2010: Pamoja Tunaweza

mwaka 2005 uligombea ukiwa umehitimu kidato cha sita. Mwaka 2010 bado elimu yako ni hiyo hiyo ya kidato cha sita. Ubungo watakuuliza umeshindwa kumaliza shule yako mwenyewe utawezaje kuleta maendeleo?Mwenzio Nape alikwenda kusoma India baada tu ya uchaguzi. wewe na chadema tu

Hao walosoma wamefanya nini la maana kumzidi Mnyika?
Nchimbi PhD
Chenge LLB,LLM(Harvard)
Prof.Ndulu
Prof.Yule waubalozi Italia
The list goes on...come on its what is in your heart and head man
 
Hao walosoma wamefanya nini la maana kumzidi Mnyika?
Nchimbi PhD
Chenge LLB,LLM(Harvard)
Prof.Ndulu
Prof.Yule waubalozi Italia
The list goes on...come on its what is in your heart and head man

Safari,

Pamoja na madudu waliyofanya hao wasomi wetu lakini isiwe kigezo cha kudharau elimu.

Mimi bado naamini elimu ndio mkombozi wa Mtanzania mmoja mmoja na pia taifa.

Kama mtu anaona ana mapungufu sehemu ni bora akasoma na sasa tuna bahati ya kuwa na OUT.

Muhimu tu ni lengo la kusoma liwe kukusaidia kuziba mapengo yalipo katika utendaji wako na wala sio kuongeza idadi ya vyeti vya kutundika ukutani na kuweka kwenye CV hata kama havikuongezei tija au uwezo wa kufanya kazi zako. Vyeti kama hivyo ni udanganyifu kwako mwenyewe na nchi yako.
 
Ndugu yangu Mnyika tupo pamoja kabisa katika harakati hizi zote na pia nakutakia kila la kheri na pia kwa sasa inatupasa kuwa makini sana pia wewe ni moja ya Nguvu kubwa sana katika CHADEMA. Unaweza yote na pia tupo pamoja kwa kila kitu mkuu wangu
 
Wakati ule sisi tulikwa Survey pale karibu na Chuo Kikuu Dar na pia mara nyingi sana tumewahi kuonana sehemu nyingi. Tupo pamoja sana mkuu wangu
 
tulisema na tunasema na tutasema KILA MWAKA UNAPOINGIA TUNA MIKAKATI KIBAO ILA ANGALIA VITENDO,the bottom line ni MANENO MATUPU HAYAFUNJI MFUPA
 
Umesema ukweli kabisa juu hapo Mnyika na pia itakuwa ni jambo la ajabu sana katika hali kama hii Jk anapaswa kuacha kupokea misaada yao na pia kuwa katika hali hii na pia labda ainapaswa asema ni kwa vipi watafanya ili kuwa na uwanja sawa wa demokrasia.
 
Safari,

Pamoja na madudu waliyofanya hao wasomi wetu lakini isiwe kigezo cha kudharau elimu.

Mimi bado naamini elimu ndio mkombozi wa Mtanzania mmoja mmoja na pia taifa.

Kama mtu anaona ana mapungufu sehemu ni bora akasoma na sasa tuna bahati ya kuwa na OUT.

Muhimu tu ni lengo la kusoma liwe kukusaidia kuziba mapengo yalipo katika utendaji wako na wala sio kuongeza idadi ya vyeti vya kutundika ukutani na kuweka kwenye CV hata kama havikuongezei tija au uwezo wa kufanya kazi zako. Vyeti kama hivyo ni udanganyifu kwako mwenyewe na nchi yako.

Uko sahihi kabisa Ndugu Mwananchi.Mimi nimeongelea kwa context ya Mnyika kuishia Darasa la kumi na nne kamailivyodaiwa hapo awali ingawa sina hakika na hilo labda John afafanue ''Kijiswali hiki''
 
Uko sahihi kabisa Ndugu Mwananchi.Mimi nimeongelea kwa context ya Mnyika kuishia Darasa la kumi na nne kamailivyodaiwa hapo awali ingawa sina hakika na hilo labda John afafanue ''Kijiswali hiki''
Ongelea masuala muhimu sana sio maisha ya watu kama hivi. Ndio sisi tunaanza kuleta haja ya mtazamo wa ajabu jaribu kujikita zaidi kwenye hoja za Mnyika na sio hivi ilivyo
 
Josh,
Labda umepandia njiani katika hoja hii.Mimi napingana na mchangiaji aliyepekenua elimu elimu ya Mnyika.I will keep mum anyway....
 
CCM inatafuta kila aina ya m ianya kujihakikishia ushindi wa kishindo utokanao na uwizi w kura , sasa wanafanya kila juhudi kuziba midomo ya maofisa balozi ili wasikemee uoza wao kwenye uchaguzi mkuu ujao,
 
Hoja ya ukabila huwa inajitokeza, na kwa kweli ni hoja ya kukemewa. Ni ubaguzi ambao Mwalimu Nyerere aliwahi kuuita ni sawa na kula nyama ya mtu. Ndugu wa karibu wa ukabila ni udini, nao huwa unasema semwa. 2005 niligombea na Keenja, ni mchagga. Mimi ni chotara wa kiafrika- baba yangu msukuma wa mwanza, mama yangu ni mpare wa same. Kwa hiyo wakati huo nilipochukua fomu, wapo walioniasa kwamba usigombee kwa kuwa wewe sio mchagga, kwa hiyo wachagga wa ubungo hawatakuunga mkono. Kama ningesikiliza sauti hizo wakati huo, hata ule ushindani wa 2005 ambao mpaka leo umebaki kuwa sehemu muhimu ya historia usingekuwepo. Nikaingia, na kwa kweli ni nikaungwa mkono na watanzania, wa makabila mbalimbali wanaoishi ubungo; wakiwemo wachagga. Sasa tuendelee na mjadala wazi kwa kweli, hiyo ilikuwa 2005; je, 2010 hali imebadilika na kwamba sasa jimbo la Ubungo lina ukabila wa hali ya juu na kwamba makabila mengine yasigombee jimbo hilo ndani ya Mkoa wa Dar es salaam?

Uko sahihi kabisa Mnyika katika hili.

Sio kweli kuwa ili kushinda Ubunge katika jimbo la Ubungo unahitaji kuwa mchagga au kabila jingine lolote. Kuna wengi ambao wameshakuwa wabunge pale na hawakuwa wachagga. Inawezekana sana kuwa Mnyika alipata support kubwa kutoka kwa hao wachagga pia. Hata Keenja hakuungwa mkono na wachaga peke yao.

Kinachohitajika zaidi ni kujua kura ziko wapi, jinsi ya kuziomba na kuzilinda kabla ya uchaguzi. Kila mtu anaeweza kukusikiliza na kukuamini anaweza kukupa kura yake. Perseverance is important katika kufanikisha hili.


Nadhani hoja ya ukabila kwa majimbo ya Dar ni hafifu sana. Maana Jiji hilo lina watu wa kila kabila na wanaishi kwa kuheshimiana kama sehemu nyingi nyingine.

Kwa hiyo changamoto kuu niliokuwa nayo kama mgombea wakati huo ilikuwa si tu kuwaeleza sera zangu nakusudia kufanya nini bali pia kuwabadili mtizamo(mindset/perception) kwamba mgombea hapaswi kugawa fedha. Na kwa kweli mwanzoni ilikuwa ngumu sana, lakini niliamua kabisa kampeni zangu msingi wake mkuu uwe ni kufanya siasa safi na kutoa elimu ya uraia.
Unaweza kuona namna ambavyo vuguvugu hili likuja kukubali; na kwa kweli wakati huo tuliweza kushindana na chama dola, na mgombea aliyekuwa waziri wakati huo akichangiwa na wafanyabiashara wakubwa akigombea kwenye chama chenye tuhuma ya kuchota fedha kifisadi na kuchangiwa na mafisadi.
Pamoja ya kuwa ninakubaliana na kuwa kuna tabia ya BAADHI ya wapiga kura kupenda kuomba pesa kutoka kwa wagombea, vile vile naunga mkono hoja ya Mnyika kuwa sio wote wenye mtazamo wa kuchagua kwa kupewa pesa. Na actually wengi wao hawapendi tabia hiyo. Hawapendi pia kudanganywa, maana ni watu wenye heshima zao na vipesa vidogo vidogo wanaviona kama vinawavunjia heshima tu. Japokuwa kama wengine, hupenda kuonyeshwa kuwa mgombea anawajali pia.

Sina uhakika kuwa katika nchi kama yetu, kuna mtu anaeweza kuwa na pesa za kuhonga watu laki 1 au zaidi, wakaridhika kuwa wamehongwa vya kutosha kuweza kushawishika kutoa kura zao (hata kama hawataki kufanya hivyo).

Kinachoweza kuhakikisha ushindi kwa mgombea yeyote, kwa urahisi, ni kuwa na timu kubwa, yenye ushawishi na uwezo wa kufikia watu wengi na kuwaomba kura/kuwashawishi kwa takwimu za ubora wa mgombea. Watu wengi huamini wanachoona kuliko wanachosikia.

Hoja yangu kuu ndani ya makala yangu; je uamuzi wa kugombea au kutogombea kwa mgombea ambaye tayari anafahamika mbele ya umma nguvu na udhaifu wake; je uwe suala lake binafsi au uhusishe pia maoni ya umma?

Kugombea uongozi kwenye nafasi yoyote kinachohitajika zaidi ni nia, sababu na uwezo wa kushawishi watu wengi kwa muda mfupi pamoja na kuweza kuhakikisha watu unaowashawishi wanabaki kukuunga mkono mpaka mwisho. Maana, wakati ukiwa unawashawishi, wapinzani wako nao wanafanya hivyo hivyo, tena sia ajabu kwa nguvu zaidi.

Kufahamika kwa mgombea kunaweza kuwa moja ya advantages mgombea anazokuwa nazo endapo tu, mgombea huyo anafahamika kwa mazuri zaidi ya wengine wote. Lakini vile vile, unaweza kufahamika sana kwa mambo yasiyo mazuri, na hii ikasababisha kutofaidika na kufahamika huko.

Kitu ambacho kinafaa kufanyika ni kuhakikisha unaonyesha mema yako kadiri unavyoweza, kujali binadamu, kuheshimu utu na kuonyesha kweli kuwa unaelewa mahitaji muhimu (general) ya kila unaetaka akupe kura yake na kutoa majibu ya kweli.
 
Josh,
Labda umepandia njiani katika hoja hii.Mimi napingana na mchangiaji aliyepekenua elimu elimu ya Mnyika.I will keep mum anyway....
Nimekusoma bwana mzee na pia sasa ni wakati mwafaka watu kama nyinyi wote mkaunga mkono watu makini na wagombea makini kama wakina Mnyika na kujitokeza kabisa ili kufanya Tanzania iwe imara kabisa
 
Back
Top Bottom