Huyo jamaa kaandika issue aliyoreport moiina imewavua nguo, bila kujua kuwa hiyo issue sio mpya hata huko Argentina media za huko zimekomalia hiyo issue. Hivyo Hadi hapo huyu baba mwajuma alitaka kutupiga uongo
Kabla hatujaenda mbali ili kupimana uelewa ni muhimu, so lazima nikuulize maswali kidogo: kwa nini FBI na US justice department wanaochunguza chama cha soka cha Argentina AFA na sio FIFA? Tuanzie hapo kwanza
FBI ipo kwenye hatua ya awali ya uchunguzi (preliminary investigation) na kulingana na taarifa zilizochapishwa na lile gazeti Nancion (sina hakika na spelling zake)
Gazeti hilo lilidai kuwa FBI ipo kwenye hatua ya kukusanya ushahidi kuhusu viongozi wa AFA na uhusiano wa kampuni ya TourprodEnter LLC iliyopo Marekani.
Kinachofanya FIFA waingie kwenye huu msala ni kutokana na tuhuma za utakatishaji fedha ambao unamkabili Raisi wa AFA na wenzake.
Hizo pesa zinawa link FIFA kwasababu wao ndio waliokuwa wahusika kwenye kutuma hizo pesa ambapo walitakiwa wazitume kwenye account rasmi ya AFA kule Argentina.
Badala yake zikatumwa kwenye account ya TourprodEnter LLC.
Kwanini FIFA inahusishwa? FIFA ndio mwenye mamlaka ya utoaji na uidhinishaji wa malipo au zawadi kwa washindi.
Na kisheria FIFA ina idaranya ukaguzi ambayo inalazimika kuzuia fedha kwenda kwenye account binafsi au taasisi isiyoeleweka.
Sasa pamoja na hayo bado FIFA walisaini na kuidhinisha hayo malipo.
FIFA haiishii tu hapo kwenye kulipa haya mashirikisho pesa za ushindi na zawadi, FIFA pia wana mandatenya kukagua hesabu na matumizi ya hayo mashirikisho ambayo yapo chini yake.
Na kingine kikubwa zaidi ambacho kinampa title Romain Molina ni uchunguzi wa kashfa za unyanyasaji wa kijinsia.
Mmoja wa makocha wa zamani wa bijana aliwahi kushtakiwa kwa unyanyasaji na wachezaji kadhaa lakini FIFA walifunga jalada la kesi hii bila kuchukuliwa hatua huyo muhusika kwa madai ya kwamba hakuna ushahidi wa kutosha.
Unaikumbuka ile kashfa ya FIFA Gate ya 2015?
Pattern zake jinsi ilivyoanza inafanana kabisa na hi sakata.
Ngoja mpaka mtu aliwe kichwa ndio mtaamini.