uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. Kimbesa11

    Ndo maana wanaume tunakufa haraka imagine Kuna mtu alikuwa haamini Kama uchaguzi upo haamini October tunatiki ndugu yangu unajipa kisukari bure

    Wanaume huwa tuna ubishi wa kitoto sana, huku tunajua kuwa kila kiongoz anaapa kuilinda Katiba ya JMT lakini bado Kuna mwanaume anajidanganya moyoni mwake eti oooh hakuna uchaguzi, oooh form haitachukuliwa Kama ulikuwa na fikra Kama hizi ujue ww ni mgonjwa tayari. Haya Taifa lipo na slogan ya...
  2. K

    GE2025 Yaani Bilion 700 kwa uchaguzi wa CCM! Tunapigwa kweli

    Uchaguzi bila reform ni sawa na u chaguzi wa chama kimoja sasa Bilioni 700 ni za nini hasa
  3. P

    Tuwe wakweli kama nchi tunapitia wakati mgumu na baada ya uchaguzi hali itakuwa mbaya

    Tuukubali ukweli kuwa nahodha ni mchanga sana. Sikiliza kutokuwepo coherence kwa hotuba zake. Angalia wasaidizi wake wa wakaribu angalia waandalizi wa kampeni. Kimsingi tuna safari kubwa. Tuiombee nchi yetu. Ni wazi hakuna maono ya kiuongozi tena. Ni vurugu tupu.
  4. Benson Mramba

    GE2025 Kwa maandalizi ambayo Mama Samia amefanya kwa ajili ya huu Uchaguzi Polepole na agenda zake anahitaji muujiza

    Kuna kitu kinaitwa point of no return it is either you win or loose in the battle field. Live or die hard Mama Samia amesha invest sana kwa ajili ya kampeni za mwaka huu. Asipogombea kwa mfano nani atamfidia gharama zake? It's obvious hawezi kukubali hasara kubwa namna hii. Leo katika kuchukua...
  5. W

    Kumbukizi: Sita walivyotimuliwa TANU kwa kupinga uchaguzi wa chama hicho. Kumbe haya mambo kitambo sana

    Gazeti la Mwafrika mwaka 1958, Oktoba 11 liliandika "WAMEFUKUZWA KATIKA TANU NA MKUTANO MKUU WA MWAKA" Gazeti hilo liliandika Mkutano mkuu wa TANU umemfukuza katika chama Sh. Sulemani Takadiri wa Dar es Salaam, ambaye alijaribu kuingiza chuki ya dini katika siasa siku chache zilizopita...
  6. W

    Baraza la katiba nchini Cameroon limeunga mkono uamuzi wa tume ya uchaguzi wa kumuondoa kiongozi wa upinzani Maurice Kamto katika uchaguzi wa Urais

    Baraza la Katiba la Cameroon limeunga mkono uamuzi wa tume ya uchaguzi ya nchi hiyo wa kumwondoa kiongozi wa upinzani Maurice Kamto katika uchaguzi wa urais wa tarehe 12 Oktoba. Wakati mwanasiasa huyo machachari akiondolewa, Rais Paul Biya mwenye umri wa miaka 92 — ambaye pia alikumbana na...
  7. K

    Hivi kufanya kampeni ni lazima,kwa nini CCM wasisubiri tu mpaka siku ya uchaguzi watu wakawapigie kura

    Niseme kwanza sitoshiriki kupiga kura,lakini naona ni jinsi gani viongozi wanamatumizi mabaya ya pesa,hii gharama ya kuzunguka inchi nzima kwa msafara wa viongozi na wapambe CCM wanashindwa kukaa nyumbani kuokoa gharama halafu wajitokeze tu siku ya kupigiwa na kupiga kura,maana kwa hayo...
  8. Roving Journalist

    GE2025 Tume ya Uchaguzi yaweka wazi ratiba ya Uchukuaji Fomu kwa Wagombea wa Urais na Makamu Rais

  9. Z

    Kwa hali ilivyo ,tungehairisha Uchaguzi kwa mstakabali mwema wa taifa letu.

    Mh POLEPOLE ameshamwaga ugali na mboga kidogo anakaribia kumaliza kabisa kumwaga mboga zote. Wananchi waliyompenda hayati JPM ni kama wanahisi kuna mchezo ulichezeshwa kulingana na taarifa ya Mh POLEPOLE, Wananchi hawa wanaweza kuwa na chuki moyoni isiyoisha. La pili ni kwamba wapinzani wa...
  10. W

    Bashe awaonya Wanasiasa wanaowandanganya Wakulima kuelekea Uchaguzi

    Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amekemea tabia ya baadhi ya watu wanaotafuta kura kwa kukosoa mifumo ya kilimo ikiwemo mfumo wa pamba, BBT (Building a Better Tomorrow) na stakabadhi ghalani, akisema ni hatari kwa ustawi wa sekta hiyo. Akizungumza leo ljumaa, Agosti 8, 2025 jijini Dodoma katika...
  11. M

    Tetesi: Njama ovu kwenye uchaguzi mkuu 2025

    Wanajamvi Huku kwetu Mtaa wa Kigezi Kata ya Buyuni Maeneo ya Chanika jijini Dar es Salaam kuna fomu za kuanzisha vikundi vya Kijamii vinavyoratibiwa na baadhi ya Wana-CCM . Kwa aliyetoa maelezo anasema kuanzishwe vikundi vya kijamii ambapo kila mkaazi wa eneo hili anatakiwa kujiunga kwa kujaza...
  12. Morning Glory1

    Uchaguzi 2025: CcmA vs CcmB vs CcmC.. ..HII NI MAAJABU!!

    Unaambiwa kinyang'anyiro cha uchanguzi wa mwaka huu ni Mama Samia vs Salum Mwalim vs Mpina.. Uchaguzi wa mwaka huu ni zaidi ya futuhi ni zaidi ya cheka tu ni zaidi ya sinema zetu kusema kweli ni vichekesho + comedy...nchi hii inadidimia na bado kuna nyumbu na vyura wa kijani unawasikia wakisema...
  13. M

    Polepole: "Offspring" (mtoto) wa mwanamtandao ambaye ni waziri anazunguka nchi hii kugawa fedha kwa ajili ya uchaguzi wa 2030

    Leo katika mazungumzo yake na wananchi, Polepole ameeleza kuwa wahuni wameanza kuzunguuka nchi hii na kugawa fedha kwa ajili ya uchaguzi wa 2030. Akasema mmoja wa wanaofanya hivyo ni mtoto/offspring wa Mtu mzito sana ndani ya Wanamtandao. Hii ngoma ni hatari sana.
  14. Parabolic

    GE2025 Tume ya Afrika yalaani vikali unyanyasaji wa wapinzani na Wanaharakati Tanzania, yataka haki za binadamu uhuru wa Habari na Mitandao kipindi Uchaguzi

    Tume ya Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Watu (ACHPR), imeeleza wasiwasi wake kwa Tanzania kuhusu kukiuka haki za binadamu, hususani uzimaji wa intaneti wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 2025. Azimio kuhusu Hali ya Haki za Binadamu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...
  15. Mto wa mbu

    GE2025 What a shame, Taifa litapoteza 1 trillion Kwa uchaguzi wa Samia Vs Salum Mwalimu

    Yanayoendelea Tanzania ni aibu kubwa mno. Watu hawana aibu. Ukiangalia nchi jirani unaona kwenye chaguzi zao chama tawala kinachuana na strong opposition leader. Kwa Tanzania Hali ni tofauti, baada ya Samia kujiteua bila kupigiwa kura kuwa mgombea urais, ameenda mbali kwa kuogopa strong...
  16. Z

    GE2025 Mhuni Hasusiwi uchaguzi

    ACT - Wazalendo wamekuja na ujumbe muhimu sana "#MHUNI HASUSIWI KURA" na OKTOBA - LINDA KURA. Ni jumbe kali sana. Napenda kuziwakilisha kwa NO REFORM NO ELECTION, ili tuzijadili hoja hizi mbili kwa kina. Kwani ni takriban miezi 3 mpaka uchaguzi, hatujachelewa kwa jumbe moja au nyingine, meza...
  17. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Jaji Asina: Watendaji wa uchaguzi muithamini dhamana mliyopewa

    Watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Kata wametakiwa kuitambua na kuithamini dhamana waliyopewa ya kusimamia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwenye ngazi hiyo. Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari leo Agosti 06, 2025 alipotembelea na...
  18. B

    Hakuna kuhama mtu chama Akishindwa uchaguzi- Yerico Nyerere

    Kweli nimeamini mwanasiasa akikuambia sasa hivi ni usiku toka nje ukaangalie kama kweli kiza kimetanda Aliyekuwa kada wa CHADEMA Yeriko Nyerere kipindi cha uchanguzi wa ndani wa chama chake hicho cha awali kutafuta mwenyekiti wa chama alikuwa upande wa Freeman Alikuwa na kauli mbiu yake...
  19. peno hasegawa

    Kero za muda mrefu za jimbo la Hai - Kilimanjaro

    1. Mkuu wa Wilaya ya Hai, Hassan Bomboko. 2. Foleni ya magari mto Kikavu. 3. Malori kupita katikati ya mji wa Hai. 4. Polisi Kusimamisha magari usiku kuomba rushwa kwa nguvu.
  20. I

    Walioenguliwa uchaguzi wa ndani kuhamia upinzani na kuteuliwa kuwa wagombea ni kukua kwa demokrasia au udhaifu wa upinzani kukosa wagombea wenye sif?

    Tumeshuhudia uchaguzi ndani ya chama tawala nchini ukitamatika hivi karibuni. Uchaguzi ambao umewaacha/ kuwaengua waliokuwa wabunge katika majimbo mbalimbali. Licha ya rafu katika chaguzi hizo; baadhi ya waliokua wagombea wameingia katika vyama vya upinzani kwenda kupeperusha bendera kupitia...
Back
Top Bottom