapatiwa posho. Posho hii itakuwa sawa kwa kila mzee, awe mkulima, awe mstaafu wa shirika la umma ama ikulu. Wote watapewa posho moja. Maana wote wamelitumikia taifa moja ktk nyadhifa na kazi tofauti. Thamani ya mzee Kikwete na mzee Matonya mkulima wa huko Dodoma vijijini wana thamani sawa, kwahiyo watahudmumiwa kwa usawa.
5. Afya itatolewa bure kwa watoto wote walio chini ya miaka 5, walemavu na wazee. Wengine wote watachangia, bila kujali ni mjamzito ama la.
6. Vyeo vifuatavyo nitavifuta. RC, DC na DED.
Mungu ibariki Tanzania. Mungu mbariki Sexless
Ili kuyapata mabadiliko haya nitaunda jopo la wataalamu 16 (8 toka Zanzibar na 8 toka Tanganyika) litakaloandika katiba mpya kwa niaba ya watanzania.
Natamani kuliona Tanzania nitakayiongoza ikiwa na:-
1. Serikali ndogo yenye mawaziri 5 na manaibu waziri 5.
2. Cheo cha makamu wa rais nitakifuta. Rais akiachia madaraka kwa sababu yoyote ile nafasi yake itajazwa kwa uchaguzi kama wafanyavyo Namibia.
3. Wabunge watakuwa 2 tu kwa kila mkoa. Mmoja mwanamke na mmoja mwanaume. Watapatikana kwa kugombea kama inavyofanyika hivi sasa. Kutakuwa na kura za kumpata mbunge wa kike na kura za kumpata mbunge wa kiume.
4. Nitafuta kitu kinachoitwa pension. Ili kutenda haki na kujenga usawa kwa wazee wote kila mtu atapatiwa posho. Posho hii itakuwa sawa kwa kila mzee, awe mkulima, awe mstaafu wa shirika la umma ama ikulu. Wote watapewa posho moja. Maana wote wamelitumikia taifa moja ktk nyadhifa na kazi tofauti. Thamani ya mzee Kikwete na mzee Matonya mkulima wa huko Dodoma vijijini wana thamani sawa, kwahiyo watahudmumiwa kwa usawa.
5. Afya itatolewa bure kwa watoto wote walio chini ya miaka 5, walemavu na wazee. Wengine wote watachangia, bila kujali ni mjamzito ama la.
6. Vyeo vifuatavyo nitavifuta. RC, DC na DED.
Mungu ibariki Tanzania. Mungu mbariki Sexless