uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. DogoWaNjombe

    JamiiForums Tanzania GE2025 Gerson Msigwa: Watanzania wangekuwa hawataki kushiriki Uchaguzi 2025 wasingejitokeza kwenye kampeni

    Msemaji Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amejibu maswali kadhaa wakati wa mahojiano aliyofanya na Kituo cha UTV, leo Jumatatu Oktoba 13, 2025; Mnadhani kwa nini Maandamano yanapangwa Siku ya Uchaguzi? Siamini kama Wananchi...
  2. DogoWaNjombe

    JamiiForums Tanzania GE2025 Gerson Msigwa: Wanaotangaza hakuna Uchaguzi 2025 wanapoteza muda na wanafurahisha genge

    Akizungumza katika mahojiano na Kituo cha UTV, leo Jumatatu Oktoba 13, 2025, Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa anasema: ‘Watanzania wawe na amani, kila kitu kitu kinaenda swa, Oktoba 29 waende wakapige kura, kwa sasa wasikilize wagombea ili ikifika siku hiyo wakafanye maamuzi sahihi.’ Kuhusu...
  3. DogoWaNjombe

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mwanamke wa kwanza kuwania Urais Zanzibar ni katika Uchaguzi wa 2025

    Laila Rajab Khamis Katika historia ndefu ya siasa za Zanzibar, jina la Laila Rajab Khamis sasa limeandikwa kwa herufi kubwa si kwa sababu ya nafasi aliyopewa, bali kwa nafasi aliyoamua kuichukua mwenyewe. Mwaka 2025, Laila amekuwa mgombea pekee wa urais mwanamke visiwani Zanzibar, na wa kwanza...
  4. October 2pm

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mr. Tabasamu usijisahaulishe. Nakukumbusha baada ya uchaguzi kituo kinachofuata ni wewe.

    Mipango yako tunajua hujaisitisha. Kule kujishusha kwako tunajua ulikuwa mtego lakini mtego mabua usioweza kumkamata hata panya. Nakukumbusha tuu baada ya huu uchaguzi kituo kinachofuata ni wewe. Kama unafikiri 2030 utamweka yule kijana wako hilo wazo futa. Nitazame hivihivi ukiniona. Habari...
  5. Mto wa mbu

    JamiiForums Tanzania GE2025 Kulikoni mbona maandamano Yana trend sana kuliko uchaguzi?

    Huyu aliyepanga maandamano siku ya uchaguzi nimpe maua yake Sasahivi kwenye Kampeini za uchaguzi wazungumzaji wote wanazungumzia maandamano tu. Madaraja makubwa kama Tazara,Kuta za majengo ya serikali yameanza kuchorwa SAMIA MUST GO. Hii kwangu sio good sign. Leo hii Samia ni wakuwaambia...
  6. The Watchman

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mgombea urais NCCR-Mageuzi asisitiza 'Asiyetaka kushiriki uchaguzi ni sawa na kuikataa Katiba'

    Mgombea urais wa Chama cha NCCR-Mageuzi ameweka wazi msimamo wake kuhusu umuhimu wa wananchi kushiriki katika chaguzi nchini, akisisitiza kuwa ushiriki katika uchaguzi ni haki ya kikatiba na njia pekee ya kuchochea maendeleo ya taifa. Akiwasilisha mojawapo ya sera zake, mgombea huyo amesema...
  7. DodomaTZ

    JamiiForums Tanzania GE2025 Uhuru wa Habari upo shakani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025

    Malalamiko kuhusu uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania yameongezeka tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu Agosti 28, 2025. Vyombo vya habari vimekuwa vikikabiliwa na vikwazo vingi, ikiwamo kupewa maonyo, kuamriwa kushusha maudhui yasiyoifurahisha Serikali, na hata kufungiwa. Mfano...
  8. kiredio Jr

    JamiiForums Tanzania Mwaka wa uchaguzi, mitihani huwa rahisi au matokeo huboreshwa ili kuvutia wapiga kura.

    Wanafunzi pamoja na jamii huamini kwamba mwaka wa uchaguzi, mitihani huwa rahisi au matokeo huboreshwa ili kuvutia wapiga kura. Je, hii ni kweli? Au ni kasumba isiyo na ushahidi? Wengine huamini kwamba serikali haitaki lawama mwaka wa uchaguzi na matokeo mazuri huongeza mvuto kisiasa. Lakini...
  9. Trainee

    JamiiForums Tanzania Kuna watu wanakusudia kuandamana siku ya uchaguzi: Tupige kura wanaounga mkono maandamano hayo na wanaoyapinga

    Nakusudia maandamano yale yenye lengo la kupinga zoezi la uchaguzi Kama ni hoja watu wametoa hoja zao sana na kama ni elimu watu wametoa elimu ya kutosha juu ya jambo hilo. Sasa tufanye tathmini ndogo hapa kila mtu aoneshe upande wake anaochagua kwamba anaunga mkono au haungi mkono maandamano...
  10. Desierto

    JamiiForums Tanzania GE2025 Huu uchaguzi Raha sana mpaka Kuna wabunge hawahangaiki hata kufanya kampeni majimboni mwao

    Wanazunguka tu na mama mm jimboni kwangu gari ya kampeni imepita tu mara Moja Tena kipindi Rais amekuja. Hamna cha kampeni za mbunge Wala diwani.
  11. Kanali_

    JamiiForums Tanzania Tumekubali kuishi na mchawi ndani?

    Hakuna aliye salama. Kama mzazi wako ni mchawi, usicheke sana unapoona anamaliza majirani. Watakapokwisha ataanza na wewe.
  12. W

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mamlaka ya uwekezaji imesema licha ya Uchaguzi kuendelea lakini Uwekezaji haujapungua

    Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania Gilead Teri amesema hamasa ya wawekezaji kuwekeza nchini imeendelea kuwa kubwa hata katika kipindi ambacho nchi yetu ipo kwenye uchaguzi jambo linaloashiria imani kubwa ya wawekezaji hao kwa serikali. Teri ameyasema...
  13. M

    JamiiForums Tanzania Bado kuna mtu anaamini 29 Sep kuna uchaguzi?

    Kwa hali iliyopo sasa na inayoendelea Nani anaamini bado kuna uchaguzi tu mwaka huu Cc Stuxnet
  14. Mafunzo yote ya Udereva

    JamiiForums Tanzania Nadhani huu ndo uchaguzi Mgumu sana kwa ccm kuwahi kutokea.

    Naona Ccm Kama watatoboa safari hii kurudi ikulu, basi sioni Kama ccm itatoka madarakani kirahisi tena.
  15. Common Folk

    JamiiForums Tanzania Swali kwa JWTZ: Vyombo vya usalama kufanya gwaride mitaani kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi siyo siasa?

    Mbona kozi zingine za majeshi huwa hamfanyii mitaani, huwa mnaenda kwenye maeneo maalumu yaliyojificha mnafanya kozi zenu huko kimya kimya bila kuleta bughudha kwa raia wa kawaida? Kwa nini kipindi hiki cha uchaguzi mkuu mnafanya magwaride mtaani, tena mmeungana majeshi yote, na hiyo yote baada...
  16. Genius Man

    JamiiForums Tanzania GE2025 Vyama vinavyoshiriki uchaguzi bandia vifutwe

    Vyama vinavyoshiriki uchaguzi bandia vifutwe , wagombea wote wa vyama hivyo wakamatwe na kuhojiwa hawatufai. Viongozi wa dini wanao support uchaguzi bandia waondolewe kwenye nafasi zao kushiriki kwenye uovu kwa viongozi hao kunapoteza nafasi ya wao kuendelea kuwaongoza wengine kwenye haki.
  17. M

    JamiiForums Tanzania We politely remind you, Samia usiendelee na Uchaguzi

    Samia itakuwa aibu kwetu na kwako, kama wananchi au askari wako wakikutoa kama mwizi. Kwa heshima, watu wako watakufikishia hizi karibuni kutakuwa na majibizano ya Risasi kama CCM itaacha kuwasikiliza Wananchi na sisi wenye masikio marefu. Tarehe 29, Polisi na Askari wa JWTZ hawatatii amri...
  18. figganigga

    JamiiForums Tanzania Je, Wanajeshi wa Tanzania wameukataa uchaguzi au ni Maigizo?

    Kuna Mwanajeshi kataka Tanzania isifanye uchaguzi. Je, Yupo peke yake au nyuma yake kuna wenzie. Kama katoka hadharani na kisema, huu mwezi wa kumi 2025 utakuwa ni mwezi kona. Anaitwa Kapteni Tesha kutoka Shule ya Anga ya Jeshi. Amesema katafakari sana.. Amesema, "JESHI LICHUKUE NCHI HARAKA...
  19. Emilio Mzena

    JamiiForums Tanzania GE2025 Majina ya watakaosimamia uchaguzi yaachiwa, wengi wao ni walimu

    Mkoa fulani umeachia majina ya watakaosimamia Uchaguzi Mkuu 2025. Wengi wao ni walimu. Watafanya interview kuanzia week inayoanza jumatatu. Oktoba imeanza kuchangamka
  20. L

    JamiiForums Tanzania Kauli za baadhi ya Viongozi kuelekea uchaguzi wa ajabu ni mtaji wa ICC

    Vitisho vya kuua watu 29 Oct 2025 ndio imekua faraja ya Viongozi wa chama tawala Kwa Sasa baada ya kuona Hali ni ngumu na halisi. Wamepoteza matumaini kabisa na hofu imewajaa. Hua najiuliza hivi Hawa Viongozi hua ni Viongozi wa watu ama Ni Viongozi wa kuongozana wao Kwa wao? Mbona hawawajali...
Back
Top Bottom