2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Racism ilianza hivyo hivyo kwa ku refer vitu vibaya na rangi nyeusi.

Ndio maana leo ukichorewa picha ya shetani lazima awe mweusi.

Pengine ndio sababu nyingine inanipa confidence kutoshabikia Argentina kwasababu ya racism
View attachment 3632938
Hata mimi Argentina wamenitoka kabisa kutokana na ubaguzi wao.

Nilipoona katoto ka ki Argentina huku kakiwa hyped na mama yake [nadhani] kakimuita nyani jina la Vinicius Jr, nikachora mstari kwenye mchanga.

Pia, jinsi ambavyo mashabiki wa Argentina walivyom treat iShowSpeed…..hapana kwa kweli.
 
Rodri kashinda player of the tournament

Man City waliposhinda Uefa championships league 2023
Spain waliposhinda Uefa nations league 2023
Spain waliposhinda Uefa Euro 2024
Leo fainal ya WC 2026 ?
 
Naukubali sana hispania na mfumo wao wa uchezaji wa 4-3-3 chini ya mbinu zinazosisitiza umiliki mkubwa wa mpira, pasi nyingi fupi (Tiki-Taka), na kushambulia kupitia mawinga yenye kasi.

Pia argentina wamefika finali kwa hu mfumo wao wa uchezaji unao badilika-badilika kutegemeana na mpinzani, huku mifumo ya 4-4-2 na 4-3-3 ikiwa ndiyo msingi mkuu. Wakiwa na morali ya kipekee ya kushirikiana sana na uvumilu wa hali ya juu(mfano kwenye mechi ya uingereza na Egypt). Huenda itakua fainali nzuri sana naya kuvutia kama ile ya(argentina na ufaransa)Qatar 2022.
 
Back
Top Bottom