2015.......Tujipange!

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Najua tupo 2010 na hata uchaguzi wa mwaka huu hauja isha. Najua bado watu wapo katika hali ya furaha na matumaini mapya kusikia Mh. Slaa ana gombea uraisi. Najua wengi wetu tuna tamani muda uwe huu na wakati uwe huu. Ukweli ni kwamba Tanzania haija jipanga kwa mabadiliko yoyote 2010. Vumbi likisha tulia tuta kuta hali ni ile ile.

Watanzania tuna kasumba ya kusubiria uchaguzi ndiyo kuwa na mwamko wa kisiasa. Hili lime thibitishwa na hali halisi ya miaka 2005-2010. Tunge kuwa ni nchi nyingine basi kwa sasa tunge kuwa tuna subiria kuhalalisha uongozi wa chama kipya na utawala mpya. Sasa pamoja na yote yaliyo tokea miaka hii mitano bado hakuna uhakika wa upinzani kushinda. Hapo lazima wenyewe tujiulize ni kwa nini.

Binafsi sina mapenzi na chama chochote cha upinzani. Na sifichi ukweli kwamba nime kuwa mpenzi wa CCM tokea udogo haswa kutokana na kumu idolize Nyerere. Ila pia naweka mapenzi ya nchi mbele ya mapenzi ya chama. Najua Tanzania ita nufaika sana na upinzani wenye nguvi na vyama vinavyo pokezana mara kwa mara. Najua fika kwamba mwaka huu uraisi unge takiwa uende kwa Slaa. Lakini sidhani kama hayo yata tokea mwaka huu.

Wakuu safari bado ni ndefu. Ushindi hautokani tu na hisia na hamu za ushindi bali hutokana na mikakati na utekelezaji. Tanzania bado hatuja jiwekea mazingira ya kupokezana madaraka au kuweka utaifa mbele ya itikadi za kichama na mapenzi yetu na watu binafsi.

Tuchukulie kwa muda mfano wa timu. Kwenye timu yoyote kuna yule mchezaji mmoja au wawili ambao ndiyo mastaa wa kikosi. Lakini timu hii hata iwe na mastaa wangapi au staa mkubwa kiasi gani haiwezi kufanikiwa bila wachezaji wa akiba wazuri, kocha mzuri na uongozi mzuri. Staa yoyote hawezi kubadilisha timu mbovu bila kete zingine kuji panga vizuri.

Wagombeaji "mastaa: tunao wengi tu kuanzia ngazi za udiwani mpaka uraisi. Lakini swala ni je hawa "wachezaji nyota" wana weza kufanikiwa bila mazingira ya kufanikiwa kuwepo? Tume jiwezesha vipi kuhakikisha kwamba wachezaji wetu nyota wana weza kutusaidia kufanikisha malengo yetu? Tukubali ukweli kwamba Tanzania tuna nyota wengi tu wa kisiasa au watu ambao wana utashi wa kuweza kuwa nyota wa kisiasa. Lakini sisi kama wapiga kura bado hatuja wawekea mazingira ya kushinda.

Kwa hiyo wakuu sisemi na wala sishauri tukate tamaa. 2010 bado haija isha. Ninavyo sema mimi ni kwamba hatuja jipanga vya kutosha na matokeo yoyote mwaka huu hayata tosha kuleta mabadiliko ya kudumu katika mfumo wetu wa kisiasa. Ila tusi kate tamaa na tusichoke. Tuji pange kwanzia sasa kwa ajili ya ushindi wa baadae. Tukumbuke kwamba ngo'mbe hanenepi siku ya mnada bali hushiba tu na kuvimbiwa. Mwaka huu ngo'mbe wetu haja nenepa bali tumefanya haraka haraka kumshibisha na kumvimbisha. Hali hii italeta mafanikio madogo kuliko tunayo taka na hayata kuwa ya kudumu. Tuji pange kwanzia sasa. 2015 si mbali!
 
Mkuu umesema kweli..lakini...
kuna watu hapa barazani KUPENDA kwao kunawafanya wasikubaliane na ukweli, sijui ni kujipa moyo!!
ila waangalie wasije wakajipa maradhi ya MOYO,, haya mambo haya!!!......
 
Binafsi sina mapenzi na chama chochote cha upinzani. Na sifichi ukweli kwamba nime kuwa mpenzi wa CCM tokea udogo haswa kutokana na kumu idolize Nyerere. Ila pia naweka mapenzi ya nchi mbele ya mapenzi ya chama. Najua Tanzania ita nufaika sana na upinzani wenye nguvi na vyama vinavyo pokezana mara kwa mara. Najua fika kwamba mwaka huu uraisi unge takiwa uende kwa Slaa. Lakini sidhani kama hayo yata tokea mwaka huu.

Angalau leo umekubali mwenyewe kuwa wewe ni mpenzi wa chama cha mafisadi ... last time uliambiwa hili ukaruka kimanga ... ohh .... msiniionee...ohh....mimi sina chama..

Come on, watu walishasoma maandishi yako muda mrefu tu wakayajua mapenzi yako kwa chama la kijani. Ndo maana ule ushauri wako feki uliokuwa unautoa hapa kwa wapinzani ulikuwa unapuuziwa.

Ama kweli siku ina masaa 24 ... umevumilia weeee kwenye closet (kibanda ndani ya chumba) lakini uzalendo umekushinda
 
Mwanafalsafa1,
Mkuu pengine umesahau kwamba mwaka 2005 tulisema haya haya kujipanga kwa mwaka huu 2010. Nakumbuka mimi sikuwa na support Chadema lakini baada ya mazungumzo marefu sana yanayohusiana na sera zao, Ukabila. Udini na hatua Chadema kuchukua hatua kadhaa za kuunganisha nguvu na vyama vingine ili mwaka huu tuweze kupata Ushindani wa kweli..

Mwisho wa siku yote haya yameshindikana..Watanzania wasomi unaowazungumzia hapa walianza hoja upya kupinga upya Chadema na vyama vikasambaratika ktk chaguzi ndogo pasipo sababu ya maana.

Hii ndiyo Tanzania nayoifahamu mimi. Hawa ndio watu naowafahamu mimi wanasema saana na wajuzi wa kuchambua lakini wagumu sana kujihusisha na harakati inafikia wakati mchango wao unahitajika..Tumekuwa Tiafa la kugawanyika kila mtu na mzigo wake na pengine kweli ile itikadi ya UJAMAA na KUJITEGEMEA ni viungo ambavyo haviwezi kuwa pamoja kama maji na mafuta.

Leo tukianza ndoto mpya ya mwaka 2015 ni vichekesho vitupu kwani nina hakika tutarudia kuzungumza maneno yale yale tulozungumza miaka mitano iliyopita. Kuchambua na kulalamika juu ya CCM, vyombo vya serikali, viongozi mafisadi, Udini, Ukabila na mengineyo ambayo ndio ktk mlolongo wa maisha yetu kama watawaliwa lakini hakuna jipya litakalo tokea by July 2015 zaidi ya kuongeza muda wa matumaini kufikia 2020.

Vijana kumbukeni kwamba kina Nyerere na waasisi wetu wote wa Uhuru wamekuwa active ktk mapambano ya kujikomboa wakiwa na umri wa miaka 20+ toka Nyerere, Salim, Fundikira, Mwapachu, Abdulrahman Babu na vigogo wengine wote juhudi zao wamezifanya wakiwa na nguvu kubwa ya Ujana wao. Sasa leo nyie kila mwaka mnaahirisha kwa sababu sizizokuwa na msingi mnasubiri hadi mmekwisha kuwa mibabu mizima yenye majukumu kibao ndio unafikiri mtapata muda wa kujipanga upya?.

Mkuu wangu hujachelewa, jiungeni nasi wakati ndio huu 2015 hujui kama utakuwa hai bado na hakika mageuzi ni kila siku ya maisha yako hayasubiri muda muafaka kwani hakuna ajuaye kati yetu - Join the force now!
 
..hii hoja yako ingesubiri kwanza uchaguzi wa mwaka huu 2010 uishe. ni hoja nzuri lakini huu siyo wakati wake.
 
Ndo maana ule ushauri wako feki uliokuwa unautoa hapa kwa wapinzani ulikuwa unapuuziwa.

Na hata huu tunaupuuzia pia,huyu Mwana FA ndo wale wanaotumiwa kutupotosha tusijadili namna ya kupata viongozi bora (kwa kuiondoa CCM Madarakani),anataka atuaminishe hivyo,anasubiri 2015 ikifika aseme "Tujipange 2020",Tumpuuzie na hii post yake na tu focus ni jins gani Dr.Slaa anaweza akaingia Madarakan na kutuletea Tanzania yenye Neema,Yenye kujali utwala wa sheria na kuwa na nia ya dhati ya kupambana na rushwa.
 
Na hata huu tunaupuuzia pia,huyu Mwana FA ndo wale wanaotumiwa kutupotosha tusijadili namna ya kupata viongozi bora (kwa kuiondoa CCM Madarakani),anataka atuaminishe hivyo,anasubiri 2015 ikifika aseme "Tujipange 2020",Tumpuuzie na hii post yake na tu focus ni jins gani Dr.Slaa anaweza akaingia Madarakan na kutuletea Tanzania yenye Neema,Yenye kujali utwala wa sheria na kuwa na nia ya dhati ya kupambana na rushwa.

Tupo pamoja Mkuu Bramo, ile janja yao ya kudai watu wa Karatu hawaafiki Dr. Slaa kugombea Uraisi imezimwa juzi baada mamia kwa mamia ya wana Karatu kujitokeza, kusimamisha shughuli zao na kwa kauli moja kumwuunga mkono agombee. Sasa tena wanakuja na janja nyingine eti tujipange kwa mwaka 2015, kwani October 3, 2010 imeshapita na msanii wetu Kikwete bado yuko madarakani ? Kwa nini linalowezekana leo lingojee kesho ? Kwa nini Watanzania tuendelee kuteseka kwa miaka mingine mitano wakati nia, uwezo na sababu tunazo za kujinasua kutoka mikononi mwa hawa wababaishaji wanaojali tu matumbo yao ?

Je tuna hakika gani kuwa mwaka 2015 hawa walafi na waroho wa madaraka watakuwa wametosheka kiasi cha kuachilia utawala kilaini bila mbinde ? Naomba tusijidanganye tena kwani kama kuna wakati mwafaka wa kuondokana na uongozi huu mbovu uliodumu kwa miaka hamsini, ni sasa. Wana jamvi, saa ya ukombozi ni sasa na maadam kamanda kapatikana, hakuna kulala hadi kieleweke - ngoja ngoja yaumiza matumbo !
 
Kumbukeni kuwa wakati mnajiandaa kujipanga kwa 2015 Rostum na vikaragosi wake tayari wamefanya maandalizi na wameanza kumulika 2020.
 
Wakuu naona wengi wenu mmeshindwa kuelewa ujumbe. Aidha kwa kuto kuangalia ujumbe kwa ndani au kuswekwa na hisia za mabadiliko mmeshindwa kuelewa ni nini haswa nasema. Kamwe sija sema mapinduzi yaanza 2015 na wala sija sema kitu chochote kisifanyike kwa sasa tuki ngojea 2015....lahasha. Hata sasa hivi tunaendelea kupambana na kudai mabadiliko tunayo yataka.

Ninacho sema mimi ni kwamba pamoja na kuamini kwamba sisi kama wananchi tunaweza fanya chochote ila pia lazima tukubali uhalisia wa mambo. Uhalisia wa mambo si kwamba mabadiliko haya wezi kuja leo. Uhalisia wa mambo ni kwamba bila mipango ya muda mfupi na muda mrefu basi mafanikio mtu unayo yapata ni ya muda mfupi. Ni watu wangapi wameweza kutoka kwenye umasikini waka tajirika ghafla lakini bila mipango ni hizo pesa zao waka jikuta wakituri walipo toka? Ninacho ongelea mimi haswa ni kuhakikisha mafanikio ni ya kudumu na si ya muda mfupi.

Nadhani wengi mnasahau kwamba kazi si mwaka huu tu. Slaa akifanikia na akashinda bado itabidi yeye na chama chake kiongoze serikali kwa miaka mitano. hamna anaye ongelea nini kifanyike baada ya ushindi kana kwamba kutoka kwa CCM tu ndiyo mwisho wa kazi. Wengi wenu mtasema tukazanie kuona kwanza ushindi wa upinzani lakini mimi ni mtu ninaye penda kuangalia mbele. Ni sawa sawa na kuomba visa ya kwenda kusoma ne bila kufikiria ada utailipaje. Mimi ni wale ambao siyo tu naangalia visa nitaipataje bali ada na mahitaji mengine nita yafanikishaje....kuangalia mbele.

Cha pili ni kwamba hata CCM ishinde mwaka huu bado itakua tishio 2015. Na kama upinzani utafanikiwa kuingia madarakani ispo angalia inaweza kufanya makosa yanayo weza kuipa CCM nguvu tena vile vile. Ndiyo maana ninasema tusiangalie kupata tu mafanikio ya muda mfupi. Lakini wengi wana taka tuamini mapinduzi ya upinzani kana kwamba ni dini isiyo weza kupingika na kwamba mkosoaji yoyte basi ni msaliti wa mapinduzi. Tuangalie facts na tuangalie jinsi ya kutatua matatizo kabla hayaja tokea.

Hoja yangu ina baki pale pale kwamba Tanzania tunge kua nchi nyingine basi kushindwa kwa CCM mwaka huu unge kua ni lazima kama vile Labor pati walivyo shindwa na kila mtu hata kabla ya uchaguzi walijua chama kile kinaondoka madarakani. Leo hii nani ana weza kusimama na kuhakikisha hilo?

Tatizo ni kwamba Tanzania tume zidi ushabiki na hatupendi kuambiwa ukweli. Mimi nimeona hatari iliyopo tusipo jiandaa mapema. Na haki ya Mungu nawa hakikishia kwamba maneno yangu yata kuja kujirudia. Nime toa hali halisi. Haimaanishi swala hili haliwezi kupatiwa ufumbuzi lakini hauwezi kusema tuvuke daraja hilo tuta kapo lifikia. Sasa hivi kuna wanaosema tayari mimi ni mpenda mafiadi. Sawa niite utakacho. Ila ukweli ni kwamba hao tunao waita mafisadi wame jipanga kutawala milele na hawa angalii leo tu. Mentality hii ya kwamba tuvuke uchaguzi huu tu ndiyo ume fanya vyama vingi vya upinzani kila baada ya uchaguzi vipotee mpaka uchaguzi ujao.

Kwa hiyo ndugu zangu niiteni mnavyo penda lakini najua kuna ukweli kwa niliyo sema hata kama nita kuwa nime kosea sehemu au kutafoutiana na mawazo yenu. Angalieni kiundani mambo yalivyo. Ushabiki usio na mantiki hakuto kusaidia Tanzania. Tanzania ita saidiwa na kufikiria mbele na kujaribu kuona matatizo au ikwazo vinavyo weza kutokea mbeleni. Kama wote mmeamua kuangalia 2010 sawa fanyeni hivyo lakini mta kumbuka maneno yangu. Asanteni.
 
Angalau leo umekubali mwenyewe kuwa wewe ni mpenzi wa chama cha mafisadi ... last time uliambiwa hili ukaruka kimanga ... ohh .... msiniionee...ohh....mimi sina chama..

Come on, watu walishasoma maandishi yako muda mrefu tu wakayajua mapenzi yako kwa chama la kijani. Ndo maana ule ushauri wako feki uliokuwa unautoa hapa kwa wapinzani ulikuwa unapuuziwa.

Ama kweli siku ina masaa 24 ... umevumilia weeee kwenye closet (kibanda ndani ya chumba) lakini uzalendo umekushinda

You got it twisted. Kamwe sija wahi kuficha kwamba mimi siyo supporter wa chama chochote cha upinzani au kuficha kwamba CCM kimekua chama changu tokea utotoni. Ulicho niaccuse wewe safari uliyo pita ni kudai mimi ni mtetezi wa mafisadi na nakumbuka sana post zote za siku hizo.

Kama nilivyo sema kwenye thread mkuu naweka maslahi ya nchi mbele ya chama. Mimi siwezi kushabikia chama kimoja ilimradi tu. Chama siyo mzazi wangu. Ila nita kuwa nami mnafiki kama baadhi ya viongozi kama nita kuwa nahama hama ushabiki wa chama kila tatizo linapo tokea. Leo nihamie chama hiki baadae muone nacho hakifai nihamie kingine tena? Mimi naangalia maslahi ya taifa na kama umesoma baadhi ya post zangu later 2010 mimi namsupport Dr. Slaa kwa moyo wote. Na 2015 kama ata tokea kiongozi mwingine ambae naamini kabisa anaifaa zaidi Tanzania nitamsuppor regardless ya party orientation yangu.
 
You got it twisted. Kamwe sija wahi kuficha kwamba mimi siyo supporter wa chama chochote cha upinzani au kuficha kwamba CCM kimekua chama changu tokea utotoni. Ulicho niaccuse wewe safari uliyo pita ni kudai mimi ni mtetezi wa mafisadi na nakumbuka sana post zote za siku hizo.


mimi napiga mluzi tu hapa ..... hizi propaganda zako zinafaa sana kule redio uhuru.
 
Mkuu Mkandara,

Kwanza nikushukuru kwa majibu yako yasiyo na jazba na papara. Hapa nita jaribu kujibu post ambazo zina weza kujibika na ninazo ona ni waste of time kabisa wala sito jisumbua nazo.

Mkuu najua wajibu wangu kama kijana. Najua fika kwamba mimi ni taifa la leo na si taifa la kesho. hayo naya tambua. Ila pia najua umuhimu wa kupanga mambo. Sizku zote mtu ukifanya kambo fulani lazima uwe na malengo kuwa niki pata kitu nataka kukifanyia nini. Bila mipango tuta kuwa kama mtu anaye taka uongozi lakini akisha pewa huo uongozi hajui cha kufanya na tumeona hili kwa viongozi wetu tu.

Yes 2010 ndiyo hii na wakati ndiyo huu. Sema mimi nachukulia uchaguzi huu tofauti kidogo na wengine. Nachukulia uchaguzi wa 2010 kama battle na uchaguzi wa 2015 kama war yenyewe. Kwamba ndiyo mabadiliko yaweza kutokea mwaka huu lakini kuhakikisha hayo mabadiliko ni ya kudumu lazima kuhakikisha kwamba ushindi utakao patikana mwaka huu unaendelea hadi 2015. Kumbuka mkuu kwamba haswa kwenye jamii zetu tumezoea precedent. Sawa Slaa ata shinda mwaka huu lakini precedent ya ushindi huo utakuwa set 2015 kama ukitokea.

Kumbuka mkuu vijana walio pigania uhuru changamoto yao kubwa haikua kulipatia taifa uhuru tu bali na pia kufikiria "what next". Mimi nimeangalia tu possibilities zote za 2010 na kuanza mapema kujiuliza what next after this year. Labda kwa wenzangu mlio na umri mkubwa zaidi mna haraka zaidi ya kuona kila jambo likifanyika kwa sasa na kwa mkupuo. Kama kijana naangalia pia mbeleni kuhakikisha kwama baadae siji kusimulia kwamba kuna mwaka fulani kwa muda fulani mambo yalikua hivi lakini hatukuweza kudumisha hayp.

Kwa hiyo mkuu don't get me wrong. Sija sema tukate tamaa na kukabidhi tu nchi kwenye mikono ya nyota. Ninacho maanisha mimi ni kwamba kama taifa we lack vision. Kila siku tunaongelea tu leo, leo, leo lakini hatuoni mbali zaidi ya urefu wa pua. Kama ilivyo kuwa kwa vijana wa uhuru changamoto yetu si kumuingiza tu kiongozi tunaye amini ni bora bali kuhakikisha akiingia na yeye ana fanikiwa na si kubadilishana tu uongozi. Ni kuhakikisha kwamba hii ina baki hulka ya wapiga kura wa Tanzania ambao watamchagua kiongozi aliye bora pasipo kujali chama.

Pia nataka pia watu waone mbali zaidi ya Mh. Slaa. Tukumbuke kwamba mwaka huu wengi watamchagua Slaa na si kuchagua chama kama chama. Mh. Slaa hata kuwa mgombea kila mara. Lazima tuangalie mbeleni kwamba baada ya yeye tuna hakikishaje bado tuna pata wagombea walio bora? Au wenzangu baada ya Slaa mna mpango wa kurudi hapa tulipo sasa mpaka "Mesaya" mwingine ata kapo tokea?

Kwa hiyo mkuu kosa langu labda mseme ni kuangalia mbele zaidi kuliko wengine na si kuangalia tu mwaka huu. That is the way I am. Pamoja na kutaka mabadiliko sasa lakini pia tayari naangali ni nchi gani na mimi nita taka kuja kuwa rithisha wanangu. Kumbuka mkuu mzazi hajifanyii kazi mwenyewe bali hufanyia kazi watoto wake na maisha yao ya baadae. Vijana wa uhuru walitupigania hadi sisi. Iweje leo na sisi tusiangalie na huko mbeleni. Binafsi I respect you a lot ndani ya JF na kama nime kukwaza basi nisamehe lakini pamoja na hukumu zote nitakazo pata humu ndani i will stand by my words kwa sababu najua nime yasemea kwa nia nzuri regardless ya majina gani nitaitwa humu ndani.
 
mimi napiga mluzi tu hapa ..... hizi propaganda zako zinafaa sana kule redio uhuru.

Wewe sema utakacho ni fikiri utakavyo. Mawazo yako wewe yata baki kuwa mawazo yako wewe. Nitaendelea kupigania mawazo yangu. Kama unaona una piga mluzi kwangu wala haulazimishwi kujibu post zangu. Unaweza ukakaa pembeni.
 
Kumbukeni kuwa wakati mnajiandaa kujipanga kwa 2015 Rostum na vikaragosi wake tayari wamefanya maandalizi na wameanza kumulika 2020.

Sasa mkuu huoni hapo una tetea hoja yangu bila kujijua? Kama unajua Rostam na vikaragasi wake ndiyo adui na tayari wana fanya maandalizi ya 2010 kwa nini na wewe usi fanye maandalizi ya kuwa counter? Hauoni hapo ndipo tunapo shindwa? Wakati wale tunao waita maadui wakijipanga sisi tunaona ni sahihi kusubiria mpaka wakati huo ufike.
 
Na hata huu tunaupuuzia pia,huyu Mwana FA ndo wale wanaotumiwa kutupotosha tusijadili namna ya kupata viongozi bora (kwa kuiondoa CCM Madarakani),anataka atuaminishe hivyo,anasubiri 2015 ikifika aseme "Tujipange 2020",Tumpuuzie na hii post yake na tu focus ni jins gani Dr.Slaa anaweza akaingia Madarakan na kutuletea Tanzania yenye Neema,Yenye kujali utwala wa sheria na kuwa na nia ya dhati ya kupambana na rushwa.

You really do not know politics do you? Nadhani hii miaka yote umeishi chini ya pango. Dr. Slaa hata shinda kwa mawazo ya kiutopia. Kitu pekee kitakacho mletea ushindi ni watu kujua kwamba kazi si rahisi. Kujua kwamba tunabidi tujipange siyo tu kwa ajili ya leo bali pia kwa ajili ya kesho na kesho kutwa. Hivi umesahau Mrema 1995 pamoja na star power aliyo kuwa nayo nini kili tokea? Mkuu kila kitu katika maisha ni mipango. Kama hautaki kuniamini endelea na mawazo hayo na uchaguzi huu ukiisha nita kupm directly na kukuuliza wewe ulifanya nini kuhakikisha Dr. Slaa anashinda. Na kasoro zote ninazo jaribu kuzionyesha ili zirekebishwe kama zita mcost Dr. Slaa nita kuja kwako tena na kukuuliza tena mipango yako wewe ilienda vipi. I think you are taking this too lightly.
 
You really do not know politics do you? Nadhani hii miaka yote umeishi chini ya pango. Dr. Slaa hata shinda kwa mawazo ya kiutopia. Kitu pekee kitakacho mletea ushindi ni watu kujua kwamba kazi si rahisi. Kujua kwamba tunabidi tujipange siyo tu kwa ajili ya leo bali pia kwa ajili ya kesho na kesho kutwa. Hivi umesahau Mrema 1995 pamoja na star power aliyo kuwa nayo nini kili tokea? Mkuu kila kitu katika maisha ni mipango. Kama hautaki kuniamini endelea na mawazo hayo na uchaguzi huu ukiisha nita kupm directly na kukuuliza wewe ulifanya nini kuhakikisha Dr. Slaa anashinda. Na kasoro zote ninazo jaribu kuzionyesha ili zirekebishwe kama zita mcost Dr. Slaa nita kuja kwako tena na kukuuliza tena mipango yako wewe ilienda vipi. I think you are taking this too lightly.

Haya mawazo yako yanawafaa sana mafisadi wa chama cha mafisadi. Hujachelewa bado kumpelekea Kikwete ili ayaweke kwenye kauli mbiu yake
 

Nadhani wengi mnasahau kwamba kazi si mwaka huu tu. Slaa akifanikia na akashinda bado itabidi yeye na chama chake kiongoze serikali kwa miaka mitano. hamna anaye ongelea nini kifanyike baada ya ushindi kana kwamba kutoka kwa CCM tu ndiyo mwisho wa kazi. Wengi wenu mtasema tukazanie kuona kwanza ushindi wa upinzani lakini mimi ni mtu ninaye penda kuangalia mbele. Ni sawa sawa na kuomba visa ya kwenda kusoma ne bila kufikiria ada utailipaje. Mimi ni wale ambao siyo tu naangalia visa nitaipataje bali ada na mahitaji mengine nita yafanikishaje....kuangalia mbele.

Wengine kinachotupa taabu ni hii dhana ya kufikiri wengine wana lengo moja tu la kuing'oa CCM halafu labda ndio wakae kufikiria la kufanya. Hii dhana inatoka wapi mathalan tuseme Chadema wanakamata madaraka. Unataka kuniambia hawana sera, hawana ilani ya uchaguzi na huyo Dr. Slaa anayataka hayo madaraka bila kujua atayatumiaje. Kwa nini tusisubiri hata hiyo siku atakapozindua kampeni yake atakapotoa vision yake ya anapotaka aifikishe Tanzania.

Wote tunakubaliana kuwa Dr. Slaa ni mtu makini halafu hapo hapo tunamkejeli kuwa anakimbilia kuing'oa CCM bila kupanga atalipeleka wapi taifa. Bila shaka unasahau kuwa tatizo kubwa linalolikabili utawala wetu wa siku zote ni utendaji. Sera na mipango ya CCM zilizo kitabuni kwa mfano sidhani kama ni mbaya kiasi hicho ila tatizo ni uaminifu, utendaji, na uwajibikaji. Mwana CCM anaapa kuwa hatatoa wala kupokea rushwa lakini shuhudia hii vurugu mechi inyoendeshwa kwenye kura za maoni.

Hapana Mwanafalsafa hatuwezi kuvumilia miaka mitano mingine ya Kikwete, hatuwezi kuvumilia miaka mingine mitano ya CCM na hatuwezi kuendelea kuwakumbatia viongozi wabovu na utawala wa kisanii usioheshimu sheria.
 
Wakti ukiwa unasoma primary au sekondary uliwai kufikiria kurudi nyuma darasa moja ili uwe best student kama si wa shule wa wilaya au mkoa au taifa.?

Je unaweza kufikiria kuchukua uamuzi huu wa kumrudisha nyuma mwanao anayekuwa wa kumi darasani ili awe wa kwanza? Wht if ukimrudisha akaendelea kuwa wa kumi au akawa wa nane na si wa kwanza.?
 
Mag3 hebu twende taratibu

Wengine kinachotupa taabu ni hii dhana ya kufikiri wengine wana lengo moja tu la kuing'oa CCM halafu labda ndio wakae kufikiria la kufanya. Hii dhana inatoka wapi mathalan tuseme Chadema wanakamata madaraka. Unataka kuniambia hawana sera, hawana ilani ya uchaguzi na huyo Dr. Slaa anayataka hayo madaraka bila kujua atayatumiaje. Kwa nini tusisubiri hata hiyo siku atakapozindua kampeni yake atakapotoa vision yake ya anapotaka aifikishe Tanzania.

Mkuu hapo ndipo unapo kosea. Hakuna anaye sema Chadema haina sera wala ilani. Kuna ubaya je kudiscuss hayo mambo? Kwani ilani na sera ni siri za chama? Kuuliza swali hakumaanishi jibu hakuna na hapo ndipo wewe unapo kosea. Sawa Chadema wana weza wakawa wamejiandaa (mimi siyo party insider na sija sikia bado hiyo ilani but I'm sure ipo) lakini kumbuka kama kuta kuwa na mabadiliko ni kwenye mfumo na wananchi na siyo chama tu. Kwani hao watakao mpigia kura ni wakina nani? Je tume jaribu kufikiria kuwa majority ya Watanzania wana dhani nini? Au tume fikiria tu majority ya wanaJF wana msupport nani? Kumbuka mkuu mapambano yapo on the ground. JF hai wakilishi Watanzania wote. Ukifikiri Mh. Slaa ata shinda kutokana na support unayo iona humu jukwaani you are wrong.


Wote tunakubaliana kuwa Dr. Slaa ni mtu makini halafu hapo hapo tunamkejeli kuwa anakimbilia kuing'oa CCM bila kupanga atalipeleka wapi taifa. Bila shaka unasahau kuwa tatizo kubwa linalolikabili utawala wetu wa siku zote ni utendaji. Sera na mipango ya CCM zilizo kitabuni kwa mfano sidhani kama ni mbaya kiasi hicho ila tatizo ni uaminifu, utendaji, na uwajibikaji. Mwana CCM anaapa kuwa hatatoa wala kupokea rushwa lakini shuhudia hii vurugu mechi inyoendeshwa kwenye kura za maoni.

Mkuu 1) You are wrong to assume kwamba kila mtu ana mkubali Slaa. Ni attitude hiyo itakayo fanya watu wadhani mtu kasha shinda kumbe kazi bado. Usi generalize mambo. 2) Hakuna ubaya kuuliza ni nini haswa Slaa ata fanya kwa taifa. Au hilo ni kosa? Kumbuka akishinda ni raisi wa Tanzania sasa ukisema hamna haja ya kuuliza what next after kuingoa CCM au kuwaondoa mafisadi hapo nita shindwa kukuelewa. Ina maana wewe mkuu hauangalii mbele zaidi ya CCM kuondoka madarakani tu?

Hapana Mwanafalsafa hatuwezi kuvumilia miaka mitano mingine ya Kikwete, hatuwezi kuvumilia miaka mingine mitano ya CCM na hatuwezi kuendelea kuwakumbatia viongozi wabovu na utawala wa kisanii usioheshimu sheria.

I agree whole heartedly. Lakini jua sija sema wala kushauri kwamba upinzani ufyate mkia uachie uchaguzi. Changamoto ninayp toa mimi ni kwamba kazi ni ngumu kuliko wazaniavyo.
 
Wakti ukiwa unasoma primary au sekondary uliwai kufikiria kurudi nyuma darasa moja ili uwe best student kama si wa shule wa wilaya au mkoa au taifa.?

Je unaweza kufikiria kuchukua uamuzi huu wa kumrudisha nyuma mwanao anayekuwa wa kumi darasani ili awe wa kwanza? Wht if ukimrudisha akaendelea kuwa wa kumi au akawa wa nane na si wa kwanza.?

Don't compare apples and oranges. Uraisi ni cheo kimoja tu. Shuleni mtu ukiwa wa kumi haimaanisha huta endelea na masomo. Kinacho angaliwa ni maksi zako. SO sioni uwiano hapo na mada iliyopo. Mada ni maandalizi. Ina sikitisha kwamba watu hawaja fikiria ni nini kinacho takiwa kufanyika kumpa mgombea wamtakae ushindi bali wanaona moja kwa moja ata shinda. Watu lazima wajifunze kutofautisha hisia zao binafsi na mawazo ya wengine. Yes wewe una weza ukamsupport Slaa, yes mimi naweza kumsupport Slaa ila ume chunguza nini hisia za wapiga kura wa Tanzania? Je una uhakika kila mtu ana mawazo kama yakwako. Fikiria.
 
Back
Top Bottom