2015 yako ilikuaje,lets share,2016 umejipangaje

2015 yako ilikuaje,lets share,2016 umejipangaje

Asante Sn, Nimepanga Tarehe Ingawa Bibi Harus Bado Hajapatkana. Lakini Mungu Ni Mwema.

Nadhani usipange kwanza tarehe, ila umpate na umchunguze kwanza. Ikiwezekana uonje kidogo japo dhambi. Kisha uweke mipango.
Baba mchungaji
 
Kweli tunatofautiana....

2014 niliweka lengo la ku establish business...DONE
2015 niliweka lengo kujenga......95% DONE
2016 lengo langu ni kuoa........HII NI CHANGAMOTO KUBWA KULIKO ZOTE NILIZOPITIA!

Ni kweli mkuu tunatofautiana katika kuweka malengo na vipaumbele .....
 
Kwa upande wangu namshukuru sana MUNGU kwa kunipa uhai mpaka kufikia siku ya leo nazidi kumuomba pia anifikishe mwaka ujao salama Amin.
 
Mie nashukuru Mungu kwa uzima wa afya pia nimeweza kumaliza masomo salama licha ya vikwazo na ushawishi nilioupata
God is soo good
 
Me ulikuwa mgumu totally kwangu,na siupendi mpaka basi.Siasa,mapenzi,maisha,kazini daaa ni misukosuko. kichwa kinauma.
 
Mimi namshukuru Mwenyenzi Mungu kwa mwaka 2015. Ukweli ni kuwa ulikuwa mwaka bora kabisa kwangu. Changamoto nilizopitia zitakuwa fursa kwa mwaka 2016.

Katika yote namtukuza Yesu Kristo. Amen
 
Mwaka huu ulikuwa mzuri kwangu almost 90percnt ya malengo yangu yametimia namshukuru Mungu ingawa niliyempenda kaniharibia mwaka kaniacha katika mazingira tatanish full stress namwomba Mungu anipe ubavu wangu mwakan
 
Namshkuru Mungu mwaka umeenda vizuri ingawa kulikua na up`s n down`s kidogo but all is well kwa kweli Mungu anajaalia.....am praying Mwaka 2016 uwe wa heri na baraka kwa kweli...
 
Namshukuru Mungu kwa uhai na afya njema mwaka huu lengo lilikua ni kupata a dream job bado sijaipata Mungu mwema najua mwakani nitajaliwa na kufanya na mambo mengine
 
Mimi namshukuru Mungu ni kutimiza malengo yangu kwa asilimia 95. Kilichonisaidia ni kupambana kuanzia januari.
 
Mwaka huu namshukuru Mungu kwa mambo yote aliyonijalia. First half ya mwaka haikuwa nzuri sana mambo kadha wa kadha hayakwenda sawa. Mwanzo wa mwaka biashara zote nilizojaribu zilifeli, nilikuwa na mahusiano unstable na changamoto nyinginezo.

Namshukuru sana Mungu second half nimefanikiwa mambo mengi japo pia nilikumbana na changamoto nyinginezo za kimaisha.

Najiandaa na mwaka ujao nikiweka focus ya kutatua changamoto za uwekezaji, mahusiano na utaalamu.
 
mwaka bora uishe tu, mana ulikua mbaaayaaaaaaaaaa" ptuuuu ............... nimshukuru mungu tu kwa uzima.
 
Huu mwaka kusema kweli ulinianzia vibaya....nilikuwa nimejiwekea mipango yakatokea mambo fulani yaliyokuwa nje ya uwezo wangu yakavuruga kila nililolipanga....namshukuru Mungu kwa kila jambo though,maana ninaamini kila linalotokea kwenye maisha ya mwanadamu lina makusudi....nimekumbana na changamoto nyingi za kimaisha mwaka huu ila nadhani ndo kukua kwenyewe. Pamoja na yote yaliyotokea mwaka mzima namshukuru Mungu mwishoni mwa mwaka nimepata faraja kwa sehemu na ninaamini ni ufunguo wa mwaka 2016.... Mungu awabariki marafiki wa Jf
 
Namshukuru Mungu kwa uhai na afya njema mwaka huu lengo lilikua ni kupata a dream job bado sijaipata Mungu mwema najua mwakani nitajaliwa na kufanya na mambo mengine

unacho nena ndicho kitakachokutokda
 
God is great, nashukuru Mungu kwa kila kitu kwa mwaka huu kuanzia mahusiano yangu na ubavu wangu kwa familia yangu, na kwa mafanikio niliyoyapata na Changamoto zake.Nilichojifunza mwaka, kesho yako utakua determined na unachokifanya leo.Mungu atusaidie tumalize mwaka vizuri na 2016 uwe full of blessings. Cheers
 
Mwaka huu kwangu kwa upande ni mzuri maana nilipata kazi serikalini iliyonipa furaha tofauti na kazi za awali nilizo kuwepo za private,upande mwingine umekuwa mbaya maana 3/4 ya kipato nilichokipata nilikiwekeza ktk biashara iliyonipa hasara sana.
2016,hope utakuwa mwaka wangu mzuri kama mungu atanipa uzima!.targets ni 1.kuanzisha familia kupata mke na mtoto,
2.kuwa na investment imara itakayoniingiza kuanzia 3M Kwa mwezi
3.kuanza ujenzi wa nyumba na maandalizi ya kwenda shule 2017

4.
 
Mwaka 2015 ulikua poa sana kwangu japo uku mwishoni kidogo sana nmeharibu but namshukuru Mungu yeye ni mwema wakati wote naamini 2016 ntafanyapoa sana
 
Back
Top Bottom