zitto kabwe

Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe (Zitto Kabwe)
Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe, maarufu kama Zitto Kabwe, ni mwanasiasa kutoka Tanzania kutoka chama cha ACT-Wazalendo. Zitto aliwahi kuwa mwanachama wa Chama Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA) toka mwaka 1992 mpaka 2015 alipoachana na chama hicho.

Zitto ameshika nafasi ya Kiongozi wa Chama ACT-Wazalendo kwa miaka 9, mpaka March 2024 ambapo nafasi hiyo imechukuliwa na Dorothy Semu. Amewahi kuwa Mbunge wa Tanzania kwa vipindi viwili kuanzia 2005 mpaka 2015 akiwakilisha Jimbo la Kigoma Kaskazini.
  1. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Zitto Kabwe: Wasemaji wa Kigoma wakiwa wengi, Bungeni mimi nitapanda juu

    Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametoa wito kwa wananchi wa jimbo la Buhigwe kumchagu Mgombea ubunge wa jimbo hilo Frank Ruhasha ili mkoa wa Kigoma uwe na wabunge wengi jambo ambalo anaamini litamfanya kuacha kuwaza ubunge badala yake afikirie kugombea Urais mbeleni...
  2. Mafyangula

    GE2025 Baba Levo: Inasikitisha sana kumuona kiongozi tuliyemuamini kuwa ni mpinzani anavizia wanaCCM kupiganao picha

    Mgombea Ubunge jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi Baba Levo amesikitishwa na Mpinzani wake kutoka Chama cha ACT Wazalendo, kuomba kupiga picha na baadhi ya Wanachama wa CCM Kwenye Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Mkoani Mwanza. "Inasikitisha sana kumuona kiongozi...
  3. DuaZaMama

    SI KWELI Zitto: CHADEMA hawataki wenyewe kushiriki uchaguzi basi waache chokochoko

    Wakuu Ni kweli kauli hii imetolewa Zitto Kabwe "CHADEMA hawataki wenyewe kushiriki uchaguzi basi waache chokochoko"
  4. R

    GE2025 Zitto: Tukishinda Mahakamani tutapiga jalamba nchi nzima na Tutaitoa CCM Madarakani

    Mgombea Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema chama hicho kitafanya kampeni katika kila kona ya nchi endapo Mahakama Kuu itatoa maamuzi yatakayoruhusu Luhaga Mpina kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho Akizungumza Oktoba 6, 2025 katika mkutano wa...
  5. DuaZaMama

    SI KWELI Zitto Kabwe: Polepole si yupo nje ya nchi Canada sasa ametekwaje Tanzania?

    "Polepole si yupo nje ya nchi Canada sasa ametekwaje Tanzania?" Ni kweli kauli hii imetolewa na Mwenyekiti wa zamani na mgombea ubunge jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe?
  6. R

    GE2025 Zitto: Wananchi Mnaweza kuiondoa CCM Madarakani

    CCM inang'ang'ania madarakani, haitaki kutoka jumlajumla, nyinyi wananchi mnaweza kuiondoa CCM rejareja kwa kuanza na wabunge. Geuzeni uchaguzi huu kuwa ni kura ya maoni, kura ya kutokuwa na imani na CCM kwa kuwachagua wabunge wa ACT Wazalendo, na kule kwenye udiwani madiwani wa ACT Wazalendo"...
  7. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Zitto: CCM inamuogopa Mpina na sababu walikuwa nae ndani ya chama chao

    "Mnajua kwamba tunapambana kwa ajili ya mgombea wetu wa urais, kesi inaendelea. Tunatarajia hivi karibuni tutapata maamuzi, na sisi tumejiandaa kesi itakapokishwa tu. Hata kama zimebaki siku kumi, tutatumia hizo hizo kuendelea kutafuta kura, na tunafahamu Chama cha Mapinduzi kinamuogopa sana...
  8. Waufukweni

    GE2025 Zitto: Tutampigania Mpina hadi atakaporejeshwa, tunaamini Mahakama itatenda haki

    Kiongozi Mstaafu wa Chama cha Act Wazalendo Zitto Kabwe, amesisitiza kuwa chama hicho kimejipanga kikamilifu kupambana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi ujao, kwa lengo la kuhakikisha demokrasia ya kweli inatamalaki nchini. Zitto ameyaeleza hayo Septemba 29, 2025 akiwa Same Mashariki...
  9. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Mwananchi: Zitto ni mbinafsi wa juu lakini Baba Levo ni mtumishi wa wananchi

    Vita ya siasa inazidi kuwa tamu huko jimbo la Kigoma Mjini ======================= Kutoka vijiweni hii ni baadhi ya mijadala ambayo inaendelea kujadiliwa na wananchi wa jimbo la kigoma mjini, kwa kupembua uwezo wa wahombea wao kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Katika mjadala huu amesikika...
  10. Waufukweni

    GE2025 Zitto: Mbunge na Madiwani wa CCM wameshauza Biafra wakidai ilikuwa Mali yao, wamekaa Vikao kazi yao kuuza kila eneo la Wazi

    Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema Jimbo la Kinondoni lina nafasi kubwa ya kuleta mageuzi ya kimaendeleo endapo litaongozwa na Kiongozi mwenye maono ya kweli, na kudai kuwa kwa sasa maeneo mengi yameuzwa ikiwemo Viwanja vya Biafra na ameahidi ACT ikishinda...
  11. W

    GE2025 Kigoma: Zitto aahidi kuwapambania waliovunjiwa nyumba zao mwaka 2023, mtaa wa Machinjioni walipwe fidia

    Zitto kupitia ukurasa wake wa X anaandika; "Katika mazungumzo yangu na wakazi wa Kata ya Machinjioni nilielezwa dhahma iliyowakuta tarehe 17/01/2023 ambapo walivunjiwa nyumba zao kupisha eneo la uwekezaji la KISEZ. Kwa uchungu mkubwa wananchi walinieleza namna wamefukarishwa na Serikali ya CCM...
  12. DuaZaMama

    GE2025 Bwege amshinikiza Zitto kujibu tuhuma za CCM, adai kufukuzwa baada ya uchaguzi wa Oktoba

    Kada wa Chama cha ACT-Wazalendo na aliyewahi kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Seleman Bungura maarufu kama Bwege, akizungumza na kituo cha Mwanahalisi TV leo Septemba 28, 2025, amesema kuwa Zitto Kabwe anatakiwa kujitokeza na kujibu tuhuma zinazodai kuwa yeye ni sehemu ya "CCM B"...
  13. McLaren

    GE2025 Zitto Kabwe ataka mdahalo na washindani wake kwenye jimbo la Kigoma Mjini

    Mgombea wa Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe awaomba Wazee wa Kigoma kuitisha mdahalo baina yake na washindani wake katika jimbo hilo kisha kila mmoja aeleze yale aliyoyafanya katika jimbo hilo. Ameyasema hayo Septemba 26, 2025 kwenye mkutano wake wa...
  14. R

    GE2025 Zitto: CCM Watueleze wamefanya nini Miaka Mitano

    Mgombea wa Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amehoji utendaji wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, akieleza kuwa yeye tayari ameonesha dira (vision) yake kwa Ujiji na kueleza mambo ya msingi yanayopaswa kufanyika ili mji...
  15. Waufukweni

    GE2025 Zitto aulizwa na Wananchi, Kura za "Urais tumpe nani?"

    Mmoja wa wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni wa mgombea ubunge wa Kigoma Mjini kupitia tiketi ya ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, uliofanyika kata ya Buhanda, alimpa changamoto kwa kumuuliza: "Ubunge tukupe wewe, lakini urais tumpe nani endapo chama chenu hakitasimamisha mgombea wa urais?"...
  16. Just Pray

    GE2025 Zitto: Nikishinda Ubunge, kujifungua itakuwa bure

    Mgombea ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, ameahidi kuwa akichaguliwa hakuna mwanamke atakayelipa fedha wakati wa kujifungua. Akizungumza leo katika Kata ya Buhanda, Kigoma, Zitto pia ameahidi kuboresha miundombinu ya barabara za kuunganisha Buhanda na mjini...
  17. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Mwananchi ampiga dongo Baba Levo, ni darasa la saba awezi kuliongoza jimbo Kigoma Mjini, anayefaaa ni Zitto

    Mwananchi kaamua kujisema bila kuogopa kwamba jamaa anajuwi kusoma wala kuandika, na Jimbo la Kigoma Mjini ni jimbo lenye viwanda kwahiyo linamtaka mbunge msomi. Na akaukubali kupiga kura kwa Zitto Kabwe kwamba yeye ni msomi ================ Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kupitia...
  18. upupu255

    GE2025 Mwananchi amwambia Zitto 'Hili jimbo anatakiwa msomi'

    Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kupitia tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameendelea na kampeni zake kwa kutembelea wananchi mtaa kwa mtaa katika Kata ya Buhanda, Kigoma Mjini, akiwahimiza kumpa kura ifikapo Oktoba 29, 2025. Zitto amekuwa akitumia fursa hiyo kueleza sera na mipango...
  19. R

    GE2025 Zitto: ACT ndiyo imeshikilia Ufunguo wa Maendeleo

    Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameahidi kuibua upya Barabara ya Msimba-Ujiji ili kuwaondolea wananchi wa Kata ya Businde changamoto ya kushindwa kufanya safari zao Zitto ameyasema hayo wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Businde...
Back
Top Bottom