Naibu Katibu Mkuu wa Twariqa Tanzania, Sheikh Haruna Hussein, ametoa onyo kwa aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba na kada wa CCM Humphrey Polepole akimtaka kuacha mara moja kutoa kauli ambazo amedai zinalenga kuchafua viongozi akiwemo Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete...
Mkituchagua chama Makini katika uchgazi mkuu 2025 tutajenga hospitali za kata nchi nzima na kuweka vifaa tiba pamoja na wauguzi, madakitari ili kuwez kuwahudumia watanzania ambapo serikali itagharamia kuwapeleka vijana kwenye vyuo vya nje ya nchi kupata elimu ya afya ili kuja kutoa huduma katika...
"Lakini kabla sijamaliza nataka nimpongeze na naomba msichukie hili, Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuilinda amani ya nchi yetu, Lakini pia nivipongeze vyombo vya ulinzi na usalama, ndugu zangu hawa Jeshi na polisi hawalali, sisi tunakuwa tunalala lakini wao wanakuwa wako macho...
Mgombea urais kupitia Chama cha MAKINI, Ndg. Coaster Kibonde, amesema endapo atapata ridhaa ya kuongoza nchi serikali itaanzisha na kutoa ajia mpya zaidi ya milioni moja kwa vijana wa Kitanzania, nakuwataka vijana kuwapigia kura Oktoba 29, 2025.
Mgombea urais kupitia Chama cha MAKINI, Ndg. Coaster Kibonde, amesema endapo atapata ridhaa ya kuongoza nchi yeye na serikali yake watatoa elimu bure kwa watoto wa kitanzania kuanzia elimu ya chekechea hadi vyuo vikuu.
Ameyasema hayo katika ufunguzi wa kampeni zao leo zilizofanyika Dar es salaam
Ipo wazi sera ya Ujamaa aliyoasisi nyerere ndiyo iliyozaa Chama ovu kisichojua misingi ya demokrasia na kilichojaa rushwa, na udikteta wa kiimla, ni wazi nchi zote zilizokulia katika mifumo ya kijamaa Zina mifumo ya kiimla au kidikteta hasa katika ugawaji wa madaraka,
Pamoja na mazuri yake ila...
Mgombea urais kupitia Chama cha MAKINI, Ndg. Coaster Kibonde, amesema endapo atapata ridhaa ya kuongoza nchi hatopunguza matumizi ya Serikali wala mishahara na posho za watumishi wa umma. Alisema hatua hiyo inalenga kuongeza morali kazini na kuzuia tamaa ya rushwa ambayo mara nyingi huzaliwa...
Wakuu,
Mwanasiasa mkongwe, kada na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbrod Slaa, amekosoa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) akisema hazijikiti kwenye masuala ya msingi yanayowagusa moja kwa moja wananchi.
Akizungumza Septemba 2, 2025 kwa njia ya...
Mwanasiasa mkongwe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mwanadiplomasia, Dkt. Wilbrod Peter Slaa amesema kuwa chadema haipo kwenye uchaguzi wa mwaka huu siyo kwa ajali kwa sababu haina uchu wa madaraka kama kama vyama vingine.
Akizungumza kwa njia ya mtandao na Baraza la Kidigitali...
Mgombea wa Urais kupitia Chama cha Wakulima AAFP, Kunje Ngombale Mwiru akiwa katika muendelezo wake wa kampeni katika Mkoa wa Morogoro kata ya Mvuha ameongea na wananchi wa kata hiyo,
Ametaja maadhi ya vipaumbele vyake moja ni kwamba serikali yake itakuwa ni serikali ya mchaka mchaka mbaka...
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini mkoani Manyara, Flatei Massay ametangaza rasmi kurudi Chama Cha Mapinduzi (CCM) akitokea ACT Wazalendo
Massay alihama CCM wakati wa mchakato wa uteuzi wa wabunge, ambapo jina lake halikurudi katika hatua za awali. Siku chache baadaye alichukua fomu...
Mgombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA), Salum Mwalimu, ameanza ziara yake mkoani Tanga kwa ajili ya kuomba ridhaa ya wananchi kumpa nafasi ya kuongoza taifa katika uchaguzi mkuu ujao.
Akiwahutubia wananchi katika mikutano wa hadhara...
Akiwa kijana wa miaka 31 tu, alishinda Jimbo la Vunjo kwa kishindo cha kura 83%.
Baada ya miaka kupita ikaibuka migogoro ya kisiasa, chama chake kupoteza nguvu, na kimya kizito kilichoacha maswali.
Je, kimya chake ni tamaa iliyokufa, upepo aliokuwa akipima, au mapumziko ya kimkakati?
Bado ana...
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Stephen Wasira amesema wakati wanamuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya Chama Dk. Samia Suluhu Hassan, Watanzania ni mashahidi wa kazi kubwa aliyoifanya katika miaka minne na nusu ya uongozi wake.
Akizungumza Septemba 1,2025 katika...
Mgombea mwenza wa urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amesema miongoni mwa ahadi za chama hicho kwa Watanzania endapo watapata ridhaa ya kuwatumikia, watakwenda kuuhusisha mchakato wa Katiba mpya.
Mchakato huo ulikwama mwaka 2014 kwenye hatua ya kura ya maoni ya Katiba...
Serikali ya Mkoa wa Simiyu, imetoa onyo kwa wanasiasa wanaotumia majukwaa ya kampeni kutoa lugha za kichochezi, kueneza chuki na kuwagawa wananchi kwa misingi ya itikadi, kabila au dini, ikisisitiza kuwa haitasita kuchukua hatua kwa yeyote atakayevuruga amani ya mkoa huo na kwamba wananchi...
MWENYEKITI wa Wazee na mwasisi wa Chama cha NLD, Tozz Mtwanga, amemtaja Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mwanadiplomasia wa kweli.
Amesema katika historia ya Tanzania haijawahi kutokea Serikali kutoa usafiri kwa wagombea wa vyama vya upinzani, lakini chini ya uongozi wa Rais Samia jambo hilo...
Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewakumbusha Watanzania kuhusu ahadi za Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizoziahidi kutekeleza ndani ya siku 100 baada ya kuapishwa endapo atapewa ridhaa ya kuongoza tena nchi.
Amesema hayo...
Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chma cha Demorasia na Maendeleo (CHADEMA)Taifa, Tundu Lissu, imepangwa kusikilizwa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, Septemba 8, 2025 katika hatua ya kusoma hoja za awali.
Taarifa hiyo, iliyotolewa na Wakili Gaston Shundo Garubindi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.