Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa, Ezekiel Mollel naye amechukua fomu ya kuwania ubunge Jimbo la Arumeru Magharibi.
Mollel ambaye pia ni mwalimu amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumapili Juni 29, 2025, na Katibu wa CCM Wilaya ya Arumeru, Kamila Kigosi.
Mbunge wa Igunga anayemaliza muda wake, Nicholaus Ngassa amechukua fomu ya kuwania tena ubunge kwa mara nyingine.
Ngassa amechukua na kuirejesha fomu hiyo leo Jumapili, Juni 29, 2025 kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Igunga, Ebeneza Mainoya.
Mhandisi na kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Jafari Hegga amechukua na kurudisha fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.
Hegga amechukua na kurejesha fomu hiyo leo Jumapili, Juni 29, 2025.
Mbunge wa zamani wa Nyamagana, Lawrence Masha amechukua fomu ya kuwania tena ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza.
Masha amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumapili Juni 29, 2025 na Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana, Deogratias Nakei.
Hakuan mtu nimemshusha vyeo kama gwajima kwa kitendo cha yeye kwenda kuchukua fomu ya ubunge hivi watanzania kweli tutatoka hapa
Nakupa scenario mbili za matukio ya gwajima uone alivyokuwa mtu wa hovyo
Wakati wa utawala wa magufuli likaja sakata la madawa ya kulevya gwajima akatajwa- baada...
Khadija Mfaume Liganga, maarufu kama Dida, ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa anayewakilisha Mkoa wa Mwanza, amechukua fomu kuomba ridhaa ya kuwania nafasi ya Ubunge wa Viti Maalum vya Wanawake kupitia Mkoa wa Mwanza.
Dida ni mwanaharakati mashuhuri wa haki...
Askofu Josephat Gwajima akiwa na walinzi wake aenda kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya WanaCCM kumteua tena kugombea ubunge wa jimbo la Kawe.
======
Ufuatiliaji uliofanywa na JamiiCheck umejiridhisha kuwa kipande cha video kinachomuonesha Askofu Josephat Gwajima akienda kuchukua fomu ya ubunge...
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Burton Mwemba @mwijaku amechukua rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Mvomero mkoani Morogoro kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hatua hiyo imeashiria mwanzo rasmi wa safari yake ya kisiasa katika kuwania nafasi ya Ubunge wa Mvomero...
Salome Sengo Amechukua fomu ya kuwania nafasi ya Ubunge katika jimbo la Lupa
Soma pia: Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kilolo Mh Justin Lazaro Nyamoga mapema June 28 ameanza safari ya kutetea tiketi ya kuwania Ubunge kwa awamu nyingine Jimboni Kilolo Mh Nyamoga baada ya kuchukua fomu katika ofisi za Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kilolo alielekea kanisani kumshukuru Mungu kwa zawadi...
Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Manonga wilayani Igunga, Seif Gulamali amejitosa tena kuchukua fumo ya kuwania nafasi hiyo.
Gulamali amekabidhiwa fomu hiyo leo katika ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Igunga Mkoa wa Tabora na Ebenezer Ole Mainoya, Katibu wa CCM wilayani humo.
Wakuu
Naona jimbo la Kawe watu wanalichangamkia sana.
===
Geofrey Timoth amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Timoth amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumapili Juni 29, 2025 na Katibu wa Vijana CCM Wilaya, Amos Richard. Jimbo hilo...
KAMA N MAPENZI YA MUNGU
SISI WANA YANGA NA SIMBA TUNATAMANI HUYU BWANA APEWE UBUNGE WA HESHIMA JAMANI SIO KWA VIWANGO VILE UWANJANI
KWAKO MAMA YETU
TUNAOMBA SIKIA OMBI LETU
MUNGU IBARIKI TANZANIA
Mbunge wa Jimbo la Ulanga (2020 - 2025), Salim Alaudin Hasham amechukua fomu ya kuwania ubunge wa jimbo hilo akiomba dhamana ya ubunge wa jimbo hilo 2025 - 2030.
Baada ya kuchukua fomu hiyo Salim amesema, “Wana Ulanga wameona kazi nilizofanya kwa miaka mitano, na nimeitikia wito wao wa kutaka...
Vijana wasio na ajira mbona hawajitokezi kuomba ujira UO? Mbona wenye ajira ndio wanao omba ubunge? Kasoro king msukuma ndo Hana ajira maana Hana elimu
Ndugu zangu Watanzania,
Nipo kimya na nimetulia kwa utulivu mkubwa sana huku macho ,masikio na mawazo yangu yote yakiwa yameelekezwa katika kufuatilia kwa kina sana na kwa ukaribu mkubwa sana zoezi la uchukuaji ,ujazaji na urejeshaji wa Fomu za kuwania Ubunge kupitia chama changu cha CCM...
Zoezi la uchukuaji fomu za kugombea nafasi za Ubunge limeanza rasmi ambapo leo June 28 watia nia kutoka sehemu mbali mbali katika Jiji la Dar es salaam wamejitokeza kuchukua fomu hizo.
Siaga Njega ni mmoja kati ya watia nia wa nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Mbagala rasmi leo june 28...
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Arusha, Catherine Magige amechukua fomu kuomba kuteuliwa kugombea ubunge kuwakilisha wanawake kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Soma Pia: Uzi maalum wa wanaotia nia kugombea Ubunge Uchaguzi Mkuu 2025
Catherine amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumamosi, Juni 28, 2025...
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Itilima mkoani Simiyu, Njalu D. Silanga amerudisha fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo hilo katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Itilima jiioni ya leo June 28, 2025
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.