Mwaka wa uchaguzi, mitihani huwa rahisi au matokeo huboreshwa ili kuvutia wapiga kura.

Mwaka wa uchaguzi, mitihani huwa rahisi au matokeo huboreshwa ili kuvutia wapiga kura.

kiredio Jr

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2024
Posts
1,141
Reaction score
2,096
Wanafunzi pamoja na jamii huamini kwamba mwaka wa uchaguzi, mitihani huwa rahisi au matokeo huboreshwa ili kuvutia wapiga kura.

Je, hii ni kweli? Au ni kasumba isiyo na ushahidi?

Wengine huamini kwamba serikali haitaki lawama mwaka wa uchaguzi na matokeo mazuri huongeza mvuto kisiasa.

Lakini NECTA inawezaje kuathiriwa na siasa? Je, kuna ushahidi wa ukweli juu ya hili? na kama hili ni kweli, je hatuipotoshi elimu? wanafunzi hawapunguzi juhudi kwa matumaini ya kupendelewa?

Au hii ni nadharia tu inayozidi kuaminika bila msingi?

Tuwe wakweli, ushawahi kuona tofauti ya matokeo katika mwaka wa uchaguzi? ni kasumba tu au kuna ukweli ndani yake?
 
Back
Top Bottom