Kanungila Karim,
- Nitalalaje wakati nchi iko njia panda?. Furaha gani niliyokuwa nayo mimi mpaka nilale usingizi mnono!
- Mfukoni chapaa hakuna, kuna watu wamepotea mpaka sasa hawajulikani wlipo, mishahara wafanyakazi hawaongezwi kwa mujibu wa sheria, trilioni 1.5 zimeyeyuka, tuna hela za kurudia chaguzi za kuunga mkono juhudi lakini hatuna hela za katiba ya wananchi.
- Nitalalaje wakati tunaambiwa imeundwa mahakama ya mafisadi lakini waliotajwa kwenye ripoti ya makinikia bado wapo mtaani wanadunda.
- Nitalalaje wakati wote waliotajwa kwenye listi ya madawa ya kulevya hakuna hata mmoja aliyeko jela?
- Hebu niambie utalalaje wakati kuna wananchi wanavunjiwa nyumba halafu wengine wanaambiwa wasivunjiwe kwa sababu walimpa mtu kura.
- Niambie wewe mwenyewe, ulale, usingizi utoke wapi wakati kiongozi anayepaswa kuheshimu sheria anaagiza mzigo kutoka nje ya nchi , mzigo unafika bandarini halafu anataka kukwepa kodi na bado anaachwa ofisini aendelee na kazi ya kuhimiza watu walipe kodi!
- hebu ndugu yangu tusemezane, utalala usingizi utatoka wapi wakati kuna watu wamefukuzwa kazi kwa vyeti feki lakini mwingine anaambiwa achape kazi tu maadamu anajua kusoma na kuandika
- Nitalalaje kwa mfano ili iweje wakati ndoto ya nchi yangu kupata Trilion 425 sawasawa na Noah Moja kwa kila mtu imepotea
- Sijui wewe mwenzangu, Lakini mimi nimeshindwa kulala kwa sababu serikali hii imekataa kutekeleza ilani ya chama, imekataa kutoa milion 50 kila kijiji, imekataa watoto wanaopata ujauzito kuendelea na masomo, imekataa kukamilisha mchakato wa katiba kinyume cha ilani. Katika mazingira kama hayo nitalalaje mimi?
- Nitalalaje wakati Trafiki wanaambiwa buku tano ni hela zakung'arisha viatu, naumiza kichwa nitazipata wapi buku tano za kumpa afande ang'arishe viatu
- Nitalalaje wakati Mbunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano yupo nje anatibiwa kwa pesa za hisani ya serikali nyingine wakati serikali yake yenyewe imekataa kumpa hata senti tano. nitalalaje mimi kwa mfano!
- Nitalalaje kwa mfano, kwa raha gani wakati siasa za kistaarabu hazipo, yaani ni ubabe ubabe, undava undava, viongozi wakuu takriban zaidi ya asilimia 90 ya viongozi wa vyama vya siasa vilivyopo kwa mujibu wa sheria wana kesi mahakamani
- Nitalalaje ndugu yangu, Nanyimwa kuwaona Laivu wawakilishi wangu bungeni, lakini naonyeshwa kila mara, kila wakati mtu mmoja
Katika Mazingira kama haya, ndiyo maana nimeamka na kusema twende na Membe tu 2020 haya mambo hayatakuwepo!