chadema

CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kiasiasa nchini Tanzania ambacho kilianzishwa tarehe 28 Mei 1992 na mwanasiasa mkongwe Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika miaka 1997 hadi 1979.

Mwaka 2000 CHADEMA hakikuwa na mgombea wa Urais. Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa namba tatu kati ya wagombea kumi akapata asilimia 5.88 za kura.

Mwaka 2010 CHADEMA ilipata asilimia 27.1% na mgombea Urais wa chama Wilbroad Peter Slaa na kura 4,627,923 kwa 31.75%.

Hata hivyo CHADEMA imekataa matokeo mengi kutokana na mchakato mzima kuwa mikononi mwa Tume ya Uchaguzi isiyo huru.
  1. Mhafidhina07

    CHADEMA LENGO LENU NI REFORMS AU CHANGES?

    Reform inajumuisha mabadiliko ya kimfumo ambapo sheria,kanuni,utaratibu,watendaji,itikadi na taasisi muundo na vyeo kwa ujumla. Moja ya sababu ya reform ni kutokuwepo kwa usawa wa mfumo na utendekaji kazi,reform mara nyingi inahisisha Changes katika itikadi na imani. Tunaambieni wadau...
  2. M

    Mrema afukuzwe Chadema mara mona

    Huyu mrema alikuwa mpuuzi aliekuwa ananga utawala wa CCM ,ni muda muafaka kwa CDM kufanya maamuzi sahihi wakati sahihi kwa niaba ya Watanzania
  3. Nipe Maji

    PreGE2025 Julius Mwita: CHADEMA lengo lake ni kushika Dola, kunapokuwa na chochote ambacho kinazuia hilo lazima kisemwe

    "Kwenye madhumuni ya uchumi yapo mambo 11, sisi CHADEMA kwenye uchumi inasema matumizi Bora ya rasilimali za Taifa katika kuwafanya Watanzania mmoja mmoja awe na uchumi wa kumuwezesha kuendesha maisha yake. Hayo ndio madhumuni ya kiuchumi ya CHADEMA" "Sisi tunaamini kwamba CHADEMA ni Chama cha...
  4. Waufukweni

    PreGE2025 Julius Mwita: G-55 inataka CHADEMA iende kwenye uchaguzi

    Aliyekuwa Katibu wa Sekretarieti ya CHADEMA, Julius Mwita, amewapongeza Tundu Lissu na John Heche kwa ujasiri wao, akisema ni viongozi wanaoweza kuleta hamasa kubwa wakati wa uchaguzi. Akizungumza kupitia Clouds FM, Mwita amesema; "G- 55 haiwavurugi watu ila watu ndio wanajivuruga, sisi...
  5. C

    Lissu alipaswa kudhibitiwa kabla hajashinda Uenyekiti CHADEMA au figisu zilishindikana?

    Huyu Mwamba alipaswa kutopewa nafasi ya kushinda Uenyekiti CHADEMA. Ni hatari zaidi ya hatari yenyewe. Kichwa kibovu kile kitaleta amsha amsha kuelekea uchaguzi ambayo Sisi Mbogamboga hatuitakagi.
  6. Scared

    PreGE2025 Wapinzani mnataka nini kama mlimpinga Magufuli aliyekuwa anafanya kazi kwa maslahi ya nchi?

    Katika kitu ambacho sikukielewa hapa Tanzania ni kipindi Rais Magufuli alipoingia madarakani wapinzani wakawa wanampinga kwa Kila anachokifanya, kufikia hatua ya Magufuli kuwachukia na sababu ilikua wanampinga maendeleo ya Kila kitu. Akishughulikia mafisadi wanamuita diktekta, mara katili...
  7. K

    Chama cha Mapinduzi Tuepuke Kunasa kwenye Mtego wa Chadema Siku ya Uchaguzi.

    CCM tusije tukanasa kwenye mtego ambao Chadema wanauandaa.Wao wanataka wapiga kura wasijitokeze kupiga kura siku ya uchaguzi. Lakini wanataka kuhamasisha maandamano nchi nzima kama kampeni ya kuzuia uchaguzi hiyo siku ya uchaguzi. Ikitokea vyombo vya ulinzi na usalama vimesambazwa kuzuia...
  8. chiembe

    Makampuni ya simu na mabenki yanayopokea miamala ya chadema, nadhani mmeona kwamba ina nia ya kutumika kwa uhalifu wa uchaguzi, msisaidie uhalifu

    Chadema wanapitishia fedha zao katika Mpesa, airtel money, na huduma za aina hiyo, pamoja na za mabenki. Nitoe angalizo kwa serikali na makampuni hayo kwamba miamala hiyo imeshasemwa na uongozi wa chadema kwamba itatumika kufanyia uhalifu wakati wa uchaguzi. Kampuni ya simu, bora uifungie...
  9. R

    PreGE2025 Chama kile kitaiba kura ya nani ikiwa CHADEMA itasusia na kuandamana siku ya uchaguzi?

    Hellow! Kanuni ya wizi Iko hivi, Ili uibe, lazima wa kuibiwa awepo, na kitu Cha kuibwa kiwepo pia(subject matter). Ni kweli, mwizi akikosa Cha kuiba, anaweza kuvua shati lake, akaliacha pale, akarudi kinyume nyume akajificha, akarudi akinyatia na kuliiba shati lake mwenyewe Ili tu ajifariji...
  10. Mkalukungone Mwamba

    PreGE2025 Joseph Mussa Mahindoni achaguliwa Mwenyekiti mpya wa BAVICHA Dodoma

    Wajumbe wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Cchadema (BAVICHA) Mkoa wa Dodoma, leo tarehe 7 Aprili 2025, wamemchagua Joseph Mussa Mahindoni kuwa Mwenyekiti mpya wa baraza hilo katika uchaguzi uliofanyika katika Ofisi za CHADEMA Kanda ya Kati. Soma Pia: Shangwe la CHADEMA...
  11. Mkalukungone Mwamba

    PreGE2025 Katibu wa CHADEMA kanda ya kati: Tukikosa viongozi ambao si chaguo halali la Watanzania, hatuwezi kupata mabadiliko ya kweli

    Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kati, Ashura Masoud, amewataka wanachama wa CHADEMA wenye maumivu ya uchaguzi kujenga mshikamano badala ya kujitenga au kupinga msimamo wa chama, akibainisha kuwa hatua ya kujitenga ni sawa na kuunga mkono Chama cha Mapinduzi (CCM)...
  12. figganigga

    John Mrema hatujamfukuza CHADEMA. Puuzeni taarifa Potofu

    Siku ya kufukuzwa ikifika mtataarifiwa Habari potofu imeandikwa kwamba Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) imetangaza rasmi kumfuta uanachama Bw. John Mrema. Kwamba hatua hii imefikiwa baada ya kubaini kwamba Bw. John Mrema na kundi lake linalojiita G55 hawana nia njema na...
  13. Allen Kilewella

    PreGE2025 Waliosema hakuna kuhama chama wanataka kuharibu chama CHADEMA

    Wakati wa kampeni ndani ya CHADEMA, kuna baadhi ya watu walikuwa wanawaambia wafuasi wa Lissu kuwa "hakuna kuhama chama" kama wakishindwa uchaguzi ule. Leo hii lile kundi lililokuwa linawaambia wenzao kuwa hakuna kuhama chama, lenyewe ndiyo limo kwenye harakati za kutaka kuharibu chama. Mengi...
  14. MamaSamia2025

    PreGE2025 Kama sio nguvu ya soda Lissu yuko sahihi ila itabidi awachukulie hatua wote walio kinyume na msimamo wa chama

    Nimeona nitoe maoni yangu kuhusu hii fukuza fukuza iliyoanza huko CHADEMA chini ya Tundu Lissu. Ni jambo limeshangaza wengi kwa chama cha demokrasia kukataa maoni tofauti na kutotaka kabisa mjadala kuhusu maamuzi yaliyofanyika. Kwa upande wangu naona Lissu na genge lake la kamati kuu wako...
  15. Erythrocyte

    PreGE2025 Moto wa No Reform No Election waibabua CCM, Masasi yalipuka kwa Shangwe

    Taarifa zingine za leo zinaonyesha kwamba Timu ya Chadema inayotoa Elimu ya Uchaguzi Huru na Haki huko Kanda ya Kusini imefika Masasi. Unaambiwa Moto uliowaka kwenye Mkutano wa Masasi haujawahi kutokea katika kipindi kirefu mno kwenye eneo hilo Kwa kifupi ni kwamba Wananchi wote wameelewa...
  16. Lord Diplock MR

    PreGE2025 Kwa Tundu Lissu ameepuka mpasuko mkubwa zaidi ndani ya CHADEMA

    Wataalamu wa mambo wanasema unapokutana na shetani wawili mbele yako chagua shetani mwenye nafuu, kwa kizungu "choose the lesser evil". Kama CHADEMA ingekubali kushiriki uchaguzi ingeenda kukumbana na mpasuko mkubwa zaidi. Watu hawajui hili baada ya Lissu kushinda uenyekiti wa CHADEMA...
  17. Knock life

    Hoja za G55 naomba wasomi na darasa la saba karibuni tujadili hizi hoja za hawa G55 bila kutumia mihemko ya kisiasa bali mantiki

    Wakuu . G55 wamejinasibu Kama wapo tayari kuongia katika uchaguzi October -2025. Hoja zao ni hizi hapa Endapo Chadema isiposhiriki uchaguzi Mkuu watakosa haki ya wao kuendelea kuwa chama kikuu cha upinzani. Na Endapo wasiposhiriki uchguzi chama kitakosa ruzuku hivyo kitashindwa kujiendesha ...
  18. sinza pazuri

    PreGE2025 Godbless Lema acha mara moja kuingilia uhuru wa Vyombo vya Habari, huo udikteta uchwara uishie CHADEMA

    Watanzania wote tumepigwa na butwaa hii tabia mbaya ya kidikteta inayoota mizizi kwenye chama cha Chadema. Baada ya kuwafunga midomo wanachama wa Chadema wasitoe maoni wala mawazo mbadala kwa kutishia kuwafukuza, kuwapa majina mabaya na kuwanyamazisha. Sasa tunaona kiongozi wa Chadema mpya...
  19. I

    PreGE2025 Olengurumwa: Kama kuna mtu anaendeleza tofauti za uchaguzi ndani ya CHADEMA, atakuwa anafanya kosa kubwa sana

    Mwanaharakati wa Haki za Binadamu, Wakili Onesmo Olengurumwa ameandika andiko kupitia kurasa zake rasmi za mitandao ya kijamii kama maoni yake binafsi kuhusu sakata la wanachadema wanaojitambulisha kama G55, ambao wanakosoa mambo mbalimbali yanayoratibiwa na chadema. #### Nimefuatilia Mjadala...
  20. Stuxnet

    No Reforms No Elections: Kama kweli itatokea ni nini kitawakabili Lissu na CHADEMA

    Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania na sheria za nchi, uchaguzi ni msingi wa demokrasia na haki ya kikatiba (Kwa mfano, Katiba ya Tanzania ya 1977, Kifungu cha 5 na 21). Kutoa vitisho vya "kuharibu uchaguzi" au kuanzisha "uasi" ni uvunjifu wa sheria za Tanzania, kama vile: (1) Kanuni ya Jinai...
Back
Top Bottom