uchaguzi mkuu 2025

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. DuaZaMama

    GE2025 Nchimbi atoa ahadi upanuzi maegesho kivuko cha magogoni pamoja na kigamboni, kudhibiti msongamano

    Mgombea mwenza wa kiti cha Urais kupitia CCM, Balozi Dkt Emmanuel John Nchimbi leo Septemba 28, 2025 ametoa ahadi ya Upanuzi kwenye maegesho ya Kivuko cha Magogoni na Kigamboni Shabaha ikiwa ni kuondoa foleni pamoja na kuboresha huduma katika kivuko hicho. Dkt Nchimbi ametoa ahadi hiyo leo...
  2. DuaZaMama

    GE2025 Kikwete: Wabunge wote wa Pwani bunge lijalo watatoka CCM, hatuko tayari kuchanganya pumba na mchele

    Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho kikwete amesema kuwa anaamini Bunge lijalo wabunge wa Pwani wote watakuwa wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) na pia anaamini hiyo itakuwa Kwa Nchi nzima. Dkt. Jakaya ameyasema hayo Leo Sept 28,2025 Kiwanja Cha Sabasaba Kibaha Mkoani Pwani Kwenye...
  3. DuaZaMama

    GE2025 Baba Levo: Wanasema sijasoma siwezi kuwa mbunge , hizi hoja nazitoa wapi?

    Nimekaa na wagombea wa nafasi za udiwani na nimewaambia siwezi kuomba barabara alafu diwani anaenda kumpa Tarura barabara laini laini,huyo diwani hawezi kunifaa kwenye jimbo langu,na wanasema sijasoma sasa hizi hoja natoa wapi?
  4. W

    GE2025 Kigoma: Zitto aahidi kuwapambania waliovunjiwa nyumba zao mwaka 2023, mtaa wa Machinjioni walipwe fidia

    Zitto kupitia ukurasa wake wa X anaandika; "Katika mazungumzo yangu na wakazi wa Kata ya Machinjioni nilielezwa dhahma iliyowakuta tarehe 17/01/2023 ambapo walivunjiwa nyumba zao kupisha eneo la uwekezaji la KISEZ. Kwa uchungu mkubwa wananchi walinieleza namna wamefukarishwa na Serikali ya CCM...
  5. LICHADI

    GE2025 Mkutano wa CCM Kibaha ni aibu

    Hapa picha ya ndege kuna dala dala za mbagala kawe,kinondoni,almost daladala za mjini kama 100 zimechota watu mjini zimewaleta huku nimejiuliza kibaha hakuna watu
  6. DuaZaMama

    GE2025 Kikwete: Nchi yetu ina umoja na utulivu, maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanapatikana

    "Nchi yetu ina umoja. Nchi yenye makabila 120 wa rangi mbalimbali, waumini wa dini mbalimbali, lakini hakuna ugomvi wa kikabila, hakuna ugomvi wa kidini, wala hakuna ugomvi wa maeneo." - Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete kwenye kampeni Kibaha mkoani Pwani
  7. Cute Wife

    GE2025 Gen Z anayekosoa Uchaguzi na kukubali maandamano, Frida Mikoroti amekamatwa na Polisi lakini mpaka sasa hajulikani alipo

    Wakuu, Binti huyu anayefahamika kwa jina la Frida Mikoroti, amekuwa akikosoa kampeni za uchaguzi mkuu zinazoendelea wakati huu kupitia kurasa za mitandao yake ya kijamii, akiwachana CCM kutokuwa na mpinzani wa kweli lakini pia kutoa ahadi za kipuuzi katika mambo ambayo walipaswa kuwa...
  8. DuaZaMama

    GE2025 Mhagama: Nitashangaa mkienda kuwapigia kura wapinzani

    Wakuu, Huyu anazungumzia wapinzani gani? Kwa maana mimi kwenye uchaguzi huu sioni upinzani wowote Mgombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Peramiho kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jenista Mhagama amesema atawashangaa wananchi wa jimbo la Peramiho wakatao wapigia kura vyama vya upinzani huku...
  9. W

    GE2025 Bwege: Dorothy Semu alikataa kujitoa kugombea Urais kupitia ACT ila wakamlazimisha wakasema watamrudishia gharama zake

    Kada wa ACT Wazalendo Selemani Bungala (Bwege) anaeleza kuwa Mpina alipojiunga ACT yalitokea makundi mawili kwa kuwa Dorothy ndiye aliyepaswa kuwa mgombea kuna watu wakasema Dorthy atolewa na kuna watu walisema abaki lakini mwisho wa siku wakamtoa. "Walimtoa, yeye si alikuwa anakataa...
  10. DuaZaMama

    GE2025 Bwege: Wanasema mkubwa hajambi, nchi hii ukitaka kupata taabu kosoa wakubwa

    Wakuu Bwege anasema Nchi hii, ukitaka kupata taabu, kosoa wakubwa. Wanachotaka ni ujikombe kwao; jambo zuri uwapigie makofi, baya pigie makofi. Ameyasema hayo wakati kifanya mahojiano na Mwanahalisi Tv. "Wanasema mkubwa hajambi, sisi wengine hatuamini tunaamini mkubwa anajamba na anapojamba...
  11. DuaZaMama

    GE2025 Bwege amshinikiza Zitto kujibu tuhuma za CCM, adai kufukuzwa baada ya uchaguzi wa Oktoba

    Kada wa Chama cha ACT-Wazalendo na aliyewahi kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Seleman Bungura maarufu kama Bwege, akizungumza na kituo cha Mwanahalisi TV leo Septemba 28, 2025, amesema kuwa Zitto Kabwe anatakiwa kujitokeza na kujibu tuhuma zinazodai kuwa yeye ni sehemu ya "CCM B"...
  12. DuaZaMama

    GE2025 Mwananchi: Kigoma ina wasomi wengi lakini Bodaboda

    Madereva bodaboda wanaofanya shughuli zao katika eneo la Ujiji, Kigoma, wamelalamikia changamoto ya mikataba inayowakabili, ikiwemo kulazimika kurejesha Sh10,000 kila siku kwa muda wa miezi 18, hali inayokuwa ngumu zaidi wanapopata ajali na kushindwa kuendelea na kazi. Wakizungumza na mgombea...
  13. DuaZaMama

    GE2025 Wasira: Vituo vya afya vilivyojengwa chini Rais Samia ni kama hospitali

    Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, amesema kuwa kwa miaka minne ya uongozi wake, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amefanikisha mambo makubwa, hivyo Watanzania wanapaswa kumrudisha madarakani ili aendelee kuleta maendeleo. Wasira amesema hayo leo, Septemba 27, 2025...
  14. DuaZaMama

    GE2025 Viongozi wa dini wahimizwa kuelimisha matumizi ya mitandao ya kijamii

    Viongozi wa dini wametakiwa kuendelea kuelimisha na kusisitiza umuhimu wa kutumia mitandao ya kijamii hasa kwa vijana ili kuhakikisha inatumiwa katika maslahi ya maendeleo ya Taifa. Kauli hiyo imetolewa na Msemaji wa jeshi la Polisi David Misime wakati wa Mkutano Mkuu wa 54 wa Jumuiya ya...
  15. R

    GE2025 Polisi Kigoma kufanya uchunguzi tuhuma za vitambulisho vya kupiga kura kukusanywa na baadhi ya viongozi wa siasa

    Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma limethibitisha linafanya uchunguzi juu ya tuhuma zinazowahusisha baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaodaiwa kupita mitaani katika Jimbo la Kigoma Kaskazini na kuwalaghai wananchi kukusanya na kuandika namba za vitambulisho vya kupigia kura katika maeneo mbalimbali...
  16. R

    GE2025 Kadogosa awapokea Wanachama 35 Kutoka CHADEMA, UDP, CHAUMMA na ACT-Wazalendo

    Mgombea ubunge Jimbo la Bariadi Vijijini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Masanja Kadogosa amewapokea wanachama kutoka vyama mbalimbali vya upinzani ambao wamejiunga na CCM wakati akinadi sera zake katika Kata ya Sapiwi Wanachama hao wanatoka Chadema, ACT- Wazalendo, UDP pamoja na CHAUMMA...
  17. R

    GE2025 Mgombea Urais CUF awaonya wanaohamasisha Maandamano Oktoba 29, 2025

    Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Gombo Gombo, amewatahadharisha wale wanaohamasisha maandamano siku ya kupiga kura, Oktoba 29, 2025, akisema nia yao ni kuichafua Tanzania huku wao wakiwa salama nchi za nje Gombo ametoa kauli hiyo leo, Jumamosi...
  18. R

    GE2025 Ally Hapi: Rais Samia amejenga Madarasa ambayo yana Vioo na Tiles

    Katibu Mkuu wa Jumuiya ya wazazi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ally Salum Hapi, amesema ukizungumzia yale ambayo yamefanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan katika afya ni mengi sana na kwenye elimu ambapo imejenga shule mbalimbali za msingi na Sekondari. Akizungumza...
  19. R

    GE2025 Ally Hapi: Serikali Itabeba Gharama Matibabu ya Figo, Moyo, Kisukari na Cancer ndani ya siku 100 za Uongozi wa CCM

    Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ally Hapi amesema katika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa wote, changamoto zote zilizopo sasa kuhusiana na bima ikiwemo baadhi ya Maradhi kutotibiwa kwa Bima zitatatuliwa na bima hiyo itaweza kulipiamatibabu kwa magonjwa yote makubwa...
  20. R

    GE2025 Prof. Kitila: Tanzania ni nchi ya Pili kwa Afrika Mashariki kwenye Kupambana na Rushwa

    Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema Tanzania imeendelea kupiga hatua katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi, jambo linalothibitishwa na takwimu za kimataifa. Akizungumza katika Jukwaa la Cafetalk lililofanyika Jumamosi, Prof. Kitila amesema...
Back
Top Bottom