Mechi ya kwanza ya mpira kuumia maumivu makali ni Man U Vs Barca 2010 kama 11 kama sikosei enzi hizo nipo shule ya msingi , napenda Man U kuliko kitu chochote Duniani siku hiyo nilipata tabu sana na ukawa mwanzo wa kumchukia Messi.
Yanga na Mamelodi sikuamini eti mtu mzima nishindwe kulala kisa maumivu ya mpira dah! maumivu yalidumu kama wiki mbili mpaka nikasahau , tokea siku hiyo mpaka leo kama nimeacha hata kuangalia mechi za Yanga . Mpaka Leo haijalishi Yanga anacheza mechi gani hauwezi kunikuta natoa hela yangu kwenda Banda umiza kucheki na kuifuatilia kama zamani .
Sasa maumivu ya mpira sina kabisa baada ya depression nilipunguza kama sio kuacha kabisa ushabiki , sasa nacheki mechi moja Moja tu au michuano muhimu kama burudani tu na sio kama shabiki kindakindaki wa kuumia kama zamani